Hapana hiyo ni general thought tu sio sheria
Mara nyingi, mazingira tuliyokulia yanaweza kuwa na mipaka ya kifikra au nafasi finyu za kimaendeleo kulingana na ndoto za mtu.
Ni vema kwenda mbali na nyumbani ulipokulia ili
1.Kupanua Mawazo:
Unapoenda sehemu ngeni, unakutana na watu wapya, tamaduni tofauti, na mbinu mpya za utafutaji ambazo hungezipata ukiwa nyumbani.
2.Kuepuka Mazoea:
Ukiwa nyumbani, ni rahisi kubweteka kwa sababu kuna "neti ya usalama" (familia na marafiki). Ukiwa ugenini, njaa ya mafanikio inakuwa kubwa zaidi kwa sababu unajua huna wa kumtegemea.
3Heshima ya Nyumbani:
Mara nyingi, thamani ya mtu huonekana zaidi akitokea mbali. Nabii hakubaliki kwao, na wakati mwingine mafanikio ya ugenini ndiyo huleta heshima unayostahili nyumbani.
Hata hivyo, si lazima kila mtu ahame, lakini roho ya utafutaji na kutokubali kufungwa na mazingira hayo hayo ni muhimu kwa maendeleo ukuaji na mafanikio