Utafiti: Kuku wa kisasa kwenye Manispaa za Ilala na Kinondoni wana kiwango kikubwa cha dawa za kuua Bakteria

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553
Utafiti uliofanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu Cha Muhimbili kwenye machinjio ya kuku ya Shekilango na Manzese umegundua uwepo wa kiwango kikubwa cha dawa za kuua bakteria ambazo wafugaji huzitumia katika kuwatunza.

Watafiti hawa wamebaini uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa ya tetracycline kinachozidi uhitaji wa dozi ya kawaida ya binadamu kwa siku. Aidha, dawa za sulphonamide zimethibitika kuwepo pia kwenye kuku hawa.

Utafiti huu unaibua sintofahamu kubwa kwenye nyakati hizi ambazo dunia inapambana na usugu wa vimelea unaosababishwa na matumizi mabaya ya dawa za antibiotics.

Madhara ya muda mrefu ya kula kuku wenye kiwango kikubwa cha dawa hizi ni kutengeneza jamii yenye watu walio na usugu wa vimelea. Jambo hili huongeza mzigo wa kiuchumi kwa watu, vifo pamoja na kuongezeka kwa ugumu katika kutibu magonjwa ya kawaida yanayosababishwa na bakteria mfano UTI, nimonia, kisonono, Kifua Kikuu pamoja na Kaswende.

Jambo hili linapaswa kuangaliwa kwa tahadhari kubwa kabla halijatela madhara makubwa zaidi kwa kuwa matumizi holela ya dawa za antibiotics kwa wanyama wakiwemo kuku huchangia uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa hizi kwenye nyama na mazao yao mengine yakiwemo mayai.

REJEA
Chapisho: MDPI
Tarehe 8 Septemba, 2022
 
Utafiti uliofanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu Cha Muhimbili kwenye machinjio ya kuku ya Shekilango na Manzese umegundua uwepo wa kiwango kikubwa cha dawa za kuua bakteria ambazo wafugaji huzitumia katika kuwatunza.

Watafiti hawa wamebaini uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa ya tetracycline kinachozidi uhitaji wa dozi ya kawaida ya binadamu kwa siku. Aidha, dawa za sulphonamide zimethibitika kuwepo pia kwenye kuku hawa.

Utafiti huu unaibua sintofahamu kubwa kwenye nyakati hizi ambazo dunia inapambana na usugu wa vimelea unaosababishwa na matumizi mabaya ya dawa za antibiotics.

Madhara ya muda mrefu ya kula kuku wenye kiwango kikubwa cha dawa hizi ni kutengeneza jamii yenye watu walio na usugu wa vimelea. Jambo hili huongeza mzigo wa kiuchumi kwa watu, vifo pamoja na kuongezeka kwa ugumu katika kutibu magonjwa ya kawaida yanayosababishwa na bakteria mfano UTI, nimonia, kisonono, Kifua Kikuu pamoja na Kaswende.

Jambo hili linapaswa kuangaliwa kwa tahadhari kubwa kabla halijatela madhara makubwa zaidi kwa kuwa matumizi holela ya dawa za antibiotics kwa wanyama wakiwemo kuku huchangia uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa hizi kwenye nyama na mazao yao mengine yakiwemo mayai.

REJEA
Chapisho: MDPI
Tarehe 8 Septemba, 2022
Inasikitisha sana..kwa jinsi wakazi wa dsm wanavyobugia hayo ma kuku ya kisasa..kuna hatari kubwa huko mbele.

Elimu izidi kutolewa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Inasikitisha sana..kwa jinsi wakazi wa dsm wanavyobugia hayo ma kuku ya kisasa..kuna hatari kubwa huko mbele.

Elimu izidi kutolewa.

#MaendeleoHayanaChama
Bora dar ukienda Zanzibar wao wana kula sana makuku kutoka nje ya nchi yani Zanzibar nzima hakuna sehemu wanayouza soup ya kuku wa kienyeji wala nyama, yani nyama yao ni ya kuku wa kizungu tu.
 
Utafiti uliofanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu Cha Muhimbili kwenye machinjio ya kuku ya Shekilango na Manzese umegundua uwepo wa kiwango kikubwa cha dawa za kuua bakteria ambazo wafugaji huzitumia katika kuwatunza.

Watafiti hawa wamebaini uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa ya tetracycline kinachozidi uhitaji wa dozi ya kawaida ya binadamu kwa siku. Aidha, dawa za sulphonamide zimethibitika kuwepo pia kwenye kuku hawa.

Utafiti huu unaibua sintofahamu kubwa kwenye nyakati hizi ambazo dunia inapambana na usugu wa vimelea unaosababishwa na matumizi mabaya ya dawa za antibiotics.

Madhara ya muda mrefu ya kula kuku wenye kiwango kikubwa cha dawa hizi ni kutengeneza jamii yenye watu walio na usugu wa vimelea. Jambo hili huongeza mzigo wa kiuchumi kwa watu, vifo pamoja na kuongezeka kwa ugumu katika kutibu magonjwa ya kawaida yanayosababishwa na bakteria mfano UTI, nimonia, kisonono, Kifua Kikuu pamoja na Kaswende.

Jambo hili linapaswa kuangaliwa kwa tahadhari kubwa kabla halijatela madhara makubwa zaidi kwa kuwa matumizi holela ya dawa za antibiotics kwa wanyama wakiwemo kuku huchangia uwepo wa kiasi kikubwa cha dawa hizi kwenye nyama na mazao yao mengine yakiwemo mayai.

REJEA
Chapisho: MDPI
Tarehe 8 Septemba, 2022
Na hawa wataandamwa kama VP
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom