Laliga
JF-Expert Member
- Apr 11, 2018
- 286
- 385
Habari zenu wakuu,
Naomba nisiwe na maneno mengi sana, mimi ni mwanafunzi hapa Chuo Kikuu Mzumbe mwaka wa pili. Hapa chuoni kuna usumbufu na kero kubwa zinazo endelea dhidi ya wanafunzi, uongozi wa chuo naona umechoka na wanafanya kazi kwa mazoea na ubabe mkubwa. Kwa mfano, sasa hivi wamegoma kufanyia watu usajili na kuwaambia waahirishe mwaka mpaka mwaka ujao kwa madai ya kwamba wamechelewa kufanya usajili.
Wanaelewa kwamba kuna watu wanalipiwa ada na bodi ya mkopo na kuna wanafunzi wanajilipia ada kupitia boom wanazopewa na bodi lakini bado wameshindwa kuelewa na kufungua usajili kwa ambao hawakua wamefanya usajili hapo mwanzo. Sababu za kuahirisha mwaka au mitihani ziko wazi na zinaeleweka vizuri kwamba, mtu ataahirisha mwaka kama atakua na matatizo ya kiafya au ana matatizo ya kifedha.
Ofisi zote wanatoa jibu moja tu rahisi la 'nakushauri ahirisha mwaka', sasa naahirisa vipi mwaka na ada ninayo? pay in slips ninazo mkononi na mtu anakushauri uahirishe mwaka? huu ni utaratibu wa vyuo vyote Tanzania? Waziri wa elimu, na watu watu wenye mamlaka ya kusaidia wanafunzi waendelee na masomo yao naomba mfike hapa chuoni mlitazame hilo. Wanafunzi ambao hwajasajiliwa ni wengi na muda wa kufanya mtihani umekaribia. Rais Magufuli naomba umulike na hapa chuoni .
Naomba nisiwe na maneno mengi sana, mimi ni mwanafunzi hapa Chuo Kikuu Mzumbe mwaka wa pili. Hapa chuoni kuna usumbufu na kero kubwa zinazo endelea dhidi ya wanafunzi, uongozi wa chuo naona umechoka na wanafanya kazi kwa mazoea na ubabe mkubwa. Kwa mfano, sasa hivi wamegoma kufanyia watu usajili na kuwaambia waahirishe mwaka mpaka mwaka ujao kwa madai ya kwamba wamechelewa kufanya usajili.
Wanaelewa kwamba kuna watu wanalipiwa ada na bodi ya mkopo na kuna wanafunzi wanajilipia ada kupitia boom wanazopewa na bodi lakini bado wameshindwa kuelewa na kufungua usajili kwa ambao hawakua wamefanya usajili hapo mwanzo. Sababu za kuahirisha mwaka au mitihani ziko wazi na zinaeleweka vizuri kwamba, mtu ataahirisha mwaka kama atakua na matatizo ya kiafya au ana matatizo ya kifedha.
Ofisi zote wanatoa jibu moja tu rahisi la 'nakushauri ahirisha mwaka', sasa naahirisa vipi mwaka na ada ninayo? pay in slips ninazo mkononi na mtu anakushauri uahirishe mwaka? huu ni utaratibu wa vyuo vyote Tanzania? Waziri wa elimu, na watu watu wenye mamlaka ya kusaidia wanafunzi waendelee na masomo yao naomba mfike hapa chuoni mlitazame hilo. Wanafunzi ambao hwajasajiliwa ni wengi na muda wa kufanya mtihani umekaribia. Rais Magufuli naomba umulike na hapa chuoni .