Kuna mkakati wa kuanzisha ushirikiano mpya wa vyama vya upinzani nchini kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2020 lengo likiwa ni kuing’oa CCM madarakani, utakaojulikana kama, The United Democratic Front (DeFront) au (U-Front).
Wazo hilo lilitolewa wakati vyama 10 vya upinzani vilipokutana Zanzibar na kutoa Azimio la Zanzibar, na huenda hatua ya Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alikuwa muumini wa UKAWA kuhamia rasmi ACT- Wazalendo kumekoleza chachu ya vyama hivyo kutaka kuungana.
Wazo la ushirikiano huo linaweza kufanana na wazo la Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe la kuanzisha muungano mpya wa ushirikiano wa vyama vya upinzani, The United Democratic Front (DeFront).
Zitto alieleza kuwa ana dhamira ya kuona vyama vya upinzani na taasisi nyingine mbalimbali zikiunganisha nguvu dhidi ya CCM katika chaguzi mbalimbali.
Ushirikiano huo wa vyama unaelezwa kuwa mbadala ya UKAWA ya sasa.
Kwa mujibu wa Mwanachama mpya wa ACT, Nassor Ahmed Mazrui ambaye kabla ya kuhamia ACT alikuwa naibu katibu mkuu wa CUF, amesema ushirikiano unaotakiwa kujengwa sasa unapaswa uwe zaidi ya vyama vya siasa kutokana na hali halisi iliyopo.
“Sasa waathirika ni wengi ukilinganisha na vipindi vingine, wafanyabiashara, waandishi wa habari, wanawake na makundi mbalimbali yameumizwa; tunahitaji mabadiliko ya haraka na siyo tu kuwa na muungano wa vyama vya siasa pekee badala yake tunapaswa kuhusisha na taasisi za kiraia.
Kwa upande wake Naibu katibu mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu amesema kwa sasa majadiliano ni namna gani vyama hivyo vitashirikiana kufanya kazi pamoja baada ya azimio lile la Zanzibar.
“Inaweza isiwe UKAWA tena na kuwa kitu kingine kabisa, pengine vyama vikaamua kuongeza chama kimoja au vyote, hii itajulikana baada ya vyama kutoa mapendekezo yake na kujadiliwa kwa pamoja pindi tutakapokutana.”
Chanzo Mwananchi.
Ushirikiano mpya upinzani kuzaliwa
Wazo hilo lilitolewa wakati vyama 10 vya upinzani vilipokutana Zanzibar na kutoa Azimio la Zanzibar, na huenda hatua ya Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alikuwa muumini wa UKAWA kuhamia rasmi ACT- Wazalendo kumekoleza chachu ya vyama hivyo kutaka kuungana.
Wazo la ushirikiano huo linaweza kufanana na wazo la Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe la kuanzisha muungano mpya wa ushirikiano wa vyama vya upinzani, The United Democratic Front (DeFront).
Zitto alieleza kuwa ana dhamira ya kuona vyama vya upinzani na taasisi nyingine mbalimbali zikiunganisha nguvu dhidi ya CCM katika chaguzi mbalimbali.
Ushirikiano huo wa vyama unaelezwa kuwa mbadala ya UKAWA ya sasa.
Kwa mujibu wa Mwanachama mpya wa ACT, Nassor Ahmed Mazrui ambaye kabla ya kuhamia ACT alikuwa naibu katibu mkuu wa CUF, amesema ushirikiano unaotakiwa kujengwa sasa unapaswa uwe zaidi ya vyama vya siasa kutokana na hali halisi iliyopo.
“Sasa waathirika ni wengi ukilinganisha na vipindi vingine, wafanyabiashara, waandishi wa habari, wanawake na makundi mbalimbali yameumizwa; tunahitaji mabadiliko ya haraka na siyo tu kuwa na muungano wa vyama vya siasa pekee badala yake tunapaswa kuhusisha na taasisi za kiraia.
Kwa upande wake Naibu katibu mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu amesema kwa sasa majadiliano ni namna gani vyama hivyo vitashirikiana kufanya kazi pamoja baada ya azimio lile la Zanzibar.
“Inaweza isiwe UKAWA tena na kuwa kitu kingine kabisa, pengine vyama vikaamua kuongeza chama kimoja au vyote, hii itajulikana baada ya vyama kutoa mapendekezo yake na kujadiliwa kwa pamoja pindi tutakapokutana.”
Chanzo Mwananchi.
Ushirikiano mpya upinzani kuzaliwa