Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Usiku wa leo wanaitaka roho yako! Leo usiku roho yako itachukuliwa! Leo usiku maisha yako yatafikia mwisho, utaondoka duniani...
Usishtuke wala usiogope; sio wewe! Maneno hayo aliambiwa mtu fulani tajiri. Shamba lake lilizaa sana. Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’ Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa maghala yangu ya nafaka na kujenga mengine makubwa zaidi nihifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu. Kisha nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, kunywa, ufurahi.”'
Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Habari hiyo inapatikana katika Luka 12. Ni habari inayotuhusu sisi sote. Inawezekana hata wewe umetafuta pesa, umeweka akiba ya kutosha, sasa unapanga mipango ya kwenda mahali kula, kunywa na kustarehe, bila kujua kwamba usiku wa leo maadui zako wanataka kukuangamiza. Sasa, hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Mungu atusaidie kukumbuka hilo. Kwamba wakati tusiodhani, maisha yetu yanaweza kukatika. Hivyo tujitajirishe pia kwa Mungu, ili tukiondoka, tuweze kupumzika na kustarehe mbinguni.
Usishtuke wala usiogope; sio wewe! Maneno hayo aliambiwa mtu fulani tajiri. Shamba lake lilizaa sana. Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’ Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa maghala yangu ya nafaka na kujenga mengine makubwa zaidi nihifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu. Kisha nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, kunywa, ufurahi.”'
Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Habari hiyo inapatikana katika Luka 12. Ni habari inayotuhusu sisi sote. Inawezekana hata wewe umetafuta pesa, umeweka akiba ya kutosha, sasa unapanga mipango ya kwenda mahali kula, kunywa na kustarehe, bila kujua kwamba usiku wa leo maadui zako wanataka kukuangamiza. Sasa, hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Mungu atusaidie kukumbuka hilo. Kwamba wakati tusiodhani, maisha yetu yanaweza kukatika. Hivyo tujitajirishe pia kwa Mungu, ili tukiondoka, tuweze kupumzika na kustarehe mbinguni.