WanaJF
Nimekuwa nikijiuliza sipati jibu kuwa hawa vijana wa Lumumba hasa wanaochangia hapa JF. Ni kuwa ni ulevi au ni uwezo mdogo wa kufikiri.Hoja zao wote utafikiri CCM ni chama cha upinzani na CHADEMA ndio chama tawala. Hivi ni kuwa hawaelewi kuitajataja CHADEMA ni kuipa promo zaidi huku mitandaoni kuliko kuiharibia.
Mbinu zao za propaganda haziendani na wakati na sehemu husika, kwa mfano mtu anaandika chadema ni chama cha kaskazini, nicha kidini ooo sijui nani kamchukua mke wa nani. Hivi watu wenye akili wanazidi kuizarau CCM zaidi. Nyinyi nichma tawala andikeni hoja za kuonyesha mmewafanyia nini wananchi sio kutaukana tuu kutwa nzima. Hivi hawana ufahamu wa kuwa waliowengi humu mitandaoni wana elimu ya kiasi fulani huwezi kuwadanganya kijinga hivyo. Akili ya kujua kuwa kuitajataja CHADEMA ni kuipa promo na kuwafanya watu watafiti sana kuhusu hiyo CHADEMA.
Mbinu za propaganda za mwaka 47 ndio mnatumia leo, hii mbunu ya chama cha kikabila cha kidini mnao itumia huku mtandaaoni mnakosea hii kama ndio mwisho wa ubunifu wenu na mnaipenda basi mngeitumia huko vijijini vya remote area kusiko na mawasiliano ambapo mpaka leo hii wanasema Nyerere wa Tanzania ni JK, hao ndio unaweza kuwaambia kuwa CHADEMA ni cha kikabila mkuwapa nchi wataleta vita sio humu humu watu wanaona wenyewe.
Mfano mwingine watu humu mtandaoni wanaona Mwanza nyomi la watu mikutano ya M4C,Iringa nyomi, Kigoma nyomi halafu hapo hapo unakuja na mada CHADEMA chama cha kikanda au watu wachache wahudhuria mkautano wa CDM. Kweli vijana wa Lumumba bado mnadhani watanzania wote ni mabwege poleni.