dfreym
JF-Expert Member
- Oct 14, 2010
- 342
- 87
Ukipata fedha usidharau watu ukajiona wewe ni bora kuliko wasiokuwa nazo,
Ukipata nafasi ya kusoma na usiwaone wale wasiosoma sio kitu, hata kama ni Wazazi wako,
huwezi kujifanya wewe ndo wewe ukawaambia Wazazi wako hawajaenda shule,
kumbuka walinyima wewe uende shule, unapata Mshahara Unakula wote, kisa mshahara hautoshi,
kwa taarifa yako hata wao ulikuwa haitoshi lakini walijipinda usome unaona Kero ukipewa matatizo ya home itakula kwako, we tukana wakunga kimoyo moyo kuwa "wamezidi".
Ukipata Mchumba au hata Boyfriend ama Girl Friend basi usijione wewe ndo Beautiful kuliko Cleopatra, unawaona wenzio wasiopata watu ni "Magume gume".
Ukiolewa wenzio wakikosa bahati usianze nyodo "Siongei na Wasio na Ndoa",
Ukipata kazi sehemu nyingi bora kuliko hapo ulipo, usiondoke na mbwembwe za matarumbeta, hii dunia bwana huwezi jua.
Dharau haziwezi kutupeleka mahali popote, unayemdharau leo hujui kesho yake itakuaje, hapa ni duniani na malipo ni hapa hapa unachopanda ndicho utakachovuana, mbwembwe na majigambo ni utoto wa hali ya Juu ukikua utaacha, Sasa kwanini kufanya dharau sababu ya mafanikio yasiyodumu??
hukuwahi sikia ama kuona watu waliokuwa na nyodo na mbwembwe wazazi wao wakiwa hai ghafla wazazi wakafaraki??
hukuwahi sikia watu waliokuwa wanafanya mbwembwe na kufuru sababu ya wapenzi wao ghafla kikaumana??
hujawahi sikia mtu aliondoka kwenye ofisi moja kwa mbwembwe huko alikokwenda kikanuka??
yangu mimi ni macho, ninarudia kusema Usitukane Wakunga Wakati Uzazi Ungalipo.
Ukipata nafasi ya kusoma na usiwaone wale wasiosoma sio kitu, hata kama ni Wazazi wako,
huwezi kujifanya wewe ndo wewe ukawaambia Wazazi wako hawajaenda shule,
kumbuka walinyima wewe uende shule, unapata Mshahara Unakula wote, kisa mshahara hautoshi,
kwa taarifa yako hata wao ulikuwa haitoshi lakini walijipinda usome unaona Kero ukipewa matatizo ya home itakula kwako, we tukana wakunga kimoyo moyo kuwa "wamezidi".
Ukipata Mchumba au hata Boyfriend ama Girl Friend basi usijione wewe ndo Beautiful kuliko Cleopatra, unawaona wenzio wasiopata watu ni "Magume gume".
Ukiolewa wenzio wakikosa bahati usianze nyodo "Siongei na Wasio na Ndoa",
Ukipata kazi sehemu nyingi bora kuliko hapo ulipo, usiondoke na mbwembwe za matarumbeta, hii dunia bwana huwezi jua.
Dharau haziwezi kutupeleka mahali popote, unayemdharau leo hujui kesho yake itakuaje, hapa ni duniani na malipo ni hapa hapa unachopanda ndicho utakachovuana, mbwembwe na majigambo ni utoto wa hali ya Juu ukikua utaacha, Sasa kwanini kufanya dharau sababu ya mafanikio yasiyodumu??
hukuwahi sikia ama kuona watu waliokuwa na nyodo na mbwembwe wazazi wao wakiwa hai ghafla wazazi wakafaraki??
hukuwahi sikia watu waliokuwa wanafanya mbwembwe na kufuru sababu ya wapenzi wao ghafla kikaumana??
hujawahi sikia mtu aliondoka kwenye ofisi moja kwa mbwembwe huko alikokwenda kikanuka??
yangu mimi ni macho, ninarudia kusema Usitukane Wakunga Wakati Uzazi Ungalipo.