Umenifungua akili sana mkuu lakin nina tatzo moja uwa navutiwa na kila wazo jema na nataman nifanye kila nalosoma kwa wakati huo ila mpaka sasa sjafanya ata moja
Umenifungua akili sana mkuu lakin nina tatzo moja uwa navutiwa na kila wazo jema na nataman nifanye kila nalosoma kwa wakati huo ila mpaka sasa sjafanya ata moja
*MORNING GREETINGs VIBE*
_Positive Mind Vibe Quotes_
*Usishangae walimwengu kukushangaa kuwa wa tofauti na wao, mana utashangaa na wewe unakuwa kama wao kupoteza muda kujishangaa. Cha msingi wakikushangaa wewe ongeza ukubwa wa hatua wa jambo lako ambalo wanalishangaaa no way out. Nakwambia hivi kwasababu haukuumbwa kuwa wa kawaida*
_Watakwambia maisha ni vita lakini kumbuka maisha ni vita vikubwa sana kama hujajitambua. Hapa namaanisha kutembea katika kusudi la watu wengine ndipo vita utakapoanza kuviona. Lakini ukitembea kwenye kusudi lako utazidi kupata changamoto za kuendelea kujitambua na mafanikio yako_.
*Ukiona maisha yako yanakuwa na majaribu mengi sio kwamba wewe umelaaniwa, kumbuka kuna watu hawapati majaribu kama yako na wanayatamani kwasababu hakuna majaribu ambayo yanaweza kumfuata mtu ambaye hana kitu cha maana ndani yake. Kwa kifupi usipojitambua usishangae kuishi maisha yenye changamoto ambazo baadae zinageuka kuwa matatizo ya kudumu*.
_Maisha yako ni kama kujivalisha miwani za rangi tofauti, ukivaa ya njano kila kitu utakiona cha njano, ukivaa nyekundu utaona vitu vyote vyekundu, ukivaa nyeusi utaona kila kitu cheusi na ukivaa ambayo haina rangi itaonesha vitu katika uhalisia wake, akili yako ndo miwani yako vile unavyofikiria na kusema ndivyo tutakavojua wewe ukoje katika akili yako na hata utakavyoongea tutajua ndani ya akili yako ukoje, ukiwa ni mtu mwenye wivu,majivuno, uongo,usengenyaji,chuki,usaliti n.k inamaana katika akili yako utakuwa umetengeneza maisha ya namna hiyo na ikizidi sana haina haja ya kujiuliza sehemu ingine ilyobaki inanini kwamaana wewe sehemu kubwa ya maisha yako utakuwa huamini katika mazuri ya wengine. Badilisha miwani ya maisha yako na mambo yatabadilika_.
*Nakutakia Siku Njema Msalimie na Rafiki Yako Mwambie Namsalimu Kwa Nia ya kubadili Watu Kifikra Na kimatendo na sio Kimaneno*.
By LAZARO SAMWEL
0753616584 / 0653386586
Subscribe Kupata Masomo Kila siku.
www.lazarosamwel.com