Ushauri wangu kwa wanaotarajia kufunga ndoa/kufanya send off

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Ukitaka sherehe ujipange sawa sawa.
Hakikisha una pesa ya kutosha kuchukua gharama za sherehe pale Mambo yanapoenda tofauti.
Vinginevyo utajikuta unawachukia watu kisa hawajakuchangia wakati sio lazima. Kuna watu wananuniana humu mijini kisa mwingine hakuchanga mchango wa sherehe.!!

Ndoa/send-off sio dharula kwamba isipofanyika kuna mtu atakufa. Tujipange ili tusiingie kwenye ndoa na mikopo kisa siku moja. Sio kila uliyesoma naye/unayefanya naye kazi/ uliyenaye group moja umhesabie Kama ni pesa yako ya sherehe.

Watu Wana Mambo mbali mbali humu duniani. Nakumbuka wakati naoa niliamua kufungia ndoa nyumbani waliko wazazi. Hii ilipunguza gharama za kuwalaza wazazi na ndugu hotelini ugenini.!! Pia nilihakikisha mfuko uko sawa ndio nikaanzisha mchakato. Kamati ilifanya kazi yake lakini sikuwa na shaka na hofu ya kuanza kukopa ili sherehe ifanyike. Na huko kijijini Mambo ni rahisi tu. Bajeti ndogo sana inakutoa na tukio linafanikiwa.

Tujipange jamani ukiona bajeti ngumu jua watu waliko wanalia na ukata wa pesa.
 
Tumetoka kwenye vitu vya muhimu tanaanza fanya showoff tuu siku hizi.

Mie nadhani cha msingi ni ndoa na sio harusi hivyo mkazo ungekuwa je hawa wanandoa watarajiwa ni mabikra? Na sio kuchangishana
 
Tumetoka kwenye vitu vya muhimu tanaanza fanya showoff tuu siku hizi.

Mie nadhani cha msingi ni ndoa na sio harusi hivyo mkazo ungekuwa je hawa wanandoa watarajiwa ni mabikra? Na sio kuchangishana
Yaani Kuna wengine unakuta Wana watoto 3.
Aafu wanakuja kutuchangisha ili wafanye sherehe.
Huu ni ujinga kwa kweli.
Watoto mpaka 3 hamjajipanga namna Bora ya kubariki ndoa yenu?
 
Kuna mmoja alinipa kadi ya kuniomba mchango miezi 2 iliyopita.
Kesho yake nikajikuta nimeingizwa kwenye group la mchango na ahadi ashaandika.
Yaani yeye ndio amenikadiria kiwango Cha kutoa.!!

Yaani ni ile akikuona mtu anawaza kuwa hii ni 150000 nitaipata.
Anachowaza yeye ni sherehe yake tu.
 
Mimi nikipata mume... Atakae kubali tufunge ndo Ile ya mkeka.. ntafurahiaa Sana... Maaan Ni shekh na Kaka ZANGU..na mume...na ndungu baaasi...

Mimi SICHANGIAGI HARUSI....
 
Kuna mmoja alinipa kadi ya kuniomba mchango miezi 2 iliyopita.
Kesho yake nikajikuta nimeingizwa kwenye group la mchango na ahadi ashaandika.
Yaani yeye ndio amenikadiria kiwango Cha kutoa.!!

Yaani ni ile akikuona mtu anawaza kuwa hii ni 150000 nitaipata.
Anachowaza yeye ni sherehe yake tu.
😂😂😂😂Anakupangia kiasi Cha kutoa anaijua akiba yako?
 
Anakupangia kiasi Cha kutoa anaijua akiba yako?
Nishawai kuwekwa kwenye group la mchango wa harusi... Kama Rafiki...wa huyo bwana harusi wakati hatukuwai Hata piga story...

Ofisini kwetu...bank mtu anakuja na withdrawal slip anakupa ujaze akatoe kwenye account yako

Yaani Kama lazima
 
Nishawai kuwekwa kwenye group la mchango wa harusi... Kama Rafiki...wa huyo bwana harusi wakati hatukuwai Hata piga story...

Ofisini kwetu...bank mtu anakuja na withdrawal slip anakupa ujaze akatoe kwenye account yako

Yaani Kama lazima
Kuna mambo tunayaendekeza ni ujinga.
Watu wanataka kufanya show off kwa pesa za watu.
 
Mimi nikipata mume... Atakae kubali tufunge ndo Ile ya mkeka.. ntafurahiaa Sana... Maaan Ni shekh na Kaka ZANGU..na mume...na ndungu baaasi...

Mimi SICHANGIAGI HARUSI....
ayaaaaaa..umetiririka vizuriiii ila hapo suala la imani ndiyo,nshakukosa tena
 
Yaani Kuna wengine unakuta Wana watoto 3.
Aafu wanakuja kutuchangisha ili wafanye sherehe.
Huu ni ujinga kwa kweli.
Watoto mpaka 3 hamjajipanga namna Bora ya kubariki ndoa yenu?

Hakuna kitu kama kubariki ndoa, huo ni utapeli wa mchana kweupeeee.
 
Mimi nikipata mume... Atakae kubali tufunge ndo Ile ya mkeka.. ntafurahiaa Sana... Maaan Ni shekh na Kaka ZANGU..na mume...na ndungu baaasi...

Mimi SICHANGIAGI HARUSI....

Niko hapa, nikupe ndoa kwa nderemo na vifijo vyote... bila kuchangisha watu.
 
mimi sichangi kabisa..hata ndugu nishawaambia kabisa.....kama familia tuliozaliwa pamoja...tumekubaliana kati yetu anaeoza au kuooza....10m mezani kwanza......huna tunafanya kimya kimya....hiii ya kusema nilimchangia ....usiweke akilini.....ndoa ni kanisani......ita wa karibu mno.....maliza mkasuguane kihalali....
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom