Ushauri wangu kwa Waziri Paul Makonda ili kuifanya Tanzania ing'are kwenye vyombo vya kimataifa

Ushauri wangu kwa Waziri Paul Makonda ili kuifanya Tanzania ing'are kwenye vyombo vya kimataifa

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
457
Reaction score
773
Waziri wa Habari, Paulo Makonda ameonesha nia nzuri ya kutaka Tanzania ifahamike kimataifa. Hata hivyo utaratibu aliouzungumza ili Tanzania iandikwe aljazeera, CNN na maeneo mengine ina walakini, na hapa nitoe mawazo yangu kwenye kutimiza hilo.

Suala la sisi kuandikwa kimataifa halifanyiki sana kwa kuwa tunawatu wachache waliokwenye taasisi za kimataifa. Je tunafanyaje kwanza kuhakikisha watu hawa wanaenda kimataifa na kuwa connected ili nasi tupate kuwatumia katika kuleta picha nzuri ya nchi yetu.

Nitoe mfano wa Kenya ambayo ina watu wengi kimataifa na mnaona jinsi Kenya inafanya vizuri hadi watu wengi wanajua vitu vingi vipo kwao. Larry Madowo, sikosoi kazi yake, anafanya vizuri lakini mliona akiripoti matatizo ya Kenya? Suala ni kwamba ukiwa na watu kama Larry ni rahisi kupata story nzuri za nchi yako kwenye maeneo hayo ya kimataifa. Larry mbali na kufanya kazi sana Kenya 2019–2020 alipata Knight-Bagehot Fellows huko Columbia University. Hapo alipata kuwa correspondent wa media outlets kubwa.

Serikali za Pakistan na South Korea kwa ushahidi nilio nao wanashirikiana na Marekani ili watu wao waende kupata exposure huko na zinawafanya waende mbali. Serikali ya Tanzania haitoi hela ili watu waende mbali. Mfano Tanzania kulikuwa na Fulbright program ambayo inafadhiliwa na Marekani. Hii program huchukua mtu mmoja hadi wawili kila mwaka kwenda kujifunza vitu tofauti tofauti Marekani. Lakini nchi nyingine utakuta zinatoa watu hadi 10 kwa kila mwaka kwa kuwa nchi zao zinatoa hela kwa hizo program ili watu wao wawe wengi.

Maana yangu ni kuwa, badala ya kulazimisha watu wabaki Tanzania, tukomae na suala la watu kupata hizi exchange programs ili kuongeza representation kimataifa. Mfano, Badala ya Samia scholarship kupeleka wanafunzi Arusha, tuwapeleke vyuo vya Marekani au Ulaya ambako watakuwa more exposed.

Kuna MicroMasters program inatolewa na wataalamu wa kubwa wa data huko MIT. Kila course inalipiwa $250, na inabidi usome course 4 ilikupata MicroMasters. Ukiangalia pale Brazil inatoa hela kwa watu wake ili wasome bure badala ya kulipa hela hiyo. Lakini kwa Africa, lazima upambane kupata hela ya kusoma, hebu fikiria ulipe $1250 ili kupata micromasters, ambayo ni milioni zaidi ya mbili kwa fedha za Tz. Lakini ile masters inawapeleka watu sehemu kubwa sana.
1768373361902.png


Mfano wa fellowship kwa ajili ya kusoma
1768373361917.png


So, nitoe wito kwa Makonda kwamba kama anafikiria kuleta picha nzuri ya Tanzania nje ya Tanzania. Asiwaze kwamba unaweza kupeleka Press release kwa editors ili waandike habari yako. Ila tukiwa na watu wengi kimataifa watasaidia katika kufanya hizo press releases ziwe stories strategically.

Nawasilisha.
 
Makonda alisema atamleta Schwazinneger, akasema atapeleka wanafunzi 1,000 India, akaendesha hadi na interview ya wanafunzi. Hadi leo ni usanii mtupu. Ogopa tapeli.
 
Makonda alichofanikiwa ni ile ishu ya kuwashtaki wazazi waliotelekeza au hawatoi matunzo kwa watoto wao.

Nina jamaa yangu mpaka leo bado anapeleka hela ustawi wa jamii.

Lakini kuliko kuhangaika na bbc sijui cnn au aljazeera, Bora wangekomaa kwenye social network.

Hawa bbc, cnn na wenzao wooote saiv wana akaunti social network kwa maana mainstream media zinaenda kupotea muda si mrefu.

Ilibidi akomae na watu kama kina ishowspeed na wengine wa kariba kama hizo, ikiwezekana tutengeneze watu wetu wenye ushawishi kwenye social network sio mainstream media.

Tazama kenya walivyofaidika na ujio wa huyo ishowspeed, lazima atakua kaitangaza kenya kimataifa
 
Makonda alichofanikiwa ni ile ishu ya kuwashtaki wazazi waliotelekeza au hawatoi matunzo kwa watoto wao.

Nina jamaa yangu mpaka leo bado anapeleka hela ustawi wa jamii.

Lakini kuliko kuhangaika na bbc sijui cnn au aljazeera, Bora wangekomaa kwenye social network.

Hawa bbc, cnn na wenzao wooote saiv wana akaunti social network kwa maana mainstream media zinaenda kupotea muda si mrefu.

Ilibidi akomae na watu kama kina ishowspeed na wengine wa kariba kama hizo, ikiwezekana tutengeneze watu wetu wenye ushawishi kwenye social network sio mainstream media.

Tazama kenya walivyofaidika na ujio wa huyo ishowspeed, lazima atakua kaitangaza kenya kimataifa
Kenya wanabebwa na mambo mengi ikiwemo na lugha
 
Waziri wa Habari, Paulo Makonda ameonesha nia nzuri ya kutaka Tanzania ifahamike kimataifa. Hata hivyo utaratibu aliouzungumza ili Tanzania iandikwe aljazeera, CNN na maeneo mengine ina walakini, na hapa nitoe mawazo yangu kwenye kutimiza hilo.

Suala la sisi kuandikwa kimataifa halifanyiki sana kwa kuwa tunawatu wachache waliokwenye taasisi za kimataifa. Je tunafanyaje kwanza kuhakikisha watu hawa wanaenda kimataifa na kuwa connected ili nasi tupate kuwatumia katika kuleta picha nzuri ya nchi yetu.

Nitoe mfano wa Kenya ambayo ina watu wengi kimataifa na mnaona jinsi Kenya inafanya vizuri hadi watu wengi wanajua vitu vingi vipo kwao. Larry Madowo, sikosoi kazi yake, anafanya vizuri lakini mliona akiripoti matatizo ya Kenya? Suala ni kwamba ukiwa na watu kama Larry ni rahisi kupata story nzuri za nchi yako kwenye maeneo hayo ya kimataifa. Larry mbali na kufanya kazi sana Kenya 2019–2020 alipata Knight-Bagehot Fellows huko Columbia University. Hapo alipata kuwa correspondent wa media outlets kubwa.

Serikali za Pakistan na South Korea kwa ushahidi nilio nao wanashirikiana na Marekani ili watu wao waende kupata exposure huko na zinawafanya waende mbali. Serikali ya Tanzania haitoi hela ili watu waende mbali. Mfano Tanzania kulikuwa na Fulbright program ambayo inafadhiliwa na Marekani. Hii program huchukua mtu mmoja hadi wawili kila mwaka kwenda kujifunza vitu tofauti tofauti Marekani. Lakini nchi nyingine utakuta zinatoa watu hadi 10 kwa kila mwaka kwa kuwa nchi zao zinatoa hela kwa hizo program ili watu wao wawe wengi.

Maana yangu ni kuwa, badala ya kulazimisha watu wabaki Tanzania, tukomae na suala la watu kupata hizi exchange programs ili kuongeza representation kimataifa. Mfano, Badala ya Samia scholarship kupeleka wanafunzi Arusha, tuwapeleke vyuo vya Marekani au Ulaya ambako watakuwa more exposed.

Kuna MicroMasters program inatolewa na wataalamu wa kubwa wa data huko MIT. Kila course inalipiwa $250, na inabidi usome course 4 ilikupata MicroMasters. Ukiangalia pale Brazil inatoa hela kwa watu wake ili wasome bure badala ya kulipa hela hiyo. Lakini kwa Africa, lazima upambane kupata hela ya kusoma, hebu fikiria ulipe $1250 ili kupata micromasters, ambayo ni milioni zaidi ya mbili kwa fedha za Tz. Lakini ile masters inawapeleka watu sehemu kubwa sana.
View attachment 3529671

Mfano wa fellowship kwa ajili ya kusoma
View attachment 3529672

So, nitoe wito kwa Makonda kwamba kama anafikiria kuleta picha nzuri ya Tanzania nje ya Tanzania. Asiwaze kwamba unaweza kupeleka Press release kwa editors ili waandike habari yako. Ila tukiwa na watu wengi kimataifa watasaidia katika kufanya hizo press releases ziwe stories strategically.

Nawasilisha.
Naunga mkono hoja
P
 
Hana ubavu wa kuing'anisha wakati washaipakaza mavi - damu za watu zaidi ya 10,000 haziwezi enda patupu...ni suala la muda tu.
 
Mnataka CNN watangaze Rais ameenda kuzindua bweni? Mnataka BBC watangaze serikali ya Tanzania imewanunulia laptop na camera waandishi wa habari wa kujitegemea? Hizo habari zitaijenga au kuibomoa Tanzania?
 
Naunga mkono hoja
P

Mwandishi nguli badili mwelekeo, habari kwa lugha ya kiSwahili zimefurika ktk majukwaa yote iwe za online n.k mbaya zaidi hakuna wasomaji au watazamaji wa kigeni kimataifa wa habari zenu kutokana na kutumia 'kiLugha' cha kiSwahili

Ni wakati wa wewe kuongoza kwa kwenda kutumia lugha ya kigeni kama kiEnglish.

YouTuber wa kiTanzania wanaotumia kiEnglish wanasomwa sana Kenya, Uganda, Zambia, Kusini mwa Afrika, Afrika Magharibi na ulimwenguni kote wanakutumia lugha ya kiEnglish
 
Hivi ahadi ya polisi wa Arusha wawe kama wa Ulaya ikawaje, wapewe na baiskeli za umeme na kila kituo kifungwe CCTV camera ilishia wapi
 
Mwandishi nguli badili mwelekeo, habari kwa lugha ya kiSwahili zimefurika ktk majukwaa yote iweze online n.k mbaya zaidi hakuna wasomaji au watazamaji wa kigeni kimataifa wa habari zenu kutokana na kutumia 'kiLugha' cha kiSwahili

Ni wakati wa wewe kuongoza kwa kwenda kutumia lugha ya kigeni kama kiEnglish.

YouTuber wa kiTanzania wanaotumia kiEnglish wanasomwa sana Kenya, Uganda, Zambia, Kusini mwa Afrika, Afrika Magharibi wanakutumia kiEnglish
Naunga mkono hoja
P
 
Waziri wa Habari, Paulo Makonda ameonesha nia nzuri ya kutaka Tanzania ifahamike kimataifa. Hata hivyo utaratibu aliouzungumza ili Tanzania iandikwe aljazeera, CNN na maeneo mengine ina walakini, na hapa nitoe mawazo yangu kwenye kutimiza hilo.

Fupa gumu lililomshinda Prof. Palamagamba Kabudi leo anatupiwa Makonda !

10 December 2025
Al Jazeera TV

Prof. Kabudi leo kapatikana, ka- panic sana kukutana na media huru ya kimataifa leo ya Doha, Qatar.

View: https://m.youtube.com/watch?v=5y4rd7_adv4
Intaneti kwa Dorothy Semu kiongozi wa ACT Wazalendo, mamlaka za TCRA walijaribu block lakini ameweza kuongea kwa utulivu kuliko Prof. Palamagamba Kabudi kucheua vifungu gandamizi vya sheria mbovu kutetea udhalimu na mauaji. Kabudi kakutana na mtangazaji wa Al Jazeera anayejua kiSwahili pale Prof. Kabudi alipojaribu kupindisha tamko kuwa kuna jaribio la kuangusha nchi lilotolewa na serikali haramu ya CCM kuwa maandamano yanataka kumpindua serikali


TOKA MAKTABA :

 
Niliwaza kwa aina ya UKONDALISM sijui kama mwana FA atawezana na UKONDALIST

Kuna umakondalism mpaka mama SAMIA suluhu Hassan ilibidi ASEME wakivutana wizarani basi wataondoshwa woteeeeeee.

Pole mwana FA Sijui kama unaweza kuishi na huyo makonda hapo wizarani maana namwonaga ujuaji ni mwingi showoff ni nyingi kiki ni nyingi kwa huyo Kondalism
 
Back
Top Bottom