Ndugu wana JF kuna utapeli mpya umeibuka kupitia sms. Hii imemutokea rafiki yangu hapa ofisini.
Kuna mtu amekuwa akimsumbua kumpigia simu kila siku!! Kufikia jana jioni akwambie mimi naitwa xyz naomba usinisumbue kama unataka kuhakikisha jina langu tuma kwenye hii namba yangu hata 500 ili uone jina langu. Baada ya muda mfupi ujumbe ukaangia kwenye simu yake. Unasema umepokea Kiasi cha Tsh.10000 kutoka kwa (JINA LA MSANII). Jamaa akahamaki na kuamua kumpigia simu huyo bwana akimwambia mbona umetuma hela nyingi hivyo jamaa akasema nilitaka kuangalia jina. Kweli ni wewe nirudishie hiyo pesa. Baada ya hapo jamaa aliyetumiwa pesa akaangalia salio ili airudishe akaona hamna kitu. Kurudi kuisoma hiyo sms iliyoingia kumbe kaituma yeye mwenyewe na sio kwenye kampuni ya simu lakini huo ujumbe umetengenezwa kama umetoka kwa -PESA!! Kwa hiyo kama jamaa yangu angekuwa na salio angeweza kutuma na mwisho wa siku angejikuta ametapeliwa.
UKIONA DALILI KAMA HIZI CHUKUA TAHADHARI.
Kuna mtu amekuwa akimsumbua kumpigia simu kila siku!! Kufikia jana jioni akwambie mimi naitwa xyz naomba usinisumbue kama unataka kuhakikisha jina langu tuma kwenye hii namba yangu hata 500 ili uone jina langu. Baada ya muda mfupi ujumbe ukaangia kwenye simu yake. Unasema umepokea Kiasi cha Tsh.10000 kutoka kwa (JINA LA MSANII). Jamaa akahamaki na kuamua kumpigia simu huyo bwana akimwambia mbona umetuma hela nyingi hivyo jamaa akasema nilitaka kuangalia jina. Kweli ni wewe nirudishie hiyo pesa. Baada ya hapo jamaa aliyetumiwa pesa akaangalia salio ili airudishe akaona hamna kitu. Kurudi kuisoma hiyo sms iliyoingia kumbe kaituma yeye mwenyewe na sio kwenye kampuni ya simu lakini huo ujumbe umetengenezwa kama umetoka kwa -PESA!! Kwa hiyo kama jamaa yangu angekuwa na salio angeweza kutuma na mwisho wa siku angejikuta ametapeliwa.
UKIONA DALILI KAMA HIZI CHUKUA TAHADHARI.