Mtego wa Noti
JF-Expert Member
- Nov 27, 2010
- 2,591
- 1,599
WanaJF, wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu, Tendwa ambaye ni msajili wa vyama vya siasa alitabiri kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu, vyama vya upinzani vitapata viti vingi vya ubunge, jambo ambalo tabibu wa CCM, Makamba alikanusha kwa kumwita tendwa mopokaji na mtu asiyejua anachokiongea. Mara baada ya uchaguzi kuisha, tumeona jinsi wagombea ubunge wengi wa upinzani walivyojitwalia majimbo mengi pamoja na hila za CCM kuiba kura. Sasa hapo nani aliropoka? Makamba au Tendwa? Kwa utabiri huu, tumfananishe Tendwa na Sheikh Yahya Husseni? Nawasilisha!!!!