USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

Kanda ya ziwa msitusahau, mimi nipo mwanza kwa mdau mwenye idea ya hawa chotara anipe abc pls
 
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful
Mkuu naomba utujuze huo mchanganyiko wa msosi mpka kuku wa kienyeji wanataga non stop.
 
Mkuu hao kuku chotara hapo tazara ulichukua kwa bei gani pamoja na ukubwa wao nataka kupata jogoo mkubwa na tetea wawili angalau wale nitakua ndo uzao wa kwanza msaada tafadhali maana Kuna watu hawajibu ukiwauliza
wanauza vifaranga hawauzi wakubwa bei ni 500 kwa kifaranga wakati niliponunua mwezi wa 3 mwaka huu nazani hawajapanda kama wamepanda c ghali sana
 
Nimesoma makala yako kwa undani but mengine si kweli.n imegundua pia unavutia biashara yako pia!
Kwa mfano mm nilianza na kuku 3,majike 2 na dume 1 wa kienyeji.ilikua mwisho wa mwezi wa 12 mwaka jana 2015. But mpaka mwez wa sita mwaka huu nilikuwa nimepata kuku zaid ya 60. Kuku wangu wanataga wastan wa mayai 15-18. Na kila baada ya miezi miwili ni lazima watoto.ninachokifanya vifaranga nilikua nabitunza mwenyewe toka siku ya kwanza kutotolewa .
Kuku wangu wanataga kila baada ya wiki 2 baada ya kutotoa.
Tena nimegundua njia nzuri ya kuku wa kienyeji kutotoa vifaranga kuanzia 20-24. Kwa wakati mmoja na kwa kuku mmoja.
Kuku wa kienyeji wanalipa kama itaamua kukomaa na kufuata maelekezo.
Ufugaji wa kuku wa kienyeji una changamoto zake japo zinaweza tatulika pia.
 
wanauza vifaranga hawauzi wakubwa bei ni 500 kwa kifaranga wakati niliponunua mwezi wa 3 mwaka huu nazani hawajapanda kama wamepanda c ghali sana
Mmnh sawa mkuu shukrani sana kingine nilikua nauliza kwa hapa ninao kuku wa nne wanaatamia na mwingine anataga je hao vifaranga vipya naweza kuvichanganya katika kuku wapya watakaototolewa Bila madhara yoyote kwa hao vifaranga chotara
 
Mmnh sawa mkuu shukrani sana kingine nilikua nauliza kwa hapa ninao kuku wa nne wanaatamia na mwingine anataga je hao vifaranga vipya naweza kuvichanganya katika kuku wapya watakaototolewa Bila madhara yoyote kwa hao vifaranga chotara
yah unaweza kuwachanganya hawana shida,,,muhimu waweke sehemu yenye joto la kutosha na isiyofikiwa na wadudu wakali kama paka.....utakapo wachukua siku ya kwanza hadi ya saba unawapa maji uliyochanganya glucose na antibiotic ya OTC 20% ili kuwakinga na maambukizi yanayoweza tokea hadi siku ya saba unawachanja chanjo ya newcastle.....
 
yah unaweza kuwachanganya hawana shida,,,muhimu waweke sehemu yenye joto la kutosha na isiyofikiwa na wadudu wakali kama paka.....utakapo wachukua siku ya kwanza hadi ya saba unawapa maji uliyochanganya glucose na antibiotic ya OTC 20% ili kuwakinga na maambukizi yanayoweza tokea hadi siku ya saba unawachanja chanjo ya newcastle.....
Ahsantee mkuu nakusumbua ila naamini Kuna wengine wanapata somo pia sasa kama nitawachanganya si watalelewa pamoja na hawa waliototolewa maana yake joto atapata kupitia huyu tetea au Kuna namna nyingine ya kuwapatia joto
 
Nimesoma makala yako kwa undani but mengine si kweli.n imegundua pia unavutia biashara yako pia!
Kwa mfano mm nilianza na kuku 3,majike 2 na dume 1 wa kienyeji.ilikua mwisho wa mwezi wa 12 mwaka jana 2015. But mpaka mwez wa sita mwaka huu nilikuwa nimepata kuku zaid ya 60. Kuku wangu wanataga wastan wa mayai 15-18. Na kila baada ya miezi miwili ni lazima watoto.ninachokifanya vifaranga nilikua nabitunza mwenyewe toka siku ya kwanza kutotolewa .
Kuku wangu wanataga kila baada ya wiki 2 baada ya kutotoa.
Tena nimegundua njia nzuri ya kuku wa kienyeji kutotoa vifaranga kuanzia 20-24. Kwa wakati mmoja na kwa kuku mmoja.
Kuku wa kienyeji wanalipa kama itaamua kukomaa na kufuata maelekezo.
Ufugaji wa kuku wa kienyeji una changamoto zake japo zinaweza tatulika pia.
Mkuu. Njia gani hiyo unayoitumia mpka kuku wa kienyeji wanataga mayai 20-24. Msaada tafadhali mkuu
 
Nimesoma makala yako kwa undani but mengine si kweli.n imegundua pia unavutia biashara yako pia!
Kwa mfano mm nilianza na kuku 3,majike 2 na dume 1 wa kienyeji.ilikua mwisho wa mwezi wa 12 mwaka jana 2015. But mpaka mwez wa sita mwaka huu nilikuwa nimepata kuku zaid ya 60. Kuku wangu wanataga wastan wa mayai 15-18. Na kila baada ya miezi miwili ni lazima watoto.ninachokifanya vifaranga nilikua nabitunza mwenyewe toka siku ya kwanza kutotolewa .
Kuku wangu wanataga kila baada ya wiki 2 baada ya kutotoa.
Tena nimegundua njia nzuri ya kuku wa kienyeji kutotoa vifaranga kuanzia 20-24. Kwa wakati mmoja na kwa kuku mmoja.
Kuku wa kienyeji wanalipa kama itaamua kukomaa na kufuata maelekezo.
Ufugaji wa kuku wa kienyeji una changamoto zake japo zinaweza tatulika pia.
Umeongea uhalisia mtupu,

1. Mfugaji anaetaka maendeleo kutokana na ufugaji wa kuku hawezi kumuacha kuku alee vifaranga kwa miezi 3 inabidi ajifunze kulea vifaranga kwa njia mbadala

2. Ni kweli kuku ukimnyang'anya vifaranga baada ya wiki 2 anataga upya

3. Si lazima kuku akitaga atamie mwenyewe, kwani kuku mkubwa anauwezo wa kutamia hadi mayai 20+, hivyo unaweza ukachagua kuku wenye maumbo makubwa wakawa wanatamia mayai yao pamoja na yanyongeza utakayoyatoa kutoka kwa kuku wengine


Kwa nyongeza tu, ukiwa na kuku 20(mitetea), unaweza ukajizalishia vifaranga 100+ kila mwezi....
 
Mkuu. Njia gani hiyo unayoitumia mpka kuku wa kienyeji wanataga mayai 20-24. Msaada tafadhali mkuu
Mkuu nimesema kuku wangu hutaga wastan wa mayai 15-18 hivyo mayai mengine hua nanunua kukamilisha lengo langu.kwa hio kama atakuwa ametaga mayai 15 hapo naongeza mayai 10 ili niweze pata vifaranga 20+.
 
Umeongea uhalisia mtupu,

1. Mfugaji anaetaka maendeleo kutokana na ufugaji wa kuku hawezi kumuacha kuku alee vifaranga kwa miezi 3 inabidi ajifunze kulea vifaranga kwa njia mbadala

2. Ni kweli kuku ukimnyang'anya vifaranga baada ya wiki 2 anataga upya

3. Si lazima kuku akitaga atamie mwenyewe, kwani kuku mkubwa anauwezo wa kutamia hadi mayai 20+, hivyo unaweza ukachagua kuku wenye maumbo makubwa wakawa wanatamia mayai yao pamoja na yanyongeza utakayoyatoa kutoka kwa kuku wengine


Kwa nyongeza tu, ukiwa na kuku 20(mitetea), unaweza ukajizalishia vifaranga 100+ kila mwezi....
Kuna jamaa yangu mmoja alinielekeza namna nzuri ya kuku kutotoa mayai yote bila kuacha. Ni kwamba aliniambia ninunue vile vibeseni vidogo vya kunawia then ndan unaweka mchanga kiasi halafu weka mayai yako tayari kwa kuliwa na kuku. kiukweli njia hii nilitumia na imefanikiwa. kwa wafugaji wenzangu jaribuni muone maajabu yake.
Kitu kingine ni utunzaji wa vifaranga baada ya kutotolewa napo hapa kuna changamoto wakati wa usiku kutokana na barid kwa vifaranga hasa kwa wafugaji wa hali ya chini,mm mwanzo nilihangaika but nikapata njia nyingine bora ya kutunza vifaranga wakati wa usiku,nilitenga sehm ya kuwalaza. Hapa unaweza chukua hata box kubwakubwa la kuwatisha vifaranga then nikatafuta chungu!! Nikaweka majivu ndani kwa hio kila usiku nilikua unaweka mkaa wa moto mle ndani ya chungu na kufunika na majivu!! Nakwambieni ndugu zangu wafugaji vifaranga hawapati barid kabisaaa! Na huo moto ulioko ktk hilo jivu utaukuta mpka asubuhi na utatumia kwa kuwashia moto hapo kwa nyumba yako. jaribuni na njia hii muone mafanikio yake na si kukaa ohhh nitanunua vifaranga 500 nianze hapana anza hata na kuku 2 au 3 baada ya mda utakuja nambia. Yangu ni hayo labda hujaelewa uliza tupeane maujuzi.
 
Nimesoma makala yako kwa undani but mengine si kweli.n imegundua pia unavutia biashara yako pia!
Kwa mfano mm nilianza na kuku 3,majike 2 na dume 1 wa kienyeji.ilikua mwisho wa mwezi wa 12 mwaka jana 2015. But mpaka mwez wa sita mwaka huu nilikuwa nimepata kuku zaid ya 60. Kuku wangu wanataga wastan wa mayai 15-18. Na kila baada ya miezi miwili ni lazima watoto.ninachokifanya vifaranga nilikua nabitunza mwenyewe toka siku ya kwanza kutotolewa .
Kuku wangu wanataga kila baada ya wiki 2 baada ya kutotoa.
Tena nimegundua njia nzuri ya kuku wa kienyeji kutotoa vifaranga kuanzia 20-24. Kwa wakati mmoja na kwa kuku mmoja.
Kuku wa kienyeji wanalipa kama itaamua kukomaa na kufuata maelekezo.
Ufugaji wa kuku wa kienyeji una changamoto zake japo zinaweza tatulika pia.
Getting interesting. Hata mm mfugaji mtarajiwa wa kuku napata masomo hapa.
 
Kumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani. Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.


Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.

Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)
Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai).

Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.

Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.


Bei juu kwa mayai ya kienyeji

Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka. Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households. (soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.

Biashara ya Nyama.
Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni. Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15000-20000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7500-8000. Hivyo basi. hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.

Nini kifanyike.
Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini. Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji). Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.

Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.

Mapungufu.
Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.



Neno la kufungia.

“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb

Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,


Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.backyard.co.tz

Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango

View attachment 385750 View attachment 385751 View attachment 385752 View attachment 385753 View attachment 385754
Asante kwa elimu nzuri uliyotoa nimekuelewa mkuu.
 
wanauza vifaranga hawauzi wakubwa bei ni 500 kwa kifaranga wakati niliponunua mwezi wa 3 mwaka huu nazani hawajapanda kama wamepanda c ghali sana
Wapi naweza kupata vifaranga chotara kama 200
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom