Utapeli mpya jijini dar

Mchaga

JF-Expert Member
Apr 11, 2008
1,378
204
Kuna bwana mmoja miraba minne pandikizi la mtu mwenye lafundi ya kaskazini anazunguka katika mabaa usiku na kutafuta watu wa kuwatapeli.

Ukiwa na marafiki unapata kinywaji huyu bwana anakufuata na kuanza kukuchangamkia kama vile anakujua, baadae atakuuliza wapi anaweza kupata mwanamke.

Baada ya muda atakuonyesha gari yake ni corolla limited nyeupe na kukuambia ndio anaingia kutoka arusha na amekuja dar kufuata mzigo kariakoo, ukiangalia gari yake kweli utaiona imechafuka vumbi/matope. (si kweli kwani wanaipka vumbi/matope).

Baada ya muda atakuuliza wapi anaweza kupata huduma ya intaneti ili aweze kuhamisha pesa zake kwako halafu wewe utoe kiasi cha pesa alichohamisha mtumie kunywa na kutafuta mabibi.

Ukijisahau ukamkubalia na kuingia kwenye gari yake basi unaporwa kila ulichonacho, huyu jamaa mawindo yake ni kinadada na wengine ambao wamelewa....kuweni macho, anazunguka maeneo ya ambiance corner bar na kwingineko jijini dar es salaam.
 
Kuna bwana mmoja miraba minne pandikizi la mtu mwenye lafundi ya kaskazini anazunguka katika mabaa usiku na kutafuta watu wa kuwatapeli.

Ukiwa na marafiki unapata kinywaji huyu bwana anakufuata na kuanza kukuchangamkia kama vile anakujua, baadae atakuuliza wapi anaweza kupata mwanamke.

Baada ya muda atakuonyesha gari yake ni corolla limited nyeupe na kukuambia ndio anaingia kutoka arusha na amekuja dar kufuata mzigo kariakoo, ukiangalia gari yake kweli utaiona imechafuka vumbi/matope. (si kweli kwani wanaipka vumbi/matope).

Baada ya muda atakuuliza wapi anaweza kupata huduma ya intaneti ili aweze kuhamisha pesa zake kwako halafu wewe utoe kiasi cha pesa alichohamisha mtumie kunywa na kutafuta mabibi.

Ukijisahau ukamkubalia na kuingia kwenye gari yake basi unaporwa kila ulichonacho, huyu jamaa mawindo yake ni kinadada na wengine ambao wamelewa....kuweni macho, anazunguka maeneo ya ambiance corner bar na kwingineko jijini dar es salaam.
 
Back
Top Bottom