habar wakuu, ushauri wenu tafadhali
nina ndugu yangu wa damu kabisa katika familia yetu tupo watatu wakike kaolewa, wapili ndio yeye nawamwisho mimi, nakwasasa nina miaka mitano hatuongei kwakuwa tuligombana kwasababu yatabia zake zakishenzi, pia nyumbani inatambulika mimi simpendi na nayeye hanipendi
yani yeye tangu mzee yupo hai alikuwa mtu wa hovyo sana mzee alikuwa anajitahidi sana kumpa mitaji yabiashara yani yeye wiki tu ameshauwa kila kitu, kwamwaka anaweza akapewa mtaji zaidi ya mara 20 nakuuwa tu.
lakini sasa tangu mwaka jana mzee afariki mama ndio amekuwa amechukua jukumu ilo anampa mtaji lakini bado vile vile, anakaa nyumbani, kwasasa hataki kujishughulisha na shughuli yoyote, anakaa tu nyumbani mda wote anaangalia tv akiomba hela kwamama anataka lazima apewe, mama akisema sina matusi yanaanza nispokuwepo nyumbani hapo hadi mimi siponi, anaanza_ unamuendekeza sana mwanao uyu, mimi sithaminiki humu ndani nmeomba sh elfu 10,000 tu nanyimwa lakini unamuendekeza sana mwanao, ukija kufa atapata shida sana na simpendi.
maneno mengi mpaka mama ata kama hana itabidi atoe tu hiyo hiyo, anasababisha matatizo anazulumu watu anafanya vituko nyumbani, kwasababu mama mpole analipa tu looooh ! nmekelwa na tabia zake , kwasasa anamiaka 32 namimi ni miaka 20 tu na mimi niwamwisho kwetu.
kwasasa naona chuki imezidi sana, ananichukia hadi mimi najishtukia najua anaweza kufanya lolote kwangu ili anione napata shida ata nkikaa home nakuwa makini sana na akiniona mimi anajua sipendi upumbavu anapoa sana lakini nispokuwepo anamtesa sana anamtesa sana mama mpaka mama anafika hatua anasema uyu mtoto analaana
ushauli wenu wadau uyu mtoto wakiume anamiaka 32 ataki kufanya kazi, akipewa mtaji anahonga, analewa kipumbavu nakwasasa nimlevi sana akipewa hela yeye kulewa na anapenda sana wanawake alafu JOGOO HAWIKI, kazi hataki. afanyweje uyu ? anataka nnachopewa mimi nayeye apewe imefikia hatua mama anamuangalia sana yeye kuliko mimi na bado hapendi uwepo wangu. mimi nibado mwanafunzi
ushauri wakuu
asanten.