Usijaribu kuuza saa, simu mbovu Kariakoo

Usijaribu kuuza saa, simu mbovu Kariakoo

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,712
Reaction score
830,745
Ukipita mitaa ya kariakoo hasa Congo, na mitaa yote karibu na shule ya Uhuru mpaka msimbazi polisi ni kawaida kukuta matangazo ya kununua simu na saa mbovu

Tahadhari: usijaribu kuuza kitu chako kibovu kwakuwa hakitanunuliwa! Sana sana kitaongezewa ubovu kwa kuchomolewa vifaa ambavyo bado ni vizima

Kinachofanyika ni hiki: wengi wanaoweka haya matangazo ni mafundi hivyo unapeleka kitu chako kikiuza hukuambia rudi baada ya muda fulani, kinachofanyika huku nyuma ukiondoka hufungua na kutoa vifaa vyote vizima na kukuwekea vibovu kabisa

Muda uliopewa ukirudi unaambia kitu chako hakiuziki hivyo kichukue tu, kwakuwa ni kibovu hutaweza kumbana kwa lolote lile lakini tayari utakuwa umeshamfaidisha kwa kuchukua vifaa vilivyo vizima na kuwekewa vibovu kabisa

Ushauri: muulizie tena kwa fedha tasilimu yeyote anayehitaji tena bila kupeana muda wa kurudi kuchukua pesa yako! Wajanja ni wengi siku hizi na wezi ndio wametamalaki kila kona
 
Loh! Kweli mjini shule' kila kukicha wanasayansi wanavumbua mbinu mpya ya kupata Escrow! Anyway ndiyo matunda ya uhuru...
 
wajinga ndo waliwao utaachaje kitu urudi badae malizeni biashara kwanza ndo uondoke
 
kabisa unaacha kifaa chako kwa fundi bila dhamana yoyote we mzima kweli?
 
kabisa unaacha kifaa chako kwa fundi bila dhamana yoyote we mzima kweli?

Wengi wamelizwa wala usiwashangae mjini hakuna mjanja bali kuna kupata na kupatwa kupiga na kupigwa
 
Watu wamechoka wanatafuta mbinu za kuishi wapate chochote, anyway, ujumbe umefika
 
Hoja ya facebook hyo
Kwan m2 mwebyewe c ndo anafanya makubaliano nao kwan huwa wanamuibia?
Mjinga ndio aliwaye
 
Wameweka Tangazo Kuwa Wanataka Simu Mbovu,na Wewe Umepeleka Simu Mbovu,sasa Wanasemaje Haiuziki? Halafu Unaachaje Biashara Kwa Mtu Bila Makubaliano?, Wezi Wa Aina Hii Ukikutananao We Piga Kelele Wapigwe Tu Kama Wezi Wengine.
 
Mzee wa photo says All, leo cjaona picha umetuletea mada iliyosheeni tu. Ah hahahahaaaaaaa.


Ukipita mitaa ya kariakoo hasa Congo, na mitaa yote karibu na shule ya Uhuru mpaka msimbazi polisi ni kawaida kukuta matangazo ya kununua simu na saa mbovu

Tahadhari: usijaribu kuuza kitu chako kibovu kwakuwa hakitanunuliwa! Sana sana kitaongezewa ubovu kwa kuchomolewa vifaa ambavyo bado ni vizima

Kinachofanyika ni hiki: wengi wanaoweka haya matangazo ni mafundi hivyo unapeleka kitu chako kikiuza hukuambia rudi baada ya muda fulani, kinachofanyika huku nyuma ukiondoka hufungua na kutoa vifaa vyote vizima na kukuwekea vibovu kabisa

Muda uliopewa ukirudi unaambia kitu chako hakiuziki hivyo kichukue tu, kwakuwa ni kibovu hutaweza kumbana kwa lolote lile lakini tayari utakuwa umeshamfaidisha kwa kuchukua vifaa vilivyo vizima na kuwekewa vibovu kabisa

Ushauri: muulizie tena kwa fedha tasilimu yeyote anayehitaji tena bila kupeana muda wa kurudi kuchukua pesa yako! Wajanja ni wengi siku hizi na wezi ndio wametamalaki kila kona
 
Ww nawe ni wakuja toka Sangamwalugesha, utaachaje kifaa chako K/koo eti njoo uchukue baadae, unless km umepeleka kwa minajili ya kutengenezwa, ingawa napo inategemea na mazingira
 
Back
Top Bottom