Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
USHETU: WAFUGAJI KUTENGEWA MAENEO YA MALISHO HALMASHAURI YA USHETU
Serikali imeahidi kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wafugaji katika halmasahauri ya Ushetu Wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga ili kuondoa migogoro kati yao na Wakulima.
Kauli hiyo imetolewa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI (Afya) Dkt. Festo Dugange wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani aliyetaka Serikali kutuma Wataalam kwenda kuyapitia maeneo ya hifadhi ya misitu yaliyopo katika halmashauri hiyo na kutenga maeneo hayo ili kuondoa migogoro hiyo.