MaxShimba
Platinum Member
- Apr 11, 2008
- 36,008
- 4,093
Na Asha Bani
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemfutia dhamana mwalimu wa madrasa, Mohamed Matimu, anayetuhumiwa kuwalawiti watoto watano.
Mbele ya Hakimu Mkazi Hadija Msongo, Mwendesha Mashitaka Nasoro Siwaya, aliiomba mahakama hiyo kumfutia dhamana mshitakiwa kwa kuwa hayupo tayari kusikiliza ushahidi wa upande wa jamhuri kwa madai ya ugonjwa kila mara.
Mimi sipo tayari kuendelea kusikiliza ushahidi kwa kuwa naumwa sana, alidai mtuhumiwa huyo na hata mwendesha mashitaka alipotaka kuona cheti cha daktari, alieleza kuwa anatumia miti shamba.
Aidha, mwendesha mashitaka huyo, alimwomba hakimu awatizame walalamikaji ambao ni watoto walivyoathirika, huku mtuhumiwa akikwepa kusikiliza ushahidi wa makosa yake kwa hofu ya kukutwa na hatia.
Mabishano kati ya mtuhumiwa na mwendesha mashitaka yalichukua dakika 10 kabla ya hakimu kupitia upya masharti ya dhamana na kuifunga kwa maelezo kuwa zipo dalili za mtuhumiwa huyo kuruka dhamana. Ilidaiwa na mwendesha mashitaka kuwa kati ya Aprili 7 na Juni 10, mwaka jana mtuhumiwa huyo aliwalawiti watoto watano wenye miaka kati ya 8 na 16 na kwamba upande wa mashitaka umekamilisha upelelezi.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemfutia dhamana mwalimu wa madrasa, Mohamed Matimu, anayetuhumiwa kuwalawiti watoto watano.
Mbele ya Hakimu Mkazi Hadija Msongo, Mwendesha Mashitaka Nasoro Siwaya, aliiomba mahakama hiyo kumfutia dhamana mshitakiwa kwa kuwa hayupo tayari kusikiliza ushahidi wa upande wa jamhuri kwa madai ya ugonjwa kila mara.
Mimi sipo tayari kuendelea kusikiliza ushahidi kwa kuwa naumwa sana, alidai mtuhumiwa huyo na hata mwendesha mashitaka alipotaka kuona cheti cha daktari, alieleza kuwa anatumia miti shamba.
Aidha, mwendesha mashitaka huyo, alimwomba hakimu awatizame walalamikaji ambao ni watoto walivyoathirika, huku mtuhumiwa akikwepa kusikiliza ushahidi wa makosa yake kwa hofu ya kukutwa na hatia.
Mabishano kati ya mtuhumiwa na mwendesha mashitaka yalichukua dakika 10 kabla ya hakimu kupitia upya masharti ya dhamana na kuifunga kwa maelezo kuwa zipo dalili za mtuhumiwa huyo kuruka dhamana. Ilidaiwa na mwendesha mashitaka kuwa kati ya Aprili 7 na Juni 10, mwaka jana mtuhumiwa huyo aliwalawiti watoto watano wenye miaka kati ya 8 na 16 na kwamba upande wa mashitaka umekamilisha upelelezi.