Optimists
JF-Expert Member
- Oct 17, 2021
- 278
- 686
Kijana wenu baada ya kumaliza chuo nikaona nijimix kwenye harakati za maisha nipo Dar es Salaaam japo Nina mda mfupi sana hapa.
Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.
Nilifanikiwa kupita tandale Sokoni kuna soko kubwa linajengwa. kwa nje kuna wafanyabiashara weengi sana nikaanza kufanya research kuhusu biashara ya Mchele kwamba nautoa Mbeya then nawapa madalali wananiuzia, kwa vile niliona sihitaji kutafuta eneo la kazi wala mizani ngoja nianze kufanya hizo issue za kuuza Mchele.
Awali ya yote nilienda pale mwananyamala Sokoni nikakutana na wafanyabiashara wakubwa wa Mchele pale wakaanza kuniambia mwenyewe pale kila kilo waliochukulia mbeya wanapata faida tsh 30_50 yaani anauchukua mbeya kwa 1100 kila kilo kufika Sokoni anauza 1250/1300 akiondoa gharama zake zoote anapata faida hiyo (sema hao wana mitaji mikubwa saana).
Turudi tandale sokoni.
Mimi kwa sababu sikua na mtaji Mkubwa nilikua na around laki 7 nikajitosa kwenda kununua Mchele mzuri sio super saana ila ni mzuri.
Nilichukua mbeya kwa 1300 nikachukua kama kilo 500 total inakua ni 650,000 ukiondoa na gharama zoote na usafiri unajikuta umetumia laki saba na ishirini (720k).
Kufika Sokoni nilitaka niuze kwa 1750@ kilo ili nirudishe gharama zangu lakini naona watu wengi wanahitaji kwa 1600-1650 na mwingine anakwambia umuuzie kwa 1300/1400.
Changamoto nyingine unaweza shusha mzigo Mkubwa kama gunia 30 ukawa unauza 1300 kwa kilo, kesho yake anakuja mwingine anashusha Mchele kama wako anauza 1000/1100 kwa kilo inakua changamoto.
Nilichogundua kwenye hii biashara wafanyabiashara wengi ambao wanauza wenyewe wengi wanachanganya mzigo anachukua Mchele super then anachanganya na Mchele mbaya kwa macho mteja hawezi kugundua kwa haraka.
Pia hii biashara kama unataka uone faida yake ni basi inafaa uwe na mtaji Mkubwa sana la sivyo wakuu mambo yatakua ni mazito sana..
Ombi la mwisho wakuu, huo Mchele wangu kwa atakae hitaji anicheck whatsap au normal text kwa namba hii 0757590836 free delivery nitakuletetea popote pale nataka nirudishe gharama yangu nirudi kijijini nikalime.
Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.
Nilifanikiwa kupita tandale Sokoni kuna soko kubwa linajengwa. kwa nje kuna wafanyabiashara weengi sana nikaanza kufanya research kuhusu biashara ya Mchele kwamba nautoa Mbeya then nawapa madalali wananiuzia, kwa vile niliona sihitaji kutafuta eneo la kazi wala mizani ngoja nianze kufanya hizo issue za kuuza Mchele.
Awali ya yote nilienda pale mwananyamala Sokoni nikakutana na wafanyabiashara wakubwa wa Mchele pale wakaanza kuniambia mwenyewe pale kila kilo waliochukulia mbeya wanapata faida tsh 30_50 yaani anauchukua mbeya kwa 1100 kila kilo kufika Sokoni anauza 1250/1300 akiondoa gharama zake zoote anapata faida hiyo (sema hao wana mitaji mikubwa saana).
Turudi tandale sokoni.
Mimi kwa sababu sikua na mtaji Mkubwa nilikua na around laki 7 nikajitosa kwenda kununua Mchele mzuri sio super saana ila ni mzuri.
Nilichukua mbeya kwa 1300 nikachukua kama kilo 500 total inakua ni 650,000 ukiondoa na gharama zoote na usafiri unajikuta umetumia laki saba na ishirini (720k).
Kufika Sokoni nilitaka niuze kwa 1750@ kilo ili nirudishe gharama zangu lakini naona watu wengi wanahitaji kwa 1600-1650 na mwingine anakwambia umuuzie kwa 1300/1400.
Changamoto nyingine unaweza shusha mzigo Mkubwa kama gunia 30 ukawa unauza 1300 kwa kilo, kesho yake anakuja mwingine anashusha Mchele kama wako anauza 1000/1100 kwa kilo inakua changamoto.
Nilichogundua kwenye hii biashara wafanyabiashara wengi ambao wanauza wenyewe wengi wanachanganya mzigo anachukua Mchele super then anachanganya na Mchele mbaya kwa macho mteja hawezi kugundua kwa haraka.
Pia hii biashara kama unataka uone faida yake ni basi inafaa uwe na mtaji Mkubwa sana la sivyo wakuu mambo yatakua ni mazito sana..
Ombi la mwisho wakuu, huo Mchele wangu kwa atakae hitaji anicheck whatsap au normal text kwa namba hii 0757590836 free delivery nitakuletetea popote pale nataka nirudishe gharama yangu nirudi kijijini nikalime.