Utapeli mpya unaohusisha wanasiasa

Utapeli mpya unaohusisha wanasiasa

Leo mchana nilitembelea kwenye ukurasa wangu wa facebook nikaona Mh. Zitto Kabwe ameandika kwenye ukurasa wake kuwa mikopo ya vikoba itawasaidia Watanzania wengi na kumhusisha mh. Rais kuwa ametoa pesa kwa ajili ya kuwasaidia wajasilia mali wadogo wadogo. Pia wameonesha mh. Lowassa akifungua taasisi hiyo katika picha kwenye magazeti ya habari leo na uhuru.

Nimetuma pesa sh. 500,000/- baadaye kidogo wakanipigia kuwa wameipata wanashughulikia mkopo wangu. Aliyepiga kwanza ni mwanaume. Baada ya kama nusu saa akapiga msichana Akaniambia natakiwa nitume 105000/- kwa ajili ya kiingilio kwenye hiyo saccos na mkopo wangu upo tayari na kuwa niitume ili wanitumie huokopo.

Ikumbukwe masharti ya mkopo yalikuwa ni kiasi utakachoweka kama dhamana utapewa mara kumi yake. Na ni kuanzia 500,000/- mpaka 1,000,000/-. Niliwaamini kwa vile Niliona viongozi wakubwa katika nchi hii wamehusika na pia magazeti ya chama na serikali yameonesha mh. Lowasa akifungua hiyo taasisi.

Wamerudi kama nilivyowahi kuleza hapo. Mwenye kuweza kuwasaidia watz afanye hivyo jamani.
 
Aliyetuma Hiyo Post ni Mh Ridhiwani Kikwete kuwa kama Unahitaji Mkopo jiunge na Vicoba Kwa Kutembelea Htt/Vicobatanzania.wapka.mob afu upate maelekezo na jinsi ya Kupatiwa mkopo kwa hiyo mimi Nashindwa kuelewa kuwa ni kweli au ni Utapeli wa watu?
 
Mkuu mbona kila siku Zitto Kabwe kila siku anatoa taarifa kuwa hana na hajawahi kuwa na taasisi inayojihushisha na utoaji wa mikopo kama kuna hela umetoa jua hao ni matapeli
 
Jamaa saizi watakuwa Mwandiga wanakamua BIA hiyo laki tano ha ha haaaah
 
Hapa turudi kwenye somo: Kwa kutumia akili kidogo hasa ukilinganisha na akili zilizotumika kupata hiyo laki 5 haikutakiwa kuwa hivyo. Au kama hizo lk 5 zimepatikana kwa njia kama hiyo.
 
Back
Top Bottom