Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,876
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza kuanza kutumia sheria katika kutoa adhabu kwa wale wote watakaokaidi kutoa au kudai risiti kwa kuwa wamekuwa wakichangia upotevu wa mapato ya Serikali hali inayodidimiza uchumi na kukosa maendeleo ya nchi.
Kamishina Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata ametoa taarifa hiyo, katika mkutano TRA na walipakodi jijini Arusha wakiwemo wafanyabiashara pamoja na wakuu wa taasisi mbalimbali.
"Kuanzia sasa tutatumia sheria zetu kutoa adhabu kali kwa wale wasiotoa risiti ni vizuri tuwe na utamaduni wa kudai risiti kwani endapo utabainika itachukuliwa hatua kali,"amesema.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela akizugumza katika mkutano huo, amewataka wakazi wa Mkoa wa Arusha kushirikiana katika kufichua biashara ya bidhaa bandia ambazo zimekuwa zikichangia kudidimiza uchumi .
"Bado mkoa wetu unatumika kama daraja la bidhaa za kughushi kwa hiyo sisi kama Mkoa wa Arusha tunatakiwa kushirikiana na kuendelea kuhamasisha kuepuka kufanya biashara za bidhaa za kughushi,"amesema.
Mmoja wa washiriki wa mkutano huo Kelvin Remen amesema mkutano huo ni jukwaa muhimu litakalowasaidia wafabishara kulipa kodi kwa njia rafiki bila kuwa na matatizo yeyote kwa wafanyabiashara.
"Hii ni fursa kwa walipakodi kupata nafasi ya kukaa na uongozi wa juu wa TRA ilinkuwaeleza changamoto zetu ili kuweza kufikia malengo yetu na Taifa pasipo kumwumiza mfanyabiashara yeyote,"alisema.
Mwananchi
Kamishina Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata ametoa taarifa hiyo, katika mkutano TRA na walipakodi jijini Arusha wakiwemo wafanyabiashara pamoja na wakuu wa taasisi mbalimbali.
"Kuanzia sasa tutatumia sheria zetu kutoa adhabu kali kwa wale wasiotoa risiti ni vizuri tuwe na utamaduni wa kudai risiti kwani endapo utabainika itachukuliwa hatua kali,"amesema.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela akizugumza katika mkutano huo, amewataka wakazi wa Mkoa wa Arusha kushirikiana katika kufichua biashara ya bidhaa bandia ambazo zimekuwa zikichangia kudidimiza uchumi .
"Bado mkoa wetu unatumika kama daraja la bidhaa za kughushi kwa hiyo sisi kama Mkoa wa Arusha tunatakiwa kushirikiana na kuendelea kuhamasisha kuepuka kufanya biashara za bidhaa za kughushi,"amesema.
Mmoja wa washiriki wa mkutano huo Kelvin Remen amesema mkutano huo ni jukwaa muhimu litakalowasaidia wafabishara kulipa kodi kwa njia rafiki bila kuwa na matatizo yeyote kwa wafanyabiashara.
"Hii ni fursa kwa walipakodi kupata nafasi ya kukaa na uongozi wa juu wa TRA ilinkuwaeleza changamoto zetu ili kuweza kufikia malengo yetu na Taifa pasipo kumwumiza mfanyabiashara yeyote,"alisema.
Mwananchi