Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kuna nyumba ambazo ukiangalia maisha ya wanaoishi ndani ya nyumba hizo huwezi kuzitofautisha na danguro. Hebu fikiria nyumba ambazo watoto wa kike wanaingiza marafiki zao wa kiume na kufanya nao mapenzi humo, iwe mchana au usiku. Watoto wa kiume nao ni kama hao dada zao nao huja na wanawake zao na kufanya nao mapenzi humohumo ndani ya nyumba.
Lakini hata baba naye akipata mwanamke wa kupitisha naye usiku hujivinjari naye ndani ya nyumba hiyo hiyo. Kama ni mama, akiibua buzi lake huko atokako atakuja nalo na kufanya nalo mapenzi humo humo ndani ya nyumba ya familia huku watoto wakishuhudia. Aibu gani hii!Mara nyingi tabia hizi hujitokeza zaidi katika nyumba za mzazi mmoja. Inawezekana wazazi wameachana au mmoja amefariki, au huyo mzazi anaishi na watoto ambao alizaa kila kona na kuwakusanya hao viumbe wake na kuamua kuishi nao.
Kwa sababu, kila mtoto amelelewa kivyake huko alikotoka au kwa sababu, baada ya mzazi mmoja kufariki au kuachana, aliyebaki na watoto alishindwa kuwalea vema na sasa wamegeuka nunda halisi. Sisemi nyumba zote zenye mzazi mmoja zinakuwa hivyo, hapana. Naogopa nitasakamwa. Nazungumzia zile nyumba za mzazi mmoja ambapo mzazi huyo kwa bahati mbaya au kwa hiyari yake bila kujua ameiharibu familia kimaadili.
Bila shaka mtakuwa mnazijua familia za aina hiyo, angalau moja.Nyumba hizi ni kama nyumba ambazo ni mtaa humohumo ndani ya nyumba. Huyu anaingiza mtu wake chumba hiki na yule anaingiza mtu wake chumba kile. Kama kwamba ni watu majirani tu wanaoishi mtaa mmoja na hakuna mwenye haki ya kuuliza kuhusu maisha ya ndani ya mwingine. Kama baba au mama anafanya hivyo mbele ya watoto, unadhani atathubutu vipi kumkemea mtoto? Tena mtoto mwenyewe ameshaanza kuvuta bangi au kubwia ‘unga,' thubutu!
Lakini hata baba naye akipata mwanamke wa kupitisha naye usiku hujivinjari naye ndani ya nyumba hiyo hiyo. Kama ni mama, akiibua buzi lake huko atokako atakuja nalo na kufanya nalo mapenzi humo humo ndani ya nyumba ya familia huku watoto wakishuhudia. Aibu gani hii!Mara nyingi tabia hizi hujitokeza zaidi katika nyumba za mzazi mmoja. Inawezekana wazazi wameachana au mmoja amefariki, au huyo mzazi anaishi na watoto ambao alizaa kila kona na kuwakusanya hao viumbe wake na kuamua kuishi nao.
Kwa sababu, kila mtoto amelelewa kivyake huko alikotoka au kwa sababu, baada ya mzazi mmoja kufariki au kuachana, aliyebaki na watoto alishindwa kuwalea vema na sasa wamegeuka nunda halisi. Sisemi nyumba zote zenye mzazi mmoja zinakuwa hivyo, hapana. Naogopa nitasakamwa. Nazungumzia zile nyumba za mzazi mmoja ambapo mzazi huyo kwa bahati mbaya au kwa hiyari yake bila kujua ameiharibu familia kimaadili.
Bila shaka mtakuwa mnazijua familia za aina hiyo, angalau moja.Nyumba hizi ni kama nyumba ambazo ni mtaa humohumo ndani ya nyumba. Huyu anaingiza mtu wake chumba hiki na yule anaingiza mtu wake chumba kile. Kama kwamba ni watu majirani tu wanaoishi mtaa mmoja na hakuna mwenye haki ya kuuliza kuhusu maisha ya ndani ya mwingine. Kama baba au mama anafanya hivyo mbele ya watoto, unadhani atathubutu vipi kumkemea mtoto? Tena mtoto mwenyewe ameshaanza kuvuta bangi au kubwia ‘unga,' thubutu!