Ushauri


Nakuunga mkono kabisa mke wako anakuomba ushauri afanye nini ili former boyfriend aache kumtumia message za kimapenzi halafu unanyanyua mabega? 😕

Alitakiwa aseme chochote kukaa kwake kimya mimi sikuelewi hata kidogo. Je, huwezi kuomba kubadilisha namba yako kutokana na usumbufu unaopata toka kwa huyo jamaa?
 
.....

Sijui mahusiano yenu yakoje, labda ndivyo mnavyoishi, au mumeo anaona akianza kukasirika ipo siku utagundua madhambi yake na wewe utakasirika, hivyo anataka siku ukigundua madhambi yake wote muwe sawa.[/QUOTE]

Yani DK kama hapo ulipo BIG five, nadhani hio ndo sababu yake yakujitia kupandisha mabega ili iwe kama ngoa yake hapo baadae. Thanks so much uminishutua mshipa wa fahamu sasa. Ciao
 

Thanks so much my dear for your comments. Will try your option.
 
Ilikuchukua muda gani kabla hujamfahamisha mumeo, isije ikawa ulipoona uta shikwa ndo uliamua kumjulisha.

Ilinichukua kama two weeks hivi, ndo ikabidi nimwambie. Nilijaribu kwanza kufanya kama mlivyoniagiza kubadilisha no. na kumkanya vile vile.
 

Kaka, hapo mwanzo kabla sijaolewa nilipokuwa huko nilishabadilishaga no. yangu mara tatu hivi. Lakini alikuwa akizitafuta mpaka anazipata! Mwishoe ili bidi nimpe kaka mmoja alikuwa rafiki wa kawaida tuu ajifanye kama ndo boyfriend wangu. Basi akaongea naye na kumtaarifu asinifatefate mimi ni girlfriend wake, then ndo akaa kimya sasa. Ambapo na Mr. angefanya hivyo natumaini ingesaidia sana.
 
huyo jamaa anastahili kupigwa na kuvunjwa miguu...ni nini haswa anataka kutoka kwako? na je mlipoanza mawasiliano tena were you leading him ama ulikuwa strict toka mwanzo? Maana unaweza kuwa ulikuwa una'flirt' nae at first and when things started to get serious you decided to back off!

Regardless ni kwamba wewe msimamo wako anaufahamu na mumeo umeshampa taarifa husiana na hilo, kama kakaa kimya akiangalia kutaka jua wewe utachukua uamuzi gani na wewe unaona xya kwamba huyo jamaa ni kichwa ngumu wala hataki kukusikiliza basi unaweza lifikisha hilo suala katika vyombo vya usalama ili wachukue hatua husika.

Ila suala la kubadili namba ya simu sidhani kama ni ufumbuzi maana kutokana na maelezo yako hayo hapo hujasema alipataje namba yako ya simu mpya (inaonekana ulibadilisha namba kabla ya kuolewa ama mara baada ya kuolewa). Je alipewa na wewe ama kuna mtu alikusaidia kumpatia.

Inabidi uchukue hatua madhubuti maana huchelewi kuishia kubomoa nyumba yako changa... Kimya cha Mtu kina maana nyingi sana!
 
Ilinichukua kama two weeks hivi, ndo ikabidi nimwambie. Nilijaribu kwanza kufanya kama mlivyoniagiza kubadilisha no. na kumkanya vile vile.

Sasa hebu tueleze, Ulimwabia sababu aliuliza kiini chako kubadilisha no. Ama hata hakuulizia kwanini unabadilisha no. yako?

Sijui lakini naona pana kitu hukisemi!
 
Sasa hebu tueleze, Ulimwabia sababu aliuliza kiini chako kubadilisha no. Ama hata hakuulizia kwanini unabadilisha no. yako?

Sijui lakini naona pana kitu hukisemi!

Mi nakubaliana na Namtih58 kuna kitu hujatuambia hapa.
 
Lorain pole sana ila namimi kama wachangiaji waliotangulia naendelea kumshangaa huyu Mr. samahani kama nitakukwaza lakini sidhani kama mume kweli mwenye mapenzi kwa mkewe anasikia kunalijamaa linamnyemelea wife yeye atapandisha mabega!! nahisi shem wetu anaupungufu fulani ndio maana ata XBf amepata mwanya wakukusumbua anajua kama akikaza buti atakupata,naamini huyu X uponae karibu kimtindo tofauti na unavyotueleza hapa au inawezekana hii story umetupatia nusu hainajakamirika kuna vitu umemiss kama si hivyo asingeweza kuwa jasiri nakutuma sms kwa mke wa mtu bila hofu nimtu ambae anafahamu udhaifu wa mume wako nandio maana hakupata shida kupata simuno yako.

Ushauri wangu jitoe kimasomaso mpigie uyu Xbf wako na umweleze kuwa uko mbioni kumchukulia hatua za kisheria endapo ataendelea kukutumia sms kwani hana nia njema kwako anachotaka nikukuvurugia ndoa yako kisha aingie mitini angekuwa mume angekuwowa mwanzo.
 
Sasa hebu tueleze, Ulimwabia sababu aliuliza kiini chako kubadilisha no. Ama hata hakuulizia kwanini unabadilisha no. yako?

Sijui lakini naona pana kitu hukisemi!

Nilimweleza na badilisha sababu ya huo usumbufu siutaki. Then akajibu Ok na kukaa kimya bila nyongeza yoyote. Ila tayari jamaa alishaipata tena NDO MAANA NIMEKUJA KUULIZA NIFANYE NINI SASA NIMECHOKAAAAAAAAAAAAAAAAA! EH!
 

Thanks alot, but this too Njembaz hazijuani kabisaaaaa hio naamini. Nadhani kuna mtu (one of my cousin husband) is the one doing this. Nimejaribu kuuliza akaniambia hajampa, nasiwezi kung´ang´na kwamba die yeye aliyempa no evidence with that. Well ningumu kidogo but will try my best from the mawazo niliyopata kwa wana JF. Asanteni sana kwa msaada wenu.
 
Loraine mie nataka kujua ni kwanini ulifunga ndoa bila kumwarifu kuwa mchezo sasa basi? Je mliahidiana nini wakati mkiwa ma-friend? Hawezi tu kupata guts kiasi hicho kama hukumpa ahadi au makubaliano fulani.
 
Lorain…huyo dawa yake ndogo..ukishidwa kubadili number/kumblock we mchunie tu, yaani unauchuna mpaka mwenyewe anajiona mpumbavu.. ukiona tu message kutoka kwake una delete, yaani wala hata usizisome…delete tu..halafu endelea na maisha yako.

Maadamu umeshamweleza mumeo umwambie pia na effort ulizofanya na unazofanya kukabiliana na hilo, ili hata siku message ikiingia simu ikiwa ikiwa mikononi mwake asikulaumu, hata kama akiendelea kupandisha mabega mwambie tu…
 
Loraine mie nataka kujua ni kwanini ulifunga ndoa bila kumwarifu kuwa mchezo sasa basi? Je mliahidiana nini wakati mkiwa ma-friend? Hawezi tu kupata guts kiasi hicho kama hukumpa ahadi au makubaliano fulani.

Ndugu mpendwa, naomba nieleweke vizuri tena. Huyu bwana toka nimeachana naye na mda wa miaka minne sasa. Natoka tumeachana hamna hata siku nilirudisha hisia zangu kwake tena. Na nilimtaamkia tena kwa herufi kubwa "MIMI NA WEWE IMEKWISHA", ila yeye hakuwa tayari kupokea maneno haya. Ndo akabakia kunipigia nakunitumia sms kila mara, nikibadilisha simu anahakikisha anaipata ile no. tuu.
 

Asante sana ndugu yangu, ushauri wako nimeupokea na nitaufanyia kazi. Ubarikiwe sana.
 
Nilimweleza na badilisha sababu ya huo usumbufu siutaki. Then akajibu Ok na kukaa kimya bila nyongeza yoyote. Ila tayari jamaa alishaipata tena NDO MAANA NIMEKUJA KUULIZA NIFANYE NINI SASA NIMECHOKAAAAAAAAAAAAAAAAA! EH!

Samahani dada, kama kuchoka kwako, nikutokana na maswali yetu.
Kama ni kotokana na swala lako basi pia usichoke ikiwa unaidhamini ndoa yako.

Ilinichukua kama two weeks hivi, ndo ikabidi nimwambie. Nilijaribu kwanza kufanya kama mlivyoniagiza kubadilisha no. na kumkanya vile vile.

Wajua ndo mtu kutoa ushauri, inabidi kujieka kwenye hali ya mwenzake. Sasa kama ulivyoandika, ilikuchukua kama wiki mbili kabla hujamwambia, hapo mbeleni ulijaribu kama ulivyo agizwa na wanaJF kama kubadili no.

Sasa najiuliza ningekuwa huyo mumeo, halafu mke wangu abadilishe no. yake singetaka kujua ni kwa nini? Na kama nisipouliza ni kwanini basi kuna kitu kitakachokuwa kumenifanya nisijishugulishe na anachofanya mke wangu. Kama hii ni kweli basi shida zako si za huyo EX wako peke yake, bali kuna mengine mumeo hakwambii hadi imefika kuwa hana interest!

Either pengine alishuku kwa kuwa aliona kama asingekuuliza basi hungemwambia, na hapo pengine yeye anakuchunguza kivyake kuona kama ulivyomwambia ni kweli [Maoni tu].

Ikiwa ni mimi sikukuelewa hapo juu na ulimjulisha kabla ya kubadilisha no. na yeye kasema tu OK, basi kama walivyo sema wengine humu, kunacho hakuambii mumeo! Itakubidi kukaa nae muongee kwani inaonekana unamengi yakubeba zaidi ya huyo Ex. wako.
 
Asante sana ndugu yangu, ushauri wako nimeupokea na nitaufanyia kazi. Ubarikiwe sana.

Ukiufanyia kazi ushauri wa ndugu yetu pia usisahau UKIMYA wa mwenza wako. Unapo-present kitu kwa mtu wa karibu (mfano mume), then receiver (mfano mume) akakaa kimya HAPA kuna maana nyingi sana.
 
Nakubaliana nawe Mr. Bauer.

Mume wa huyo dada yetu ni mtu makini na mwenye taadhari ya hali ya juu.Kabla ya kucomment anasoma alama za nyakati.Dada yetu muhusishe zaidi katika kila utakalofanya mumeo kuhusu huyo Ex wako.

Lorain:
Ushauri wangu ni wewe kubadili namba yako ya simu baada ya kumweleza huyo Ex wako kuwa huhitaji mawasiliano na/au mahusiano yeyote naye ukiwa UNAMAANISHA.

Lastly,jitazame upya uhusiano wako na huyo Ex wako.Sote tunaheshimu ndoa na hata wale wanaotongoza wake au waume za watu,wanafanya hivyo KWA KUWEPO MAZINGIRA yanayowasukuma kufanya hivyo.ANGALIA MAZINGIRA YAKO.
 
ni wanaume wachache wanaopenda kufahamu background za wenzi wao na huwa zinatuudhi.Naamini kukaa kwake kimya ameudhika.Kaa nae upate msimamo wake muone kama mwaweza kushirikiana kulimaliza tatizo.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…