Ushawahi kula chakula cha ajabu ugenini? Ulichukua hatua gani?

mpasta

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
917
1,997
Waswahili wanasema "Msafiri Kafiri" na "kuku mgeni hakosi kamba mguuni". Hii misemo yote inaelezea tabu na adha unayoweza kukutana nayo ukiwa safarini au ugenini.

Leo nimetafakari juu ya homa ya MGUNDA iliyoibuka Mkoa wa Lindi, nikakumbuka kisa nilichowahi kusimuliwa na marehemu Mjomba wangu mwaka 1995. Mjomba alimuoa shangazi mtu wa Nyasa, Ruvuma. Sasa walipofunga ndoa baada ya miezi kadhaa akampeleka shangazi kijijini Masasi kusalimia wakweze.

Huko ndio kisa mkasa kikaibuka Bwana. Walifika usiku usiku, asubuhi na mapema, Mama mkwe akamuuliza shangazi kama anakula Kima. Shangazi akajibu hana shida anapenda sana kima. Baba mkwe alitoka Nae Asubuhi na mapema na bunduki yake kwenda porini. Mjomba na Shangazi nao wakaondoka kwenda kusalimia ndugu na jamaa pale kijijini. Waliporudi mchana wamekuta mama mkwe anababua nyama ya nyani/kima kwenye moto.

Mchana kufika ukapikwa ugali kwa nyani/kima. Unaambiwa kichwa cha nyani na meno yake yupo kwenye supu kaletwa mkekani. Unaambiwa shangazi kuona ile mboga akatapika hapo hapo mkekani kwa kichefuchefu. Ikabidi Mjomba awaambie kuwa huyu hali nyama ya nyani. Mama mkwe akajitetea mbona nimemuuliza asubuhi kama anakula Kima akanijibu anakula. Shangazi ndio akafafanua kuwa alijua nyama ya kusaga hakudhani kama kima ni nyani

Kusini bana kunalika vyakula vya ajabu sana, ukinusurika labda uwe Muislamu au Mkristo kwelikweli ndio hutokula hivyo vyakula vya ajabu. Nadhani serikali inawajibika kupeleka miradi ya ng'ombe, mbuzi na kuku kwa wingiiii ili kuwezesha wananchi kupata vitoweo muruwaa
 
4c049e7af5c69df8053df7c6fa8e6297.jpg
 
Kuna kipindi tulikwama huko ikwiriri porini ndanindani gari liliharibika tukaenda kuomba msaada kwa mjumbe wa nyumba kumi sasa akatuambia tutalala mkekani na chakula atatupikia ilikuwa ni porini kwelikweli sasa tunakaribishwa chakula ni ugali na samaki hawa wa baharini wa kuchemsha hana kiungo chochote ile shombo sijawahi ona aisee nilishishindwa kula nikala ugali hivyo hivyo bila mboga nikala na maji. Wenyeji wanakula bila shida yeyote kabisa.
 
Kipindi nipo iringa nilisikia mwenyeji wangu anamuita mjukuu wake kuwa aende kwa fulan akanunue nyama ya 1000( buku)
Then after 5 min nakuta dg anakuja na kilo ya nyama......kwa vile nmesoma Cuba. Nlinotice kuwa man down mwamba nakula hapa....

Sema nliinjoy baada ya kusikia akiita .....we enjoy.....Leo utalala na mgeni

Anyway sikutumia hata Kinga.....
 
Kipindi nipo iringa nilisikia mwenyeji wangu anamuita mjukuu wake kuwa aende kwa fulan akanunue nyama ya 1000( buku)
Then after 5 min najuta dg anakuja na kilo ya nyama......kwa vile nmesoma Cuba. Nlinotice kuwa man down mwamba nakula hapa....

Sema nliinjoy baada ya kusikia akiita .....we enjoy.....Leo utalala na mgeni

Anyway sikutumia hata Kinga.....
Fwalaaa sanaaa, hahaha...fun sana.
 
Kipindi nipo iringa nilisikia mwenyeji wangu anamuita mjukuu wake kuwa aende kwa fulan akanunue nyama ya 1000( buku)
Then after 5 min najuta dg anakuja na kilo ya nyama......kwa vile nmesoma Cuba. Nlinotice kuwa man down mwamba nakula hapa....

Sema nliinjoy baada ya kusikia akiita .....we enjoy.....Leo utalala na mgeni

Anyway sikutumia hata Kinga.....
 
Kipindi nipo iringa nilisikia mwenyeji wangu anamuita mjukuu wake kuwa aende kwa fulan akanunue nyama ya 1000( buku)
Then after 5 min najuta dg anakuja na kilo ya nyama......kwa vile nmesoma Cuba. Nlinotice kuwa man down mwamba nakula hapa....

Sema nliinjoy baada ya kusikia akiita .....we enjoy.....Leo utalala na mgeni

Anyway sikutumia hata Kinga.....
Kwani si ulitakiwa utuambie chakula tu jamaa
 
Kusini bana kunalika vyakula vya ajabu sana, ukinusurika labda uwe Muislamu au Mkristo kwelikweli ndio hutokula hivyo vyakula vya ajabu.
😅😅😅 mimi sio muislamu wala mkristo ila siwezi kula hivyo vyakula vya ajabu as a vegetarian🥰
 
Back to 2011 zenji hiyo kitope hiyo nilikaribishwa nyama ya kenge mi nilijua samaki baada ya kumaliza kula kuzunguka nyuma ya nyumba kwa kupata hewa nakuta mabaki ... oyaa bonge la kengee.. ila mtamu balaaa
Pole, ila hamna ambacho hakiliwi..ni mapokeo tu ya sehemu na sehemu
 
Back to 2011 zenji hiyo kitope hiyo nilikaribishwa nyama ya kenge mi nilijua samaki baada ya kumaliza kula kuzunguka nyuma ya nyumba kwa kupata hewa nakuta mabaki ... oyaa bonge la kengee.. ila mtamu balaaa🤣
Jamaa katuhadithia alikuwa Mombasa akajenga urafiki na Wapemba flani wavuvi, siku moja akakuta msosi unapikwa wakamwambia wakimaliza kuswali ajongee wale chakula cha mchana. Jamaa anasema kilikuwa kitamu sana. Kumaliza anawauliza mmempata wapi huyu kuku, wakamwambia ni kenge huyo Yakhe!
 
2018 hiyo kwenye pori fulan kaskazin tulienda kulima na unga na dagaa tu alaf tukakaa miez mi3 mbugan usafiri tulio nao ni trekta tu tulikula dagaa za kuchemsha Hadi nikazichukia
Muhuni mmoja akawinda fisi ikakatwa kichwa na miguu ikafukiwa porin alaf mnyama akaja kashachunwa ngozi na kutolewa takataka zote

Tulichoma tukala nyama choma fresh nmekuja kugundua nimekula fisi siku za karibuni nikauliza masheikh vipi? Fisi anaruhusiwa kuliwa? Nikaambiwa haina noma siyo haram, natamani nikawinde tena siku moja mtamu sana
 
2018 hiyo kwenye pori fulan kaskazin tulienda kulima na unga na dagaa tu alaf tukakaa miez mi3 mbugan usafiri tulio nao ni trekta tu tulikula dagaa za kuchemsha Hadi nikazichukia
Muhuni mmoja akawinda fisi ikakatwa kichwa na miguu ikafukiwa porin alaf mnyama akaja kashachunwa ngozi na kutolewa takataka zote

Tulichoma tukala nyama choma fresh nmekuja kugundua nimekula fisi siku za karibuni nikauliza masheikh vipi? Fisi anaruhusiwa kuliwa? Nikaambiwa haina noma siyo haram, natamani nikawinde tena siku moja mtamu sana
 
Kwa historia nina miaka kadhaa sijaenda kijijini, nimeishi mjin almost kama miaka 10 japokuwa kwa wazee naenda ila sio kiivo na hom kidogo hata kama ni kijijin ila kwenye suala la mapishi wanajitaidi, sasa siku hiyo nimeenda kumtembelea mwanangu tuliosoma nae nikapewa Ugali na mboga aina ya Sukuma wiki nahis ni kamii ya chaineeze, sasa zile mboga zimepikwa mchemsho bila mafuta wala kitunguu na nyanya, na ugali wa mhogo uliochanganywa na mtama, Picha linaanza kwanza mwanangu tulikuwa nae alivyoona ule ugali akajua mkate ile kutia mdomoni tu nikaona anatema anatupa aibu ikanikamata sana maana wazee wetu wa vijijini hawachelewi kukusema kama mnalinga, kibarua kikarudi kwangu inatakiwa nile nikajitahidi nikamega tonge nikachukua mboga kumeza ngoma ikifika kooni inapanda yenyewe juu kurudi nje jitahid kumeza ila ngoma ikifika kooni inapanda, kukagua wote hawanioni nikatema nikaweka mfukoni fasta, kisha nikanawa nikawaambia kiuzuri tu nimejitahidi kula maana hom ndio natoka kula walinielewa ila kishingo upande ila nikashukuru! Kibaya nikaondoka kuja hom nikasahau kutoa lile tonge mfukoni hadi wife alipochukua kufua nguo ndio akalipata nae, na ndio tulikuwa tumeenda kijijini kwa wazee wote wife nae ikabid anitunzie maana hakuelewa ni kitu gani alijua pengine ni hirizi ila baadae ndio akaniuliza nikamsimlia mkasa wote ila ilikuwa fedheha sana kwa kweli na sikupenda ile hali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom