USIA wa Baba wa Taifa!

USIA wa Baba wa Taifa!

Nape Nnauye

MP Mtama
Joined
Dec 26, 2012
Posts
99
Reaction score
408
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.

Nyie ndo warioba anasema msimtumie Nyerere kama hirizi?
 
Wewe Nape huko Zanzibar huna tofauti na Mkenya

Huwezi kumilikishwa ardhi ya aina yeyote

Huwezi kuajiriwa kwenye serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Huwezi kuomba nafasi yeyote ya kugombea huko kama ambavyo unaweza ukajaribu kwenye jimbo lolote huku Bara
Sasa kwa nini tuendelee kuwa watumwa wao?
Kwa nini hamridhiki na Tanganyika yetu?mbona Rwanda na Burundi ni nchi ndogo kama baadhi ya mikoa hapa kwetu Bara lakini wamejikubali?
Bila kuungana na Zanzibar Tanganyika haiwezi kusimama?
Hebu fungukeni zaidi mtueleze agenda za siri za Muungano huu mnaoung'ang'ania manake sidhani kama zimeshawahi kuwekwa wazi asilani
Tanganyika kwanza,Tanzania baadaye
 
Hakika mkuu Mwalimu alikuwa anabadilika kulingana na wakati sio kumtumia Nyerere kama hirizi

Je unakumbuka swali na warioba kwamba Nyerere akija leo ni nan atamuona msaliti?

Nyerere akifufuka leo ameone warioba anavyotoa mishipa kuiua Tanzania atamlaani na warioba akimuona mwalim atakufa hapo hapo
 
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.

kwa katiba ya zanzibar ya 2010 tayari tumeizika Tanzania.
Rethink critically.
 
Nyerere akifufuka leo ameone warioba anavyotoa mishipa kuiua Tanzania atamlaani na warioba akimuona mwalim atakufa hapo hapo

Nyerer atarudi kaburini haraka sana akiona wabunge wa zanzibar kushiriki bunge la muungano per se lakini wabunge wa muungano kutoshiriki bunge la zanzibar.
 
Kijana Nape Nnauye
Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu,

Kwa bahati nzuri katiba inayoandikwa ni ya wananchi na si ya wanachama wa ccm. Wananchi watachagua katiba inayowafaa sasa na si ile iliyokuwa inafaa wakati wa Mwl. Nyerere. Kusema kuwa ccm 'katu haitakubali' ni kuonyesha jeuri mliyo nayo dhidi ya Watanzania na kujifanya kwamba mnayo hati miliki ya Tanzania. Mbona vyama vingine havise,i kuwa 'havitakubali katu'bali vipo tayari kusikiliza maoni ya wananchi??? Jeuri yenu hii ndio itakayowamaliza.
 
Hivi nape wewe ni mwanasiasa au mtumwa wa siasa, kama huwezi kuna kazi hii hapa chini
 

Attachments

  • 1399197047461.jpg
    1399197047461.jpg
    10.8 KB · Views: 296
Nyerere akifufuka leo ameone warioba anavyotoa mishipa kuiua Tanzania atamlaani na warioba akimuona mwalim atakufa hapo hapo

Kabla ya kujiuliza ebu jihoji mwenyewe aliacha serikali ngap na nchi ngap na leo kuna nin?
vip kuhusu rushwa ?
 
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.
Tanzania haihitaji CCM ili idumu bali CCM inaihitaji Tanzania kwa udi na uvumba ili idumu.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.
We mjinga wa kutupwa! liko wapi Azimio la Arusha? iko wapi Elimu ya Kujitegemea "Education for Self Reliance" ambayo ilikuwa dira ya Elimu ya Tanzania! Nakutaka uache kumtaja Nyerere kwa maslahi ya mafisadi wanao kutumia kama mpira wa kiume.
 
We mjinga wa kutupwa! liko wapi Azimio la Arusha? iko wapi Elimu ya Kujitegemea "Education for Self Reliance" ambayo ilikuwa dira ya Elimu ya Tanzania! Nakutaka uache kumtaja Nyerere kwa maslahi ya mafisadi wanao kutumia kama mpira wa kiume.
Wao wanaona moja tu la muungano utadhani muda wote wa utawala wake alisisitiza jambo moja, hata hivyo Nyerere ninayemjua hakuacha nchi mbili kama ilivyo leo.
 
Yaani Nyerere anatumiwa pale panapohusu maslahi yao!!Mambo mengine kama RUSHWA,UFISADI,NEPOTISM!Wako speechless....
 
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.

Mkuu, Mwalimu alikuwa sahihi kabisa kauli yake ikisomwa kwa pamoja na sehemu nyekundu. CCM yenye WANACHAMA WENYE AKILI, UKWELI, na UJASIRI. Sujui kwa CCM ya leo "akili" hasa maana yake ni nini? Ni kuvunjwa kwa Katiba ya JMT bila chama kusimama imara kukemea? Na ukweli wa CCM ya leo ndio upi?

Au ujasiri wa ndani ya CCM ya leo maana yake nini? Ni yale matusi, kejeli, kashfa, na ubaguzi tulioshuhudia BMK na kwenye mikutano mbalimbali ya Chama? Au ni ujasiri wa kupora rasilimali za nchi? Au ni kuvusha madawa ya kulevya na kuigeuza nchi kitovu kikuu cha biashara hiyo haramu?

Nyere alikuwa sahihi lakini sio kwa aina ya CCM ya leo inayomtumia kama hirizi!
 
ccm ni wapuuzi kabisa
nape mwanzoni ulionekana wa maana sana ulipoaamua kutumia akili zako sawasawa na uzalendo dhidi ya kupinga rushwa chamani kwako, hata ukafikia kukorofishana na mzee makamba na uvccm, lakini ulipokubali kuwasaliti vijana wenzako kwa vipande vya lupia, basi ukawasaliti watanzania wanaoitafuta haki na kweli, hakika umepotoka na huna maana tena mbele ya taifa hili, wewe na masisiemu menzako mmeamua makausidi kabisa kuendelea kufanya watanzania kuzidi kuwa masiki, nafukara kabisa, ndio maana hamtaki watu wapate elimu nzuri, wala fursa. Mlaaaniwe milele

leo kwenye sula la katiba ndio mnamkoti nyerere kila speech....
Nikuulize, nipe speech ya nyerere juu ya watu dizaini ya lowasa.. Malecela etc,.. Aliwaambia nini?? Na leo wako sisiemu au mmewafukuza.... Leo hao watu si ndio tegemeo lenu.. Mnawakumbatia kama malaika.. Hakika sisiemu imelaaaniwa

1. Nyerere alitetea rushwa, kama leo mnavyofanya?? Epa, richmond, kagoda etc mmechukua hatua gani??
2. Nyerere alianziasha azimio la arusha kwanini mmeliua?? Nani mmemuwajibisha kwa hilo
3. Kwanini nyerere hakuuza migodi wakati ule, mbona nyinyi leo mmeiuza imebaki mashimo tu, nchi imefaidika nini??
4. Nyerere alipambana na adui maradhi, ujinga, na umaskini, nyinyi mnapambana na nini>? Nchi inamiaka 50 watoto wanakaa nchini, mpaka leo hospitali hazina madawa, wala vitanda, watu wanakufa kwa njaa
5. Nyerere alitetea elimu ya kujitegemea, nyinyi leo ndio mmeona kupitia elimu ndio muharibu kabisa shule za serikali, na huku nyinyi maintarahamwe mkiharibu ubora wa elimu ,mkianzisha shule zenu binafsi, ili mtoto wa maskini abaki maskini hivyohivyo, halafu wa kwenu wakasome shule nzuri na wazidi kutawala..

Nailaaani sisiemu kwa nguvu zangu zote.
 
Nape Nnauye,sasa mbona CCM hambadiliki kwenda Serikali moja kama mnamzingatia Mwalimu Nyerere? Acheni unafiki nyinyi CCM.Hii nchi ni yetu wote na sisi tunataka Serikali tatu sasa. Mtatutisha na hatutatishika;mtatusema hatutasikia.Tunataka Serikali tatu tu....hakuna zaidi
 
Last edited by a moderator:
My foot kiongozi mzima unaandika thread ya kuitetea serikali mbili kwa kutumia mistari minne?
You are so shallow my dear
 
Nasikia muda mfupi ujao leo utakuwa na mdahalo ITV pale Serena Hotel. Au ndio umeanza kupaniki na kuanza kutafuta majibu? Ha ha ha! Yetu macho nasubiria kuona ukavyojenga "hoja".
 
Back
Top Bottom