Usiombe hili likakukuta

Usiombe hili likakukuta

Daty

Senior Member
Joined
Jul 1, 2011
Posts
126
Reaction score
13
Wenyewe mmetoka mbali toka mume hana kitu mnapigana na maisha ukiwa na matumaini ni mume wako miaka minne ya shida mnafanikiwa kupata kipato halafu mume anakumwaga tena kwa kashfa, kwa wanawake zake na talaka juu.

Wakati alikuwa anakuulilia mke wangu nakuomba usijenikimbia kwa umasikini wangu nivumilie ipo siku nitapata.

Na alivyopata akakumwaga mazima
 
We umemwagwa? Kama vipi ungemlia timing unamwaga wewe kabla hajakumwaga.
 
ya kawaida hayo ndani ya jamii,Na hiyo ndo tabia halisi ya huyo jamaa,Wahenga wanasema "pata pesa tujue tabia yako filisika ujue tabia ya mkewe
 
hiyo ikitokea msusie hadi nguo zako ondoka kama ulivyo
laana yake aiseeeee haina tiba
 
Mwanaume akiwa na dhiki anajua kupenda na kubembeleza!!! Akizipata ni habari nyingine,atataka aonje za kila rangi!!
Pole kama yamekukuta,Bora kakutimua kakuepushia STD's na maradhi ya moyo!
 
Hujatueleza kisa cha kukumwaga. Hapa unaeleza mapungufu ya upande mmoja tu.Kutafuta wote siyo lazima kwamba nawe unapaswa jiona uko juu yake. Lazima kuna sababu.
 
Namna hii ndo mana nawashauri wadogo zangu akina miss neddy kuwa bora mwanaume mwenye hela tu hata akikumwaga hujutii sana mana umefaidi.....unasota weee then matunda anakula peke yake
 
Last edited by a moderator:
Hapo ukute nia mimba alishakutundika. Ila usijali atafirisika atakua kama awali halafu hao wake zake watamwacha kama alivokuacha wewe. Amini.
 
Namna hii ndo mana nawashauri wadogo zangu akina miss neddy kuwa bora mwanaume mwenye hela tu hata akikumwaga hujutii sana mana umefaidi.....unasota weee then matunda anakula peke yake

hahahaha unapigwa free p mambo yakiwa mazuri anafaidi mwingine lol
 
Last edited by a moderator:
Namna hii ndo mana nawashauri wadogo zangu akina miss neddy kuwa bora mwanaume mwenye hela tu hata akikumwaga hujutii sana mana umefaidi.....unasota weee then matunda anakula peke yake
Si Bora ale peke yake!
Anasaka vibint vya Kula nae!!
Mijanaume ya hivi ni kuiombea tu ife ikiwa maskini,Mungu awape hela ya Kula tu wasife njaa.
 
Last edited by a moderator:
Si Bora ale peke yake!
Anasaka vibint vya Kula nae!!
Mijanaume ya hivi ni kuiombea tu ife ikiwa maskini,Mungu awape hela ya Kula tu wasife njaa.

Kweli kabisa aisee ila wachache wanaofanikiwa na ujinga huu
 
Kumuacha mtu ambae mmetafuta nae ni laana ambayo haifutiki hata kwa maji matakatifu...
 
hiyo ikitokea msusie hadi nguo zako ondoka kama ulivyo
laana yake aiseeeee haina tiba

laana?! Laana bongo? Tena kwa kizazi hiki cha nyoka? Ukitendwa na ukategemea laana basi ujue imekula kwako. Hapa ni jino kwa jino. Japo ulinifukuzia njiwa wangu Vaislay
 
Last edited by a moderator:
laana?! Laana bongo? Tena kwa kizazi hiki cha nyoka? Ukitendwa na ukategemea laana basi ujue imekula kwako. Hapa ni jino kwa jino. Japo ulinifukuzia njiwa wangu Vaislay

Jifariji inawezekana ndo walewale
 
Last edited by a moderator:
Ndio ujue sasa kwa nini wanawake wa siku hizi wanataka ALIYENAZO
 
ahaaaaaa jaman kwel usithubutu kukutwa na hali hiyo
 
Back
Top Bottom