Utajiri wa Kaseja ni ugolikipa tu?

Utajiri wa Kaseja ni ugolikipa tu?

Golota na matumla wamekamatwa ethiopia, mmoja kilo 3 mwingine kilo nne tha thembe. teh teh teh teh!
 
kazi ipo! nielekezeni basi na mie niende nikawe ngamia, naona mapunda yamekuwa mengi!
 
Hahaha,nimecheka sana kwa mjadala huu,hapa mimi mwenzenu ninapita tu jamani,watakuja watu wenye evidence zao wazimwage hapa jamvini.
 
Hivi kila mwenye vijisenti lazima awe Punda au muuza Sembe?

Possibly yes! Kwa maana jinsi uchumi ulivyojengwa mtu mlipa kodi na mwenye kazi ama biashara ya kawaida hawezi kuwa bilionea over night! Lazima transaction zake zileweke. Wanaoweza kuwa matajri design ya wabongo ni fortune winners, mastar wa michezo, inventors kama kina Billy Gates, etc wengine wote lazima historia yake ipande kwa awamu huku ijionekana ni jinsi gani anapanda bila chenga!

Ni umbumbumbu kutokutaka kujua historia ya utajiri wa watu kwa maana hiyo inaathiri utendaji wa nchi na ikiwa watu wanaweza tu kuwa matajiri kama vile magic basi ujue soon or later raia wote attitude zao zitaanza kufikiria in that direction ambapo ku govern nchi itakuwa kazi mno. Hii pia itahatarisha usalama wa Taifa kwani it pays to be "bad" ! Na its costly to be "good" yaani kufanya kazi halali kufuatana na taratibu na sheria tulizojiwekea.

Mine concern ni je serikali na wadau wanajisikiaje mbele ya mataifa kuona kuwa watanzania wanaishi kama vile ghost! Kila kitu chao hakielezeki. Mikataba tunaambiwa ni siri, baadhi ya majina ya wahalifu ni siri ila waiba simu na kuku hiuo siyo siri, mishahara siri! Why siri hizi zisiwekwe wazi ili kila mtu ale chakula chake kwa amani? Amani ni pamoja na kuondoa suspicious way of getting your livelihood!
 
Huyu mkaka ni mwanakandanda tajiri kuliko unamvyomdhania.Je utajiri huu kaupatia kwenye soka tu au kuna siri nyuma ya pazia?
Kwani mtu mpaka aitwe tajiri shurti awe anamiliki nini? Mbona hukutaja hizo mali anazomiliki? Maana isije kuwa ana pesa ya kubadili mboga tu unatoka mbio mpaka jukwaani kumuita mtu tajiri.

Nimeona tutoe angalizo maana mabilionea feki wanazidi kuongezeka siku hizi, utafikiri tuko Arusha bhana.
 
kuuza unga imekuja vipi hapa?mimi nauliza tu,kwani mwanangu anapenda mpira tena ugolie kama kaseja.sasa kashaanza kataa masomo anasema soka la bongo linalipa.natafuta ushahidi wa kumkubalia au kumkatalia.
mpira unalipa kila mwaka juma k juma...ana uhakika wa kukunja mill 40 ili mradi awe na kiwango kizuri...
 
Saiv Tanzania ishaharibiwa jina na ya sembe na pia watu wameshajengewa saikolojia kuwa kila anayetajirika ni sembe. Siwezi kukataa wala kukubali kwan kila lisemwalo lipo. Kama halipo basi laja.
Kwa tetesi nilizozipata ni kuwa usafirishaji wa sembe unakuwa rahisi sana kupitia wachezaji hasa pale timu inaposafiri.
Na kuna tetesi zinazomhusisha manji na hii ishu ya sembe pale timu ya yanga inaposafiri kwenda kufanya mazoezi nje ya nchi.
Saiv kila unapopita mtaani utasikia watu wanahusishwa na sembe kila kona. Ila kama ni ukweli ipo siku yaja na watakamatwa wote kama waliokwisha kunaswa.. but bad enough wanaonaswa ni punda ila wenye mizigo wanazid kubun mbinu mpya..
 
Ha ha ha! Ufreemason na dawa za kulevya vinaenda pamoja. Unajua freemason ni devil worshiper hivyo vitu vyote vya kishetani lazima wafanye!!! Hii ni pamoja na kunywa pombe kupindukia, kuwomanise, kuua etc.
Naona siku hizi hamuwaiti tena ma freemason
 
labda kabla hamjaanza kumchambua ungeweka utajiri wake pengine anaweza asiwe tajiri kabisa kama mnavyomuongelea!!!
 
Nasikia nae ni punda wa ngada.

TUTAWAJUA PUNDA WOTE NA MALI WALIZONAZO... zamu ya punda kutaja wamiliki wao nayoitafuata...
kuna haja ya kwenda TRA tuangalie ulipaji wa kodi wa watu hawa... endelea kutaja listi ni kubwa...
 
Duuuuhh utajiri mkubwa eeeeh au freemason, teheteheteh aliwazalo mjinga ndilo litalomtokea
 
kumiliki bodaboda na bajaji nao ni utajiri kwani wangapi wanavyo hivyo?
 
huyu mkaka ni mwanakandanda tajiri kuliko unamvyomdhania.je utajiri huu kaupatia kwenye soka tu au kuna siri nyuma ya pazia?
we endelea tu kula hela zake nguruwe ukimchunguza humli ,au unataka kumchafua????
 
Kama na wewe ni msomi basi TZ ina safari ndefu. Hivi unakumbuka alilipwa sh ngapi wakati anatua Yanga plus mshahara, then akarudi Simba akalipwa sh ngapi plus mshahara na bonus! Usikimbilie kwenye hitimisho jaribu kushirikisha akili yako kuchanganua mambo.

mkuu,simba alirudi bure..
 
Back
Top Bottom