Ushuhuda kilichonitokea Kona Bar Sinza, Dar es Salaam

illegal migrant

JF-Expert Member
Oct 18, 2013
1,277
1,119
Nilikuja Dar kwenye biashara fulani, mida ya jioni nikatafuta bodaboda nikamueleza sehemu ambayo ninaweza kwenda kupumzika na kupunguza msongo, akaniambia kuna sehemu Sinza panaitwa Kona Bar pamesheheni kila aina ya burudani hata kama biashara hazi kwenda vyema naweza kujifariji.

Tukaelekea mpaka Kona Bar aiseee niliona idadi kubwa sana ya warembo wakiwa katika hali ya ujasiriamiili, nilikaa nje kwa muda nikiwa napata chakula na kinywaji. Alipita dada mmoja nikashindwa kujizuia, nikamwita baada ya salamu hakutaka maneno mengi Bali alinipa bei ya huduma anazotoa, muda mfupi 20000 kulala 40000, nilienda naye kwa huduma ya muda mfupi akanionyesha gesti ambayo gharama zake ni shilingi elfu tano kwa muda mfupi, na nikakuta kuna msururu wa watu wanaingia na kutoka.

Tukapewa chumba Chetu tukaingia wakati naanza kufungua zipu nikasikia makelele chumba cha pili kama mtu alikuwa anapigwa nikashtuka kidogo, ndio nikagundua walikuwa ni Askari. Sikuweza kuendelea kufanya chochote, mlango wetu uligongwa kwa nguvu nikafungua akatokea mtu mwenye Miraba minne aliyevaa sare za Askari mwenye cheo cha mbavu tatu.

Nilifungwa pingu nikapelekwa kwenye gari aina ya Noah ambapo huko nikakuta kuna Askari pamoja wazinzi wengine wengi wamekamatwa. Cha kusikitisha ni kuwa kila mtu alikuwa amekamatwa na ushahidi yaani mwanaume na mwanamke ila mimi nilikuwa pekee yangu nikagundua Askari yule baada ya kunikabidhi kwenye Noah alirudi chumbani “kumalizana” na dada yule.

Baada ya muda tulianza kuelekea kituo cha polisi ambacho nilikitambua kwa jina la Mabatini, jamaa mmoja aliyevaa kiraia alisema tunaenda kupigwa picha kisha zinawekwa kwenye mitandao kauli hii ilizua vurugu kubwa na ukumbuke wanaume tulikuwa tumefungwa pingu, tulifika kituoni Majira ya saa kumi alfajiri ambapo hatukushushwa kwenye gari bali Askari yule aliyetukamata mwenye mbavu tatu ambaye nilimtambua kwa jina linalofanana na la Waziri Mkuu wa sasa alituambia kuwa tutoe laki kila mmoja, tuliweza kujitetea kila mmoja na uwezo wake wa ushawishi tukaachiwa ila wanawake wooote hatukujua walienda wapi.

Mwisho
 
Nakupa siri ya kazi hapa..

usilale guest au lodge uliyochaguliwa na mwanamke asiye mkeo..
ukilala na mwanamke usiyemjua hakikisha funguo unajua wewe ulipoziweka..
usiokoteokote mwanamke ukampeleka kwako.
Uwe makini na Camera ya uliyelala naye..
Ukimwaga maji yako hakikisha yako salama..(dunia ina mengi hii vijana mkue sasa).

KUCHEPUKA NI GHARAMA UKITAKA UNAFUU NI RISK SANA, OTHERWISE CHAGUA UMPENDAYE MFUNGE PINGU MTAFUNANE MTAKAVYO, CHUMBANI, SEBULENI, JIKONI, BAFUNI, MZINGATIE LISHE BORA TU..
 
Nakupa siri ya kazi hapa..

usilale guest au lodge uliyochaguliwa na mwanamke asiye mkeo..
ukilala na mwanamke usiyemjua hakikisha funguo unajua wewe ulipoziweka..
usiokoteokote mwanamke ukampeleka kwako.
Uwe makini na Camera ya uliyelala naye..
Ukimwaga maji yako hakikisha yako salama..(dunia ina mengi hii vijana mkue sasa).

KUCHEPUKA NI GHARAMA UKITAKA UNAFUU NI RISK SANA, OTHERWISE CHAGUA UMPENDAYE MFUNGE PINGU MTAFUNANE MTAKAVYO, CHUMBANI, SEBULENI, JIKONI, BAFUNI, MZINGATIE LISHE BORA TU..
Ushauri mbaya umechanganyikana na uzuri, humo humo.. kama makande,inabidi achague binzi aweke kulia na maize kushoto!!!
 
Back
Top Bottom