valid statement
JF-Expert Member
- Sep 18, 2011
- 2,851
- 870
kuharisha kwenye choo cha kuflash ugenini na ukakuta hakuna maji ya kuchamba wala kuflash.
kupanda na viatu juu ya seat cover ya choo cha kizungu
Kukojolea seat cover
Kumwagamwaga maji ovyo kwenye choo ya kizungu hadi kinakuwa chepechepe...hili huwa linaniudhi mpaka basi!Si bora kama unatak akutumia maji bila ustaarabu uende choo cha kiasia?
nice avatar...TM
kujaribujaribu nguo za mitumba zinazopitishwa na wamachinga lol
Jamani mmesahau kitu muhimu! Kucheka mbele za watu huku una kisamvu au uju wa ulezi kwenye meno. Kunuka mdomo. Kua na kucha ndefu zenye uchafu ndani mithili ya mtu aliyelima kwa mikono. Kuvaa singlet wakati mivuzi ya kwapa ina ukoko Kuvaa undersketi ndefu kuliko sket au dress. Kua na matongotongo machoni
.
Kwa wanawake: kuvaa jeans na blouse ya kitenge
u.
Sasa hivi hii ndio HABARI YA MUJINI....
Aah Twin wapi huko
Nitamani jeans? No situmiagi mimi hizo mambo
Kuvaa kaunda suti huku tshirt inachomoza kifuani na mikononi
Kuvaa goggles usiku
kujazia sahani kama ugomvi kisa umealikwa shereheni
Kutokuwa wastaarabu kwenye chakula hasa mahoteli makubwa- umepangiwa sahani kuanzia bakuli ya supu, sahani ndogo za salad, sahani kubwa za chakula kikuu na kisha sahani//vibakuli vya dessert - badala ya kula kwa mpangilio huo, unapakua kila kitu na kujaza sahani hadi inafurika ( wali, viazi,salad , kuku, nyama ya ng'ombe, samaki, matunda, keki, ...loh!)
Hii thread imenipita vipi? Nilikua sijaiona aisee...
Kwa wanawake: kuvaa jeans na blouse ya kitenge
kwa wanaume: kuvaa chupi ya chuichui alafu ionekane. (or any chupi ya maandishi na michoro michoro)
Kwanza now that I think of it, hata isipo onekana ni noma tu.
Kama hiyo kwenye picha? Inamaana hujui African prints ziko kwenye fashion. Kweli we wakizamani