Puna
JF-Expert Member
- Oct 9, 2013
- 2,770
- 4,856
Baadhi ya mambo ambayo watakumbana nayo endapo Magufuli atashinda ni kama ifuatavyo:-Kwanza watanzania wengi watamkumbuka sana Rais Kikwete. Pili watanzania wengi tutachukiana wenyewe kwa wenyewe hii ni kwa sababu ya hali ngumu ya maisha na hapa tutegemee noti ya sh elfu hamsini maana shilingi yetu itaporomoka mara dufu,kama uhamini ebu angalia shilingi ilivyo wakati tuna raisi mchumi na mawaziri wachumi wenye first class sembuse akija injinia?.Tatu elimu itaporomoka kuliko kipindi chochote kile maana walimu watazidi kudharauliwa na wao kuizika mazima elimu,shule za private zitakuwa na ada maradufu na wenzangu na mie hapa ni kufunga kizazi tu maana hatutaweza kusomesha tena.Nne Afyan itadolola hii ni kutokana na maisha magumu na huduma nazo zitakuwa mbovu hakuna mfano,hapa tutegemee vifo kuongezeka hasa watoto,wazee,wamama na wale masikini,tukumbuke kutenga maeneo ya kutosha ya maziko maana madokta watuua maksudi maana bado wanadai stahiki zao.Hawa madokta na walimu ndo wataimaliza kabisa hii nchi.Tano na mwisho wawekezaji waatahamisha mali kwa kasi ya ajabu sana huku watanzania wakiishia kusoma vichwa vya habari vya magazeti tu na kuisihia kushangaa na kubishana kwenye meza za magazeti si unajaua tena nchi ya wapumbavu na malofa.Amani nchi hii itaendelea kuwepo hakuna wakuvuruga amani na baada ya uchaguzi tutaendelea na yale yale maisha yetu ya kushundia mihongo.Huu ni utabiri wangu msikasirike Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Afrika.
WEWE MTANZANIA MWENZANGU MAAMUZI YAKO NDIO KESHO YAKO AMUA VEMA UPATE MEMA. TAR 25/10/2015.:A S 27:
WEWE MTANZANIA MWENZANGU MAAMUZI YAKO NDIO KESHO YAKO AMUA VEMA UPATE MEMA. TAR 25/10/2015.:A S 27: