Utapeli mtandaoni: Matapeli wanajuaje namba ya Siri?

Utapeli mtandaoni: Matapeli wanajuaje namba ya Siri?

Nilikuwepo hapo hayo yote yakiendelea. Alitoa simu akampa, yule Kaka akajifanya anapiga then akasema haupatikani akarudisha Simu. Akashuka akisema anaenda maramoja kununua vocha. Asante ntakucheck
Huenda huyo jamaa alimtumia IT man hiyo namba ya mama yako,
 
Mkuu Grena naomba kuuliza maswali mawili.
1. Hiyo simu ni smartphone au hizi za kawaida?
2. Kama ni smartphone, App ya tigopesa imekua istalled na inatumika kwenye simu hiyo?
 
Habari zenu wakuu.

Jana mama yangu katapeliwa hela kutoka TigoPesa. Nilimsindikiza Ubungo mida ya mchana tukapanda basi kwenye ile seat aliyokaa tukamkuta mkaka amekaa dirishani kwasababu mama siti yake ni dirishani na tulikuwa tumewahi sana, akatupisha akasema nawaacha mkae pamoja kidogo mpige story siti yangu ni ya pembeni akaenda siti ya nyuma.

Baadae kidogo akarudi ikabidi niinuke nimpishe akae siti yake. Akamuuliza mama unasalio naomba nipige mama akijua ni msafiri mwenzake akampa simu, akajifanya nampigia hapokei akarudisha Simu, Mara hiyo hiyo akashuka akasema Naenda kununua vocha.

Jioni mama amefika nampigia ananambia yule mkaka hakurudi kwenye bus. Ile siti haikuwa yake alikuja kukaa mtu mwingine, nawaambia siti Ina mtu Hadi konda akaja akasema hii siti sijaikatia ticket.

Nikas-ense something is wrong nikamwambia mama ameshika simu yako na hakurudi kwenye bus kuna kitu kafanya angalia salio lako la TigoPesa. Kweli kuangalia salio limekombwa loooteeee.
Tuliangalia Taarifa ya miamala pesa imetumwa namba 0719169535 na muda uliyotumwa Ni muda ambao Tulikuwa ndani ya bus. Kweli imetuumiza sana

Usalama wa pesa zetu kwenye mitandao ya simu upoje? Hawa wezi wanajuaje namba zetu za siri?

Mimi nimeogopa kwenye simu saivi siachi zaidi ya elfu 5 na kujifanya mwema kumpa Sim mtu nisiyemjua never.

Update: Wakuu kunamdau comment 109 kaeleza vizuri kilichotokea. Ni maengineer wa mitandao wasiowaaminifu wanashirikiana na wezi Kuwapa USSD jinsi ya kutoa fedha. Ukiweka USSD option ya kuweka namba ya Siri inarukwa unatuma tu hela.

Tuweni makini kuwapa watu tusiowajua simu zetu, kujifanya msamaria mwema sometimes unaishia kulizwa.
Basi halina ccctv camera kwani.
Ukimuazima simu mtu mpige picha Kama ni mhalifu atagoma Kama ni kweli ana shida hawezi goma pigwa picha
 
Matapeli hawapumziki.
Screenshot_20210221-190614.jpg
 
Ukimpa au ukiuza smart phone faster badili namba za siri.wajanja wanayo mbinu ya kupitia touch screen wanayo namna ya kuinasa namba ijirudiayo
 
Back
Top Bottom