Usiombee kukosa hela

Ndio maana halisi ya maisha,kuna kupanda na kushuka na kuna kipindi Mungu anakupitisha hatua kama hiyo Ili ujifunze.sizani kama kuna mpambanaji hajawahi pitia msoto kama hivo Ila yote ya yote jua yatakwisha na utasahau.
 
Wakuu mtu kama hajapitia hii hali akisoma hapa anahisi kua ni chai,ila nimepitia hii hali na bado napambana ila nilikotoka kulikua kubaya mno,home hujaacha kitu nauli yenyewe ya kukuleta kazini umeenda kukopa kwa mangi mliozoeana tena mia tano ya kukupeleka kurudi utajulia huko huko kazini,madeni ni kila mahali unaishi kama digidigi unawaza kichwa kinauma,mda wote ni hasira tu hata dogo home akitaka kucheza na wewe unamuwakia utadhani yeye ndo kasababisha hali hii,wife anakuogopa maana mudawote umekula wa mbuzi hutaki story.
Wanaume wenzangu katika kuoa tuombe mungu tupate yule mwanamke anaeweza kuvumilia hali yoyote ile ,ilifika mahali nikahisi huyu mwanamke anaweza kunikimbia manana ukikosa hela hata kujiamini kunapotea. Nashukuru amekua bega kwa bega na mimi na mdogo mdogo najipanga sitaki nirudi nilikotoka.Japo wanaume sijui hua tunafeli wapi unaweza pitia magumu yote hayo lakini siku ukizipata unasahau unarudi kulekule.Mungu anaisaidie na anisimamie.Amina
 
Ndo hapo sasa inabidi kujicommit walau kusave kiasi....yaan walau kwa mwez usave 50k
 
Touching! Sasa kuna wengine unawavumiliaaa...wakipokea mshahara badala akupgir tafu na ww majukumu unaona anaongizana daily na jirani kuzigonga bia na makitimoto...bas akusaidie kununua walau sukar hakuna...huyoooo..tar 1 ikifika hana mia ..anarudi kuanza kuomba omba...wanaume mna matatizo sana aise...
 
Unachosema ni kweli,ila sasa mimi basi huo upuuzi taratibu nauacha,life limenipa somo kibabe sana,na nimenyooka dadeki.
 
Nipo hapa
 
Aiseeee nilidhani nateseka peke yangu katika maisha kumbe tuko wengi, mimi kuna kipindi nilipitia wakati mgumu sana tena sana yaani kila nachokifanya kinagoma, sio shambani sio mtaani hadi nikahisi mwezi wa 3 mwaka huu sitatoboa, maana kila unaemuambia shida zako nae anakupa matatizo yake hali ni mbaya, unakataa tamaa nakumbuka last time nikawaza niuze hii simu, godoro na vitu vya gheto nirudi home ila nikawaza home nitaenda kufanya nini na nilishakacha tangu 2016, kuna manzi yangu alikuwa anafanya kazi Tanga alikuwa ananipiga company maana anajua hali yangu yeye kasoma afya so alivyoua chuo tu akapata pa kushika, mimi nikawa kitaaa naganga njaa mwaka jana nikachoma hela kama milioni 2 hivi katika biashara bado kidogo nijiue
huyu manzi akashtuka nimi sijui nikashangaa kanitumia 50k kaniambia njoo Ta upumzike kwanza ujipange upya, to cut the story mwaka huu mwezi wa tatu ndio nilichoka nadaiwa kodi, mara shamba nililomaga limenishinda n.k nakumbuka siku hiyo nimebaki na mb 200 nikaandika uzi nikautupia kule kwenye Jukwaa la tenda na ajira baada ya hapo bundle likakata wadau wakaanza kunicheki nikapata msaada japo bado napambana maana sina kazi ila haya maisha ukiwa lele mama unaweza ukakimbia dunia hii au unaweza ufanye mambo ya ajabu ili usurvive hali inatisha, ila nimegiundua kwamba Mungu anatupa mitihani kutupima imani yetu juu yake na anatupa mitihani ambayo tunaweza kuikabili.. pia tuishi na watu vizuri haswa watu baki maana wao ndio wanaweza kukusaidia kuliko ndugu zako talking from the experience..


Marufuku kukataa tamaa


uzi ulinisave huu hapa

 
Kwa kweli ni kazi sana haya maisha acha tu ndugu yangu kuna siku Unaamka huna hata miaa alafu upo na familia..!! Dada wa kazi anakuangalia na mama anakuangalia..

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
Kwa kweli ni kazi sana haya maisha acha tu ndugu yangu kuna siku Unaamka huna hata miaa alafu upo na familia..!! Dada wa kazi anakuangalia na mama anakuangalia..

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
Unaweza kupagawa,kuna siku wife usiku kachemka balaa kama pasi ya moto nikawa naombea asubuhi ifike akiwa mzima,lakini mfukoni sina hata ile inayoitwa sh. kumi,palipokucha nikakaa kwenye kiti natafakari nimpigie nani simu walau nipate hata elf 20 nimpeleke hospitali maana kadi yake ya bima ya afya aliisahau bush alipokwenda kusalimia.Nasema ni Mungu tu mawazo yakanijia nikasema hebu niangalie kwenye akaunt yangu ya benki labda kunaweza kua na maajabu yoyote,kucheck daah nakuta laki na elf tano,sikujiuliza imetoka wapi wala nini nikaivuta kwa simu nikaenda kuitoa chap,nikamwambia wife jiandae tunaenda hospitali,akaniuliza hela umetoa wapi nikamwelezea jinsi ilivyokua akashangaa,nikamwabia asiyeamini kua mungu yupo huyo muacheni tu ila hili ni mungu kanitendea,mpaka leo sijajua ile hela iliingiaje kwenyee akaunti yangu na wala haijawah kukatwa.Huyu Mungu huyu.
 
Yeye hufanya njia pasipo na njia huyu Mungu ni wa kushukuriwa wakati wote.
 
Pole sana,ipo siku yatakwisha

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 

Hapo sukari unaikoregea kwenye maji, unakunywa kama chai... Huu wakati huwa ni mgumu sana hasa kwa wanaokata tamaa mapema huchukua hatua ya kujiua. Maisha yana siri nzito!
 
malipo ni hapahapa dunuani watu walimsifia sana mwendazake , sasa ndio tunaona reality, kila mtu analia hata wabunge na posho zote bado wanalia, walimu ndio kabisaaa, wafanyakazi choka mbaya mikopo kibaaao kuna jamaa alinionyeshaga nakala yake ya mshahara (salary slip) yaani mtu ana mke na watoto anapokea 72,000/= na bado anaishi hajafa, hapo mshahara wake ni zaidi ya laki7 ni mtumishi wa umma , mikopo sijui nini sijui nini balaa tupu, na mtu kama huyo unakuta anaenda kabisa kupiga kura
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…