Ushuhuda: Makaburu wanavyotuibia dhahabu kwenye migodi sisi na Wakanada

May 20, 2013
71
151
Nilikuwa nafanyakazi tarime mgodi wa North Mara miaka ya 2009/10 kwenye kitengo cha security. Kuna kijana anaitwa John tulikuwa naye kwenye kitengo cha security. Mimi na John tulikuwa tunasimamia ugawaji wa mufuta kwenye machine zilizopo kwenye machimbo (Pit) kwa kutumia fuel boozer. Ratiba yetu kwa siku ilikuwa inaanza saa 12 asubuhi tunajaza boozer mafuta na kwenda nalo pit.

Siku moja nikaamka asubuhi pale camp nikampitia john nikakuta ameshaondoka, basi nikajua ametangulia offisini, nikaenda ofisini sikumkuta nikawa namsubiri, nilivyoona anachelewa nikaanza kumtafuta kwenye simu lakini simu yake ikawa imezima. Muda ukawa unaenda nikashangaa hata wazungu mabosi wa security hawapo, basi nikaamua kwenda kusimamia ujazaji wa mafuta mimi mwenyewe. Baada ya muda John akawa amekuja nikamuuliza ulikuwa wapi. Akanijibu siku ilivyoanza;

Alipigiwa simu kama saa 11 alfajiri na security manager (SM) aende ofisini, akaenda alipofika pale akamkuta manager na mkaburu mwingine, wakamwambia azime simu yake halafu awape, alipowapa wakamwambia aendesha gari wakaende nae camp anakokaa security superintendent (SS). Yeye akaambiwa asubiri kwenye gari, wakaingia ndani wakakaa kama dk 10, halafu wakatoka wamebeba maboksi kama ya ukubwa wa sabuni za mche, kilichomshangaza yale maboksi ni madogo lakini wameyabeba wawili, mmoja akaja kufungua mlango wa nyuma wa gari na kubakia pale, wale SS na SM wakaingia ndani kuja na boksi jingine mpaka yakafika maboksi matatu. Wakati huo walikuwa wanawasiliana na makaburu wenzao kwa simu za mkononi kwa ki-africana. Walikuwa hawatumii radio call.

Baada ya kumaliza kuyapakia SS akapanda mbele na SM na Yule kaburu mwingine wakapanda nyuma kwenye yale maboksi, akaambiwa aendeshe gari kuelekea plant. Akaendesha gari kuelekea plant akashangaa mageti yote kutokea camp kuelekea plant yapo wazi na kuna security officer mkaburu kila geti hadi geti la “high security” , alipofika plant wakayashusha yale maboksi wenyewe na kuyaingiza kwenye helicopter ambayo ilikuwa imekuja kuchukua mzigo wa dhahabu ambao unakuwa umekaguliwa na kuwekwa seal na TRA na TMAA tokea jana yake.

Ile helicopter ikaondoka. Baada ya kuondoka ndio wakamrudishia simu yake na kumruhusu aondoke. Aliponisimulia hivyo nikajua wameshatuibia dhahabu, kwa sababu kiutaratibu, dhahabu huwa haitoki gold room, maafisa wa TRA na TMAA huja siku moja kabla ya kusafirisha dhahabu na kufunga seal zao, siku inayofuata dhahabu iliyofungwa hupakizwa kwenye helicopter ambayo hutua hapohapo plant.

Nikaamua kumpigia Yule afisa wa TRA wa Musoma anayekuja kufunga seal pale mgodini nikamweleza huo mkasa mzima akampigia afisa mwingine wa TRA aliyepo mwanza aende akaiwahi ile helicopter kabla haijatua ili aone kama kuna mzigo wa dhahabu ambao haujafungwa seal. Bahati mbaya Yule afisa wa mwanza akafika uwanja wa ndege wa mwanza akakuta ile helicopter imeshatua na mzigo umeshafaulishwa. Ikwawa imekula kwetu.

USHAURI wangu kwenye kukagua haya madini maafisa wetu wawe wanakagua na kufunga seal siku hiyo hiyo ambayo dhahabu inasafirishwa ili wahakikishe dhahabu inayosafirishwa ndio ile iliyofungwa seal pekeyake. Otherwise makaburu wanatupiga sana, kwa sababu wenyewe kwa wenyewe wanazungukana na kuiba dhahabu, case za makaburu kuiba dhahabu ni nyingi tu humu migodini, wakanada wenyewe wanajuwa kuwa makaburu wanawapiga
 
naamini shida zote hizi zimeletwa na ccm. wenyewe wanakabidhiana ulaji, wewe kula hapa mi nakula pale ,wewe kula huko huko
 
Inamaana hizo dhahabu zilizalishwa vipi bila mkaguzi wa TMAA kuwepo.Ila kwa kipindi hicho nadhani TMAA haikuwepo; kulikuwa na Alex Stewart wazungu.Nipo tayari kusahihishwa
 
Kuna jamaa flan alinisimulia geita gold mine Kwa siku wanapata dhahabu kilo 25 lakini Iyo 25 kg ni mchanga tipa elfu labda.sasa yale makontena ya Sizonje bandarini usikute mchanga ukisafishwa unapata kilo moja na robo
 
Kuna jamaa flan alinisimulia geita gold mine Kwa siku wanapata dhahabu kilo 25 lakini Iyo 25 kg ni mchanga tipa elfu labda.sasa yale makontena ya Sizonje bandarini usikute mchanga ukisafishwa unapata kilo moja na robo
Acha uongo
 
[QUOTunapanhagen DN, post: 20532971, member: 251293"]Kuna jamaa flan alinisimulia geita gold mine Kwa siku wanapata dhahabu kilo 25 lakini Iyo 25 kg ni mchanga tipa elfu labda.sasa yale makontena ya Sizonje bandarini usikute mchanga ukisafishwa unapata kilo moja na robo[/QUOTE]
Hesabu rahisi ni hivi.Kabla ya uchimbaji unafanyika uchunguzi wa grade kwa tone moja ya mawe.Mfano kila tani moja ina gram mbili za dhahabu. Kama umesaga tani mfano tani 10, ni kwamba unachukua tani 10 unazidisha na grade ya 2g kwa tani.
=2g/t*10t=20g. Sasa huwezi kupata zote; itategemea umezikamata kwa asilimia ngapi ndio unazidisha tens
Mfano kwa asilimia tisini
=20g*90/100=18g
 
Humu tulishamjuzeni hata lile dege lililokuwa linatua geita 2002 kila alhamisi kwamba laondoka na mizigo lakini hamkutuelewa.
 
Hakuna wizi,hujuma,ufisadi,rushwa unaofanyika nchini bila ccm na serikali yake kujua. Mikataba yote nchi hii na wawekezaji imefanywa na ccm na serikali yake na uzuri bado serikali ya ccm ndio inatawala toka uhuru.
So hizi kelele toka chumbani ambako serikali ya ccm na wawekezaji wamejifungia zinashangaza,au labda ni mbinu tu ya kuzuga wasiojitambua.
 
Ndo maana nikimkumbuka mwazuoni nguli kupata kutokea aliyekuwa akiitwa Dr. Walter Rodney kutoka nchini Guyana alipokuwa akielezea kwa machungu katika kitabu maarufu cha "How Europe underdeveloped African" namna ambayo wazungu walivyofanikiwa kutajirika kwa kuchuma maliasili zetu kama dhahabu Kiasi cha kutengeneza kitu linaitwa "Gold Bullion" kwa mataifa zao 25kg of pure gold bars zinakupa utajiri wa kupindukia
 
Wewe ulipewa sh ngapi
Nilikuwa nafanyakazi tarime mgodi wa North Mara miaka ya 2009/10 kwenye kitengo cha security. Kuna kijana anaitwa John tulikuwa naye kwenye kitengo cha security. Mimi na John tulikuwa tunasimamia ugawaji wa mufuta kwenye machine zilizopo kwenye machimbo (Pit) kwa kutumia fuel boozer. Ratiba yetu kwa siku ilikuwa inaanza saa 12 asubuhi tunajaza boozer mafuta na kwenda nalo pit.

Siku moja nikaamka asubuhi pale camp nikampitia john nikakuta ameshaondoka, basi nikajua ametangulia offisini, nikaenda ofisini sikumkuta nikawa namsubiri, nilivyoona anachelewa nikaanza kumtafuta kwenye simu lakini simu yake ikawa imezima. Muda ukawa unaenda nikashangaa hata wazungu mabosi wa security hawapo, basi nikaamua kwenda kusimamia ujazaji wa mafuta mimi mwenyewe. Baada ya muda John akawa amekuja nikamuuliza ulikuwa wapi. Akanijibu siku ilivyoanza;

Alipigiwa simu kama saa 11 alfajiri na security manager (SM) aende ofisini, akaenda alipofika pale akamkuta manager na mkaburu mwingine, wakamwambia azime simu yake halafu awape, alipowapa wakamwambia aendesha gari wakaende nae camp anakokaa security superintendent (SS). Yeye akaambiwa asubiri kwenye gari, wakaingia ndani wakakaa kama dk 10, halafu wakatoka wamebeba maboksi kama ya ukubwa wa sabuni za mche, kilichomshangaza yale maboksi ni madogo lakini wameyabeba wawili, mmoja akaja kufungua mlango wa nyuma wa gari na kubakia pale, wale SS na SM wakaingia ndani kuja na boksi jingine mpaka yakafika maboksi matatu. Wakati huo walikuwa wanawasiliana na makaburu wenzao kwa simu za mkononi kwa ki-africana. Walikuwa hawatumii radio call.

Baada ya kumaliza kuyapakia SS akapanda mbele na SM na Yule kaburu mwingine wakapanda nyuma kwenye yale maboksi, akaambiwa aendeshe gari kuelekea plant. Akaendesha gari kuelekea plant akashangaa mageti yote kutokea camp kuelekea plant yapo wazi na kuna security officer mkaburu kila geti hadi geti la “high security” , alipofika plant wakayashusha yale maboksi wenyewe na kuyaingiza kwenye helicopter ambayo ilikuwa imekuja kuchukua mzigo wa dhahabu ambao unakuwa umekaguliwa na kuwekwa seal na TRA na TMAA tokea jana yake.

Ile helicopter ikaondoka. Baada ya kuondoka ndio wakamrudishia simu yake na kumruhusu aondoke. Aliponisimulia hivyo nikajua wameshatuibia dhahabu, kwa sababu kiutaratibu, dhahabu huwa haitoki gold room, maafisa wa TRA na TMAA huja siku moja kabla ya kusafirisha dhahabu na kufunga seal zao, siku inayofuata dhahabu iliyofungwa hupakizwa kwenye helicopter ambayo hutua hapohapo plant.

Nikaamua kumpigia Yule afisa wa TRA wa Musoma anayekuja kufunga seal pale mgodini nikamweleza huo mkasa mzima akampigia afisa mwingine wa TRA aliyepo mwanza aende akaiwahi ile helicopter kabla haijatua ili aone kama kuna mzigo wa dhahabu ambao haujafungwa seal. Bahati mbaya Yule afisa wa mwanza akafika uwanja wa ndege wa mwanza akakuta ile helicopter imeshatua na mzigo umeshafaulishwa. Ikwawa imekula kwetu.

USHAURI wangu kwenye kukagua haya madini maafisa wetu wawe wanakagua na kufunga seal siku hiyo hiyo ambayo dhahabu inasafirishwa ili wahakikishe dhahabu inayosafirishwa ndio ile iliyofungwa seal pekeyake. Otherwise makaburu wanatupiga sana, kwa sababu wenyewe kwa wenyewe wanazungukana na kuiba dhahabu, case za makaburu kuiba dhahabu ni nyingi tu humu migodini, wakanada wenyewe wanajuwa kuwa makaburu wanawapiga
 
Tulisha ibiwa sana, sasa hivi wanamalizia kwenye visigino. Kwa sababu si zaidi ya miaka 10 mbele migodi mingi itakuwa haina dhahabu tena.

Tatizo ni , serikali dhaifu, viongozi na watendaji tamaa mbele!!

Yaani, sisi bado sanaaaaa!!
 
To late ma men, tungewalipua wote ,mnajua aliyeongoza serikali kipindi hicho ni yule ambaye akijua unakosa atakueleza angalia usikamatwe ,siyo huyu wa sasa atakulipua na huyu ni mpango wa mungu, 'Yesu alipelekwa kuwakomboa wayahudi lakin wayahudi hawakujua hilo wakasema asurubishwe barabara'
 
Waloofanya kazi migodini wanajua mengi ambayo wakiyasena hapa watu mnaweza kudata na ikaleta natatizo
 
Back
Top Bottom