Usipokuwepo, Hakuna Kilichopo!

Unafikiri kuchanganya changanya lugha ili usieleweke kirahisi ndiyo utaonekana una akili.

Kwani ukifa unafikiri uhai unaisha na wewe?

Nafikiri hili ni swali zuri na inaonekana umeelewa, sijajua masuala ya kuchanganya lugha yametoka wapi tena.

Kabla ya wewe kuwepo, bila shaka hukujua kama kulikuwa na uhai. Upo, ndio maana unajua kama kuna uhai. Sina hakika kama kutokuwepo kunaweza kutofautiana. Yani kabla ya kutokuwepo na baada ya kuwepo. Hatukuwa na ufahamu wowote wa uwepo kabla ya kutokuwepo, pengine ndivyo itakavyokuwa hata baada ya uwepo. Hatutapata kitakachoendelea baada ya uwepo wetu (kutokuwepo).

Suala la kuamua kuwa kutakuwa na uwepo baada ya uwepo lipo ndani ya uwezo wetu alimradi tupo. Tusipokuwepo, hatutaweza kwani kabla ya kuwepo hatukuweza, na kimsingi, hakuna kilichokuwepo, hata uwepo wenyewe. Hadi tulipokuwepo ndio tukagundua kulikuwa na uwepo.
 
Umemjibu vizuri maana bado hajui kitu na anatumia akili tu ya kawaida. Kwa Mungu hategemei uwepo wa chochote kile ili Yeye awe Mungu! Mwanzo 6:6-7. Watu wengine wamekuwa wepesi sana wa kuongea mambo wasiyo yajua, hivyo wanapotoka zaidi na kupotosha wengine wasiojua kitu!

Ili awe Mungu, hakika binadamu lazima awepo. Hata sasa wewe unamuona kuwa ni Mungu kwa kuwa upo.

Ningefurahi sana kama ungenipa tafsiri ya hiyo mistari kuliko kuniwekea hapo hivyo. Mimi siamini kwenye ku-quote maandishi ya vitabu hivyo. Ninapenda namna wewe unavyotafsiri maandiko hayo ili kukidhi na kupata namna bora sana ya kuishi inayolinda ubinadamu.
 
ha ha ha! mkuu hapa umeingia pahala pengine! ya mungu mnayajua nyie,ndo maana hata sijamhusisha sorry kwa hilo

Tatizo ni kuwa, ukishaonesha kuwa hutoi nafasi kwa Mungu wa vitabuni, basi nawe unawekwa kwenye kundi la akili ya kawaida. Akili nzuri ni ile inayoamini kuwa kuna Mungu, haswa yule wa kwenye vitabu.
 
Kati wewe na space nani alianza kuwepo.Tuanze hapo

Lazima mimi niwepo kwanza, ili space iwepo. Je, una kumbukumbu yoyote ya kuwepo kwa space kabla ya kuwepo kwako? Kwa kuwa bado upo, unaweza kututhibitishia namna utakavyoendelea kufahamu kuwa kuna space mara baada ya wewe kutokuwepo?
 
Mkuu, siyo kwamba unatumia advantage ya wewe kuwepo ndio maana unaweza kueleza kuwa uwepo ulikuwepo na utaendelea kuwepo?. Kabla ya wewe kuwepo ulifahamu kuwa uwepo ulikuwepo na kwamba utaendelea kuwepo?. Nafikiri unaweza kuyasema haya kwa kuwa upo. Je, kisichokuwepo sasa kinaweza kuelezea uwepo wa sasa na uwepo ujao? Hatuoni kuwa, kwa kisichokuwepo, hakuna kilichopo?
Uwepo hautegemei wewe kuwepo au wewe kuuelezea ndiyo upate hiyo sifa ya kuwa uwepo upo, uwepo ni kama atmosphere, wakati wewe huoni chochote kuna mwenye uwezo wa kuona chochote!

Unajua mwanzisha maada anajaribu kuambatanisha asili isiyo onekana na asili inayo onekana kwa kutumia akili tu ya kawaida ya utashi wake.

Kwa maana uwepo upo kiroho zaidi ndiyo maana mtu anaweza kuwepo mahali fulani kimwonekano tu wa kimwili lakini akawa mahali pengine kabisa kiuwepo.

Na hii ndiyo sababu mwanadamu ni zaidi ya mwili wa damu na nyama. Kama ni msomaji wa vitabu soma kitabu hiki Zaburi 139:16.
 
Kila mmoja wetu ndio chanzo cha uwepo wake mwenyewe (bila kuwepo, huwezi kujua kama upo) na uwepo wa kila kitu. Hivyo, ni muhimu sana kutambua nguvu kuu tuliyo nayo, tujithamini na tuitumie kujenga tafsiri yenye tija tungalipo hapa duniani. Tukiona thamani yetu, ni lazima tuone thamani ya wengine maana nao wana nguvu ya namna hii iliyo na thamani sawa.
Sasa hiyo nguvu unayoiongelea ndiyo chanzo cha huo uwepo wenyewe wa wewe kuwepo, kwa hivyo wewe ulikuwepo hata kabla ya kuwepo katika mwili wa damu na nyama.

Changamoto uliyokuwa nayo hapo kabla na huenda hata sasa bado unayo, ni kutokuwa na elimu ya kujitambua wewe ni nani, chanzo chako ni nini na upo kwa kusudi gani?

Hizi ni baadhi tu ya changamoto za kujitambua ambazo wengi wetu tunaendelea kuzipitia mpaka sasa kwa sababu ni elimu pana mno!
 
ha ha ha! mkuu hapa umeingia pahala pengine! ya mungu mnayajua nyie,ndo maana hata sijamhusisha sorry kwa hilo
Unakimbia kutoa references siyo? Hahaha maisha katika uhalisia wake hayapaswi kuwa katika hali ya kufikirika zaidi bali kwatika uhalisia wake kwa kadiri mtu anavyo boreshwa kiasili.
 
Unakimbia kutoa references siyo? Hahaha maisha katika uhalisia wake hayapaswi kuwa katika hali ya kufikirika zaidi bali kwatika uhalisia wake kwa kadiri mtu anavyo boreshwa kiasili.
nikimbie wapi..?
fikra zako ndo zimekimbia! maana sijamhusisha mungu,nimezungumzia uwepo kama uwepo nawewe umekuja na hiyo ya mungu and then unasema nakimbia! ha ha ha wewe ndo unatakiwa ujitetee tokana na ulichokiandika mi ntajitetea kutokana na nilichoandika.. laiiiini kama mrenda.
 
Tatizo ni kuwa, ukishaonesha kuwa hutoi nafasi kwa Mungu wa vitabuni, basi nawe unawekwa kwenye kundi la akili ya kawaida. Akili nzuri ni ile inayoamini kuwa kuna Mungu, haswa yule wa kwenye vitabu.
si unajua vitu vya kumezeshwa tena.. tatizo wanaamini kabla ya kuelewa
 
si unajua vitu vya kumezeshwa tena.. tatizo wanaamini kabla ya kuelewa
Vyovyote vile utakavyo elezea huwezi kuepuka habari ya Mungu kwenye mambo kama haya yanayohusu asili isiyo onekana kwa damu na nyama, sababu Yeye Ndiye mwanzo wa mambo yote haya, hata dhamiri yako ni shahidi wa hili labda tu uwe na uelewa mdogo juu ya mambo haya.

Sasa ukiulizwa wewe umeyatoa wapi haya unayoyasema? Utasema umesoma kwenye vitabu vya waandishi hasa wale maarufu wa nyakati hizo ama historia, lakini ujue tu wazi hata hao wanafalsafa wenu wanasoma vitabu vinavyo mwelezea Mungu huyu huyu mnayesema Mungu wa kwenye vitabu na kisha wanayaboresha mawazo yao na kuandika hivyo mnavyovisoma nyie mnaojidhania kwamba mnapata uelewa nje ya vitabu hivi vinavyo mwelezea Mungu wa kwenye vitabu.
 
Vyovyote vile utakavyo elezea huwezi kuepuka habari ya Mungu kwenye mambo kama haya yanayohusu asili isiyo onekana kwa damu na nyama, sababu Yeye Ndiye mwanzo wa mambo yote haya, hata dhamiri yako ni shahidi wa hili labda tu uwe na uelewa mdogo juu ya mambo haya.

Sasa ukiulizwa wewe umeyatoa wapi haya unayoyasema? Utasema umesoma kwenye vitabu vya waandishi hasa wale maarufu wa nyakati hizo ama historia, lakini ujue tu wazi hata hao wanafalsafa wenu wanasoma vitabu vinavyo mwelezea Mungu huyu huyu mnayesema Mungu wa kwenye vitabu na kisha wanayaboresha mawazo yao na kuandika hivyo mnavyovisoma nyie mnaojidhania kwamba mnapata uelewa nje ya vitabu hivi vinavyo mwelezea Mungu wa kwenye vitabu.
haya wewe mwenye uelewa mkubwa hebu nionyeshe mungu na utendaji wake wote kabla hatujafika mbali..
 
Ukitaka kuamini alichokisema jamaa hata jf isingekuwepo comments zenu zisingekuwepo hapo juu lazima jf iwepo na nyie ndo mtupie comments. Sema namimi nime mwelewa kwa mbinde
kwahyo asingekuwepo ni kweli jf nayo isingekuwepo?
 
Ndio, usipokuwepo, hakuna kilichopo. Hata Mungu hayupo ikiwa wewe haupo. Ndio maana wapo wanaohoji kwamba kati yako na Mungu, nani wakwanza kuwepo.

Hoja hii inaweza kuwa na mashiko sana. Lazima uwepo ili Mungu awepo. Kwa hiyo, lazima wewe uwepo ili Mungu na kila kitu viwepo.

Ili uwepo uwepo,lazima wewe uwepo. Usipokuwepo, hakuna kilichopo.
kwahyo tukikunyonga leo ukifa na mungu anakua hayupo si ndio
 
According to mtoa mada. Over
Nisipokuwepo, au wewe usipokuwepo, hakuna jamii forums wala chochote, wala Mungu. Kabla ya kuwepo kwako, ulikuwa na kumbukumbu yoyote ya kuwepo kwa chochote? Hapana. Kwa hiyo hakuna kilichokuwepo hadi ulipokiwepo, siyo?
 
kwahyo tukikunyonga leo ukifa na mungu anakua hayupo si ndio

Kwa kuwa sina ushahidi wowote wa kuwepo kwa Mungu kabla ya mimi kuwepo, halikadhalika, nisipokiwepo, Mungu hatakuwepo pia.

Unaweza kuuliza ama kujiuliza, lakini baada ya kuwepo si nimegundua kuwa Mungu alikuwepo tangu enzi na enzi? Kuijua enzi na kujua kuwa Mungu alikuwepo, kunahitaji uwepo wako. Kwa hiyo, ili vitu viwepo, lazima kwanza wewe uwepo.
 
Vyovyote vile utakavyo elezea huwezi kuepuka habari ya Mungu kwenye mambo kama haya yanayohusu asili isiyo onekana kwa damu na nyama, sababu Yeye Ndiye mwanzo wa mambo yote haya, hata dhamiri yako ni shahidi wa hili labda tu uwe na uelewa mdogo juu ya mambo haya.

Sasa ukiulizwa wewe umeyatoa wapi haya unayoyasema? Utasema umesoma kwenye vitabu vya waandishi hasa wale maarufu wa nyakati hizo ama historia, lakini ujue tu wazi hata hao wanafalsafa wenu wanasoma vitabu vinavyo mwelezea Mungu huyu huyu mnayesema Mungu wa kwenye vitabu na kisha wanayaboresha mawazo yao na kuandika hivyo mnavyovisoma nyie mnaojidhania kwamba mnapata uelewa nje ya vitabu hivi vinavyo mwelezea Mungu wa kwenye vitabu.

Tatizo moja kubwa la mnaotumia maandiko ya vitabu vya dini, mnayatumia kama katiba. Hakuna kuwaza kuhusu tafsiri ya maandiko na namna yanavyokidhi mazingira, tamaduni, hali na wakati. Ndio maana kwa utaratibu huu, maandiko yanapingana tu. Jizoeshe kutafsiri maandiko badala ya kucopy tu na kupaste mistari.
 
Back
Top Bottom