Utapeli katika kuuza ardhi dar es salaam: tahadhari

Utapeli katika kuuza ardhi dar es salaam: tahadhari

Mokoyo

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2010
Posts
15,145
Reaction score
5,574
Kuna utapeli unaendelea kufanyika katika uuzaji wa maeneo kwa kushirikiana baina ya wauzaji, madalali na serikali za mitaa ambazo zimekosa uadilifu. Mnaonunua maeneo mitaa ya Goba, Kinyerezi, Kibamba, n.k kuweni makini sana. Leo nimeshuhudia ndugu mmoja alikuwa anataka kuuziwa kiwanja huko Goba na jamaa mmoja akisema ni shamba la mkewe lakini jamaa na baadhi ya watendaji wa serikali ya mtaa wakiwepo wakati wakijua wazi kuwa eneo lile lina utata...
 
Yaani mkuu haya matatizo ni mengi sana, cha msingi wakati wa kununua kitu kikishakuwa ni cha mtu mwingine hata kama yuko ulaya ni lazima uamuru aje hapa mwenyewe. Na kama hataweza basi angalao wakati wa mauziano chukua video, mchukue jamaa tu wako simple hata kwa laki mbili anakutolea DVD yenye masuali ya msingi ambapo utakuwa pia unawahoji hao viongozi wa serikali za mtaa. Nina hakika kama kuna ka uongo utaona wakikimbia kuhojiwa tu. Pia kama ni sehemu mtu alinunua mwambie akupe original karatasi ya kununulia eneo husika na ikiwezekana akupeleke kwa muuzaji kama atapatikana. Picha usisahamu mkubwa wangu, ziwekwe. Sema na viranja wakubwa wako Wizara ya Ardhi na Manispaa zetu hasa kama ni eneo muhimu au niseme liko maeneo mazuri.
 
Yaani mkuu haya matatizo ni mengi sana, cha msingi wakati wa kununua kitu kikishakuwa ni cha mtu mwingine hata kama yuko ulaya ni lazima uamuru aje hapa mwenyewe. Na kama hataweza basi angalao wakati wa mauziano chukua video, mchukue jamaa tu wako simple hata kwa laki mbili anakutolea DVD yenye masuali ya msingi ambapo utakuwa pia unawahoji hao viongozi wa serikali za mtaa. Nina hakika kama kuna ka uongo utaona wakikimbia kuhojiwa tu. Pia kama ni sehemu mtu alinunua mwambie akupe original karatasi ya kununulia eneo husika na ikiwezekana akupeleke kwa muuzaji kama atapatikana. Picha usisahamu mkubwa wangu, ziwekwe. Sema na viranja wakubwa wako Wizara ya Ardhi na Manispaa zetu hasa kama ni eneo muhimu au niseme liko maeneo mazuri.

Hahahah unadhani wanaogopa mkuu, hali ni mbaya kuliko mnavyodhania.... maeneo ya mapinga na kerege kuna mtandao unaitwa MUNGIKI yani hao wamepinda mbaya, biashara inafanyikia ofisi ya mtendaji wa kata au wa kijiji na wanakuwepo mwenyekiti na viongozi wengine wa kata na kijiji, afisa mtendaji anawaachia ofisi yeye anatoweka. unafanyiwa biashara vizuriii. siku ukishtuka ukija kwa Mtendaji wa kijiji anakwambia ulitapeliwa anakuonyesha muhuri wake ambao kidogo umetofautiana. hali ni mbaya saaana kuliko mnavyoweza kufikiria.
 
hata hao vijana wa Goba walioko halmashauri ya mtaa ni kama wahuni wahuni Fulani hivi, shamba la mke linauzwa na mume pasipo mke kuwepo ni kinyume na utaratibu, spouse consent is very crucial
Hahahah unadhani wanaogopa mkuu, hali ni mbaya kuliko mnavyodhania.... maeneo ya mapinga na kerege kuna mtandao unaitwa MUNGIKI yani hao wamepinda mbaya, biashara inafanyikia ofisi ya mtendaji wa kata au wa kijiji na wanakuwepo mwenyekiti na viongozi wengine wa kata na kijiji, afisa mtendaji anawaachia ofisi yeye anatoweka. unafanyiwa biashara vizuriii. siku ukishtuka ukija kwa Mtendaji wa kijiji anakwambia ulitapeliwa anakuonyesha muhuri wake ambao kidogo umetofautiana. hali ni mbaya saaana kuliko mnavyoweza kufikiria.
 
Back
Top Bottom