Usumbufu kununua voda internet. Kwa nini?

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Habari zenu wanasayansi wa jukwaa hili.
Natumia modem ya Voda Broadband, na baada ya kwisha kwa kifurushi nilichokuwa natumia, nikataka kununua kingine.
Kifurushi nilichohitaji ni namba 4 kwenye menu yao ambayo ni MB150. Nikanunua na ikaja mesj inayosema 'Unable to Provision Subscriber with Service. Please contact customer care'
Nilijaribu tena na tena na mambo yakawa hivyo hivyo......."Unable to......"
Customer care nikajaribu kuingia. Ni yaleyale..... bonyeza 1, 2, 3 nk. Hakuna msaada.
Sasa, wanaTech wa hapa JF, mmeshakutana na hii kadhia? Nifanyeje?
Asanteni.
 
mimi sio mwana tech,ila mimi ikinisumbua nafanya ifuatavyo:chukua hiyo line yako iweke kwenye handset ya simu,then piga *149*01# utaona maelekezo mbalimbali,utaendelea kufuata maelekezo yako hadi ununue kifurushi unachotaka,ila hakikisha hiyo line yako ya voda ina hela inayotakiwa kununua kifurushi unachotaka,utapata ujumbe wa ombi lako kushughulikiwa,then utapata activation message ya kifurushi chako!then rudisha hiyo line kwenye moderm yako,endelea kuperuzi mtandaoooo!vifurushi viko bwelele tena bei rahisi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom