uporo wa wali ndondo
JF-Expert Member
- Dec 3, 2013
- 3,455
- 2,237
Bravo, watanzania tuamke na tufanye, utafiti mkubwa umefanywa juu ya huyu kuku hapa Tanzania, ni aibu kufanya mazoeaN
Nyongeza ndogo kwenye eneo la uzalishaji.Kuku huatamia mayai kwa siku 21.Fuatilia tarehe ya kwanza ya kuku wako wanapoanza kuatamia,jifunze mbinu za kuwafanya kuku wako waanze kuatamia na kutotoa kwa wakati mmoja.Mfano una kuku 10,unawalazimisha kuku 5 waanze kuatamia kwa pamoja (rejea masomo ya nyuma juu ya ufugaji wa kuku wa asili/kienyeji).
Siku ya 21 alfajiri wanyang'anye kuku waliokuwa wanaatamia vifaranga vyao kabla havijatoa milio,wape mayai mengine.Hawatatoka hapo hadi siku nyingine 21 zifike na watotoe vifaranga vingine.Wanyanyang'anye vifaranga na kuwaachilia wapumzike.Ukiwatunza kwa chakula cha uhakika na kinga za magonjwa majuma mawili/matatu wataanza kutaga tena.Idadi ya vifaranga na mayai atakayokupatia kila kuku haitakuwa ya mazoea.
Kanuni rahisi ni (1) Jua kitu cha kufanya (2) Jua namna ya kufanya (3) Kifanye.
Mambo haya hatupaswi kuyaweka hadharani kiasi hiki.Tanzania wengi wetu hatua ya kwanza na ya pili tupo vizuri sana ,tatizo lipo kwenye hatua ya tatu.Kenya kwenye hatua ya kwanza na pili wapo dhaifu kuliko sisi ila hatua ya tatu wametuacha mbali ndiyo maana baadhi yetu hatutaki kuweka kila kitu hadharani.
Tunalenga kufundishana wenyewe wanafaidi wapita njia kwa tuliyofundishana kisha wanaanza kutucheka nasi tunashangilia.
Ninaposema breed selection maana yake ni wewe kwenda kitaa kuchagua kuku wa kienyeji wakubwa,mf, kuchi, hii inachukua miaka mingapi?, hawa ukiwasupplement they are always big and heavier comparatively. My take: mleta mada ni copy cat na hajafanya consultation yoyote kwa wataalam, huu ni ugonjwa sugu kwa wajasiliamali wengi.
Addendum: hata kupeleka yai bovu sokoni kwa zama hizi ni aibu kwani kuna candling touch inayokuwezesha kujua kama yai ni bovu ama la, kauli ya mleta mada kuwa yai LA kienyeji (lililorutubishwa) huharibika haraka viz aviz lisilorutubishwa ni ulongo mtupu, the fact is yai lolote ukilitunza kwenye shelf temperature kama ya pwani huharibika haraka.
Kuhusu size ya kuku: kumbuka kuwa hata hawa kuku wa kisasa wanabodysize tofauti so is egg size na egg laying, kwa broiler for instance Ross ni wadogo kuliko arboacres, big dealers huchagua lines wa kufuga na siyo kujifugia tu
Makala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.Kumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani.
Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.
Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.
Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)
Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.
Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai)
Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.
Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.
Bei juu kwa mayai ya kienyeji
Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka.
Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households(soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. Kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.
Biashara ya Nyama
Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni.
Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15,000-20,000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7,500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7,500-8,000.
Hivyo basi, hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.
Nini kifanyike?
Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). Hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini.
Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji).
Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.
Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.
Mapungufu
Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. Hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. Kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.
Neno la kufungia:
“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb
Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,
Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.backyard.co.tz
Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango
View attachment 385750
View attachment 385751
View attachment 385752
View attachment 385753
View attachment 385754
bantulileMakala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.
Nadhani, pamoja na andiko lako zuri unahitaji kwenda zaidi ya hapo ulipofikia.
Mimi nimewahi kuanza kufuga kuku mmoja wa kienyeji. Akataga mayai 11 na akatotoa vifaranga 11. Kwa bahati mzuri vifaranga wote wakakua kufikia kuanza kuataga. Nikawauza kwa bei ya shs 2500 kwa wakati huo. 2500x10= 25000. Nikanunua nguruwe. Baada ya miezi 6 nikampandisha na baada miezi minne nguruwe akazaa piglets 11 @ 10, 000 maana bei ilikwisha panda nikapata 110,000 nikanunua ngombe crossbreed na Mpwapwa na Fresian. Binafsi niona hayo ni maendeleo kuanzia na kuku mmoja wa kienyeji.
Mtandaoni hatudanganyani ila tunachosema ni kuwa ukiwa mtaji mdogo unaweza kufanya kitu. Development by definition means change. Change from one inferior stage to another a bit supperior stage. Tunataka kila mtu ajione anaweza hata yule aliyekuwa anafikiria everything is imposible aone angalao hili kwa kiasi hiki anaweza
Makala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.
Nadhani, pamoja na andiko lako zuri unahitaji kwenda zaidi ya hapo ulipofikia.
Mimi nimewahi kuanza kufuga kuku mmoja wa kienyeji. Akataga mayai 11 na akatotoa vifaranga 11. Kwa bahati mzuri vifaranga wote wakakua kufikia kuanza kuataga. Nikawauza kwa bei ya shs 2500 kwa wakati huo. 2500x10= 25000. Nikanunua nguruwe. Baada ya miezi 6 nikampandisha na baada miezi minne nguruwe akazaa piglets 11 @ 10, 000 maana bei ilikwisha panda nikapata 110,000 nikanunua ngombe crossbreed na Mpwapwa na Fresian. Binafsi niona hayo ni maendeleo kuanzia na kuku mmoja wa kienyeji.
Mtandaoni hatudanganyani ila tunachosema ni kuwa ukiwa mtaji mdogo unaweza kufanya kitu. Development by definition means change. Change from one inferior stage to another a bit supperior stage. Tunataka kila mtu ajione anaweza hata yule aliyekuwa anafikiria everything is imposible aone angalao hili kwa kiasi hiki anaweza
nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.Ginner
Nimekuelewa Mkuu vizur sana
Ila napenda kukusahihisha kidogo kwenye utagaji mayai kwa kuku wa kienyeji
Kwa uzoefu wangu wa miaka mitano kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji, kuku mmoja jike kwa mwaka anaweza kutaga mayai 150.
Ninachokifanya mimi kuku akianza kutaga huwa nampunguzia mayai hadi idadi ninayoitaka ikamilike ndo nampatia mayai yote tayari kwa kuatamia.
Then akitotoa ninamwacha wiki moja akilea vifaranga baada ya hapo namtoa kwenye chumba cha kulelea vifaranga [namwacha huru] akitoka nje hukaa wiki moja kisha huanza kutaga tena.
Ina maana ukizungusha hivyo kwa mwaka kuku mmoja anaweza kukupa vifaranga 150~ 200
Sema Changamoto Iko Kwenye Soko
Nawasilisha...
Samahani kuu naomba nitoe uzoefu wangu kwa hili la mayai.nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.
Mwaka una wiki ngapi? 52nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.
Ahsante sana kwa kunirekebishia hiyo hesabu!jumla ya wiki ni 7.
52÷7 ~ 8.
8 x 12 ~ 96.
kwa mwaka.
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful
Mayai ya kanga mimi ndiye mzalishaji mkubwa na nakaa Dodoma. Kwa uzoefu wangu kanga hutaga kuanzia mwezi wa kumi mpaka may maka unaofuata. Kwa sasa kanga wamenipungua sana ninao kama mia mbili na ushee. Katika msimu wa utagaji huwa sikosi trei tatu kwa siku na yai moja nauza mia tano. Ukipenda vifaranga pia utapata kwani ninayo mashine ndogo ya kutotoresha yenye uwezo wa mayai 96, na kifaranga kimoja nauza sh 1500 cha siku moja. Kikifika kipindi hicho tuwasiliane kwa simu na 0786775663 /0757284076 /0715557342 . Pia ninafuga kuku wa kienyeji ( crosbreed) kwa sasa ninao zaidi ya mia tatu na pia nafuga bata mzinga ila soko linanishawishi kuacha kuwafuga.Jamani nahitaji mayai ya kanga, please
ni kweli kabisa... ni ubunifu na kufata taratibu za ufugaji... hawa kuku hawawezi kua na hasara.safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful