Ushauri wangu kwa wapambe wa Lissu

Ushauri wangu kwa wapambe wa Lissu

Mbogo nyeusi

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
230
Reaction score
541
Ni kweli mapokezi ya Tundu Lissu ya tarehe 27/7 tayari yameharibika na Kuna zuio la mikusanyiko kwa barua inayo zunguka mitandaoni.

Nashauri wapambe wa Lissu waandae utaratibu utakao mfanya Lissu ashiriki kwenye hatua zote za kuaga na kumzika rais wetu mstaafu kuanzia Dar hadi mtwara,waandae waandishi wa habari wafanye coverage kwa kila hatua atakayo fanya.

Najua kwa sasa ni vigumu kwa chama kuandaa utaratibu wa kumbrand kwa vile wataonekana wanambeba kwani ni miongoni wa watia nia kugombea uraisi,hivyo wapambe wake wachukue jukumu la kuandaa utaratibu unao faa kutengeneza attention na popularity kwa mh Lissu.
 
Tuko na Msiba Wa Mzee Wetu Kipenzi Benjamin W. Mkapa.

Poleni kina Blasia Mkapa na wanafemili wengine,Mungu awape utulivu kipindi hichi kigumu.

AIRPORT SI SEHEMU YA KUFANYA MAANDAMANO NA VURUGU.
 
Kwani tangu lini hapa Tanzania kumekuwa na kuomba kibali cha kufanya Mapokezi???

Mapokezi ya Hussein Mwinyi juzi Zanzibar yaliombewa kibali???
Maisha halisia nje ya maisha ya mitandaoni hayapo hivi usemavyo.
Matukio au watu unaofananisha ni kama mtoto wa miaka 16 anakoromea ndugu zake anasema namimi narudi saa 6 usiku, mbona baba kila siku anarudi muda huo?.

Huyo mwingine analindwa na dola(chama tawala) , na mwenzie ni mtoto wa nje ya ndoa (chama pinzani + bado hajapitishwa na chama chake kuwa mgombea).

NB: Mimi sitetei wala kuunga au kupinga mkono kuandamana wala kuzuia watu kuandamana, I'm just stating the obvious ..
 
Hili LA mapokezi polis na chadema wakae wajadiliane, yote yetu, msiba Ni wetu.Pia kumpokea lissu kunatuhusu....hatutaki jeshi LA polis linalottumia nguvu kwa jambo sio LA kutumia nguvu
 
Tuko na Maombolezo ya siku 7.....

Airport si sehemu ya maandamano na vurugu....
 
Ha ha ha ha zile fulana nyeupe Walizokuwa wanashinda nazo,kuogelea nazo,kulala nazo toka Ile sabasaba?!!!

CDM na tamthilia zisizokwisha.....😂😂😂😂
Nina fulana yako , karibu kwenye mapokezi ya Lissu
 
Ndiyo..na ninyi ombeni kibali..
Tuonyesheni icho kibali chenu.

Tatizo la CCM mnafikiri mkifanya hivi ndo mnamkomoa Lissu kumbe ndo mnavozidi kujenga mapenzi ya watanzania wote kwa ya Lissu maana wanaona uonevu wenu wa wazi mnaoufanya kweupe kabisa.

Nawaambia tena mwisho wa haya yote ni October 2020 na pale ndo mtakapoona hasira za watanzania zikoje
 
Tuonyesheni icho kibali chenu.

Tatizo la CCM mnafikiri mkifanya hivi ndo mnamkomoa Lissu kumbe ndo mnavozidi kujenga mapenzi ya watanzania wote kwa ya Lissu maana wanaona uonevu wenu wa wazi mnaoufanya kweupe kabisa.

Nawaambia tena mwisho wa haya yote ni October 2020 na pale ndo mtakapoona hasira za watanzania zikoje
Watanzania wa wapi hao wenye mapenzi na Lissu?! Yaani hii Oktoba 2020 watanzania wataontesha hasira kwa JPM...nadhani haupo Tanzania wewe...
 
Kwani tangu lini hapa Tanzania kumekuwa na kuomba kibali cha kufanya Mapokezi?

Mapokezi ya Hussein Mwinyi juzi Zanzibar yaliombewa kibali?
Airport iko bize kupokea wageni wa kuja kumuaga mkapa, ulinzi utakua tight. Wapange siku nyingine tu.
 
Awawezi kuelewa,hawanaga mipango ni wakurupukaji tu.hawanaga plan B.
 
Ni kweli mapokezi ya Tundu Lissu ya tarehe 27/7 tayari yameharibika na Kuna zuio la mikusanyiko kwa barua inayo zunguka mitandaoni.

Nashauri wapambe wa Lissu waandae utaratibu utakao mfanya Lissu ashiriki kwenye hatua zote za kuaga na kumzika rais wetu mstaafu kuanzia Dar hadi mtwara,waandae waandishi wa habari wafanye coverage kwa kila hatua atakayo fanya.

Najua kwa sasa ni vigumu kwa chama kuandaa utaratibu wa kumbrand kwa vile wataonekana wanambeba kwani ni miongoni wa watia nia kugombea uraisi,hivyo wapambe wake wachukue jukumu la kuandaa utaratibu unao faa kutengeneza attention na popularity kwa mh Lissu.
Huyo muuaji zikeni wenyewe hatuna mda naye
 
Watanzania wa wapi hao wenye mapenzi na Lissu?! Yaani hii Oktoba 2020 watanzania wataontesha hasira kwa JPM...nadhani haupo Tanzania wewe...
...huyo atakuwa anachat toka KUZIMU😂😂😂
 
Back
Top Bottom