Utahamia lini kijijini?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,107
Reaction score
55,524
Tangu nilipoondoka mjini na kukimbilia huku kijijini, nimekuwa na maisha ya amani na utulivu mkubwa sana.

Nilifanikiwa kupata shamba la ekari nne, ambapo nilijenga kibanda changu cha kujipumzikia pamoja na mama chanja wangu, pia nikachimba na kisima.

Nikaweka uzio wa mimea kuzunguka hilo eneo lote la shamba, ili mifugo yangu isiweze kutoroka hapa na pale.

Nililigawa eneo kwa makundi (A,B,C,D,E) ili kuweka mifugo mabali mbali.

A. niliweka banda la ng’ombe 5 kwa ajili ya kunipa maziwa kila siku

B. niliweka banda la mbuzi 50 kwa ajili ya kubadilisha mboga

C. niliweka banda la kuku wa kienyeji 200 kwa jili ya mayai na nyama

D. nimeweka banda la kitimoto 50 kwa ajili ya nyama

E. bustani ya mboga mboga, nyanya, vitunguu, mchicha n.k

Pia nikaotesha miti ya matunda kama michungwa, papai, parachichi, migomba, miwa n.k

Mabaki/uchafu unaotoka kwenye mifugo, unakuwa unaenda maeneo ya shambani/bustanini na kuboresha uoto wa mimea.

Kwa ujumla, mazingira haya yameniwezesha kuwa na utulivu wa akili, uchumi, na afya bora; magonjwa ya akaili hayatanipata.

Rafiki yangu mmoja, alikuja kunitembelea huku kijijini kwangu; alipofika tu na kusikia miluzi mbalimbali ya ndege ikipiga pambio, akaniambia, ‘’Equation x na mimi sirudi tena mjini.’’

Nikamuuliza kwa nini? akanijibu, ‘’tangu nimekuja huku, akili yangu imetulia kabisa, naokota matunda nakula, mayai nakula nitakavyo, kachumbari najitengenezea, nyama nachoma nitakavyo, Napata hewa safi, ndege wanakuja na kuniimbia nyimbo mbalimbali; kusema kweli naenda kuuza mali zangu zote mjini na mimi nakuja kuhamia huku kijijini.’’

Nikabaki nacheka tu.

Je, wewe, utahamia lini kijijini?
 
Hongera sana mkuu sema naona kila ulichofuga ni kwaajili ya nyama hapo home sijaona ulichosema umefuga kwaajili ya biashara 😃
Kitimoto 50 kwaajili ya nyama, kuku wa kienyeji 200 kwaajili ya nyama mayai, ng'ombe 5 kwaajili ya maziwa na mbuzi 50 kwaajili ya kubadilisha mboga.

Familia yako ni kubwa kiasi gani?
 
CHAI YA BARIDI,
IMEKARIBIA KUGANDA.

Chap chapa nipe consumption ya pumba na maji per day.
Ukiemda chat GBT ukaleta takwim za kupika ntakukamata ambapo hujaeleza kuwa na kibanda cha wafanyakazi, ila umesema ypo wewe na mkeo... wewe na mkeo hamuwez kuhudumia hao wanyama abadan + bustani.

Sasa bosi hao mbuzi, kuku, nguluwe , na ng'ombe ulihitaji kuwa na vijana watatu kama ungefuga kwa mtaji wa vifaa na machine. ... kwakukosa vijana na maelezo thabiti .... Basi hapo umenipa chai.
ni chai tu.
 
Njoo kijijini
 
Maisha bora yapo kijijini
 
Mkuu itakuwa kashajipataaa ndio maana ni yeye na nyama na matunda tuu😀😀😀
 
Kijijini ili uenjoy maisha unahitaji mtaji mzuri mkuu, ukienda kichwa kichwa utateseka, pesa kule si rahisi..
Hayo mabanda ya ng'ombe na 🐄 wenyewe wa5 kuwapata sio mchezo, hapo bado mbuzi 50, kuku 200.

Jiuliz kwanini wa vijijini wengi hawajatobolea maisha wakiwa huko huko?
 
Story hili limeandikwa na CHATGPT..... wadau muonage aibu kuwa watu tunajua chat gpt ikiandika kitu...
 
Umefanya kitu inaitwa manifestation

Yaani unatangulia mbele then ndo unaanza mwanzo .

Wakati nafundisha , nilikuwa nikiitumia Sana hiyo mbinu

Unamwambia Mwanafunzi aandike marks anazotaka azipate kila baada ya session then ukiwapa test or exam inatokea the same au kukaribiana na kile alichokuwa anaandika kila siku
 
Listory lizima kaandika na CHAT GPT ....
 
Wewe story kaandika na CHAT GPT hiyo yote kama mtaalamu wa AI utajua tu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…