jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,990
- 22,523
Wanajamvi,
Kwanza niseme kuwa niliitizama ile interview ya TL kule HARDtalk!
Nimeona maoni ya tofauti, maoni ambayo pia yamegawanyika kutokana na msimamo ama misimamo ya watoa maoni. Lakini jambo moja wengi wasilolifahamu, ni kwamba siyo watizamaji wote watakaotizama suala lile kama vile ni siasa tu.
Watizamaji wengi, haswa wale ambao walitizama kwa nia ya kupashwa habari, audience ambayo haitizami kwa jicho la ki unazi, kinachobakia kwenye fikra zao, ni ule ukweli kwamba huyo aliyeko kwenye screen, ni mtu aliyepigwa risasi 16 Lakini akapona! Hilo ndilo lilobaki kwenye fikra zao! Na sanasana, sidhani kama walisikia chochote ambacho kwenye akili yao, kitaonekana kuhalalisha jaribio lile la mauwaji. Kwahiyo kina Pole Pole wasidhani kuwa hadhira ile iliyolengwa, Inafikiria kwa namna wanavyofikiria wao!
Pia kwa upande mwingine, Lissu asingeulizwa maswali yale, wangeishia tu kusema “ni mipango ya mabeberu”, na ikija kutokea interview ile ikachukuliwa tofauti na hadhira ile iliyokusudiwa, kinyume na walivyofikiri wao kina Polepole, watakuja tu kudai kuwa ni mipango ya mabeberu. It is just a matter of time. Maana maswali hayo hayo aliyoulizwa Lissu, serikali ama Maghufuli akiulizwa anaweza kujibu? Sidhani!
Pia kuna watu wanaendelea kupotosha. Kuhusiana na alivyojibu maswali yale. Aliyajibu vyema tu, sema tu ni aina ya uulizaji maswali kwenye kile kipindi, ambapo anakuwa kama yuko “all over the map”, yani hakuna mpangilio!
Kwa maoni yangu, hakufanya vibaya. Lakini pia, angeweza kufanya vizuri zaidi. Nilichokiona mimi, pengine ni ukosefu wa maandalizi ya kutosha kabla ya kwenda kwenye hiyo interview.
I believe he could’ve prepared better! Kuna kitu kinaitwa “mock interview ”, ambapo yeye alitakiwa awe ameshatizama sana kile kipindi, halafu angetafuta mtu ambaye ange act kama yule host wa HARDtalk hivyohivyo! Na aulizwe “possible questions”
Kwa marekani Mfano, kabla ya debate ama mdahalo kwenye kugombea, Mfano urais,wale wagombea wanatafuta watu ambao wanauwezo wa kuongea hivyo hivyo kama mtangazaji na pia mpinzani wake. Unakuta wamejiandaa kwelikweli!
Pia hakikisha una points zako ambazo utaziwakilisha no matter what! Kazi yako ni kuchagua kuwa unaziwakilisha kwa kupitia maswali gani ili usiwe nje ya topic unapojibu. Lakini majibu mengi tu yanaweza kufit kwenye aina mbali mbali za maswali!
Mfano swali lolote lenye kuhusiana na demokrasia, ni lazima jibu lake linaweza kuwa lolote lenye kuelezea hali hiyo, na siyo lazima kujibu swali specifically!
Swali alilloulizwa kuhusiana na mashoga, lilikuwa la kimtego, lakini alijibu vyema kabisa!
Niwape Mfano mmoja tu, na wala siyo kwamba nafananisha directly! Mfano ni kwasababu ya audience ambayo nina uzoefu nayo. Mfano mwanamziki maarufu wa Hip hop, anayeitwa 50 cent, yeye umaarufu wake ulipanda maradufu, kwasababu aliweza kusavaivu shambulizi la risasi tisa mwilini! Hiyo story tu, kwa wengi ilimpandisha chati vibaya mno kuliko hata bifu lake na Ja Rule ambapo ndiyo ilikuwa kama kigezo chake cha kumtoa. Lakini kila utakayemuuliza, atakumbuka hilo la kusavaivu shambulizi zaidi kuliko bifu lake na Ja rule! Risasi tisa mwilini na hakufa! Hilo lilibaki kwenye akili na fikra zao!
Audience ile haijali kuhusu eti alipigwa risasi zote hizo kwasababu sijui alipinga ununuzi wa ndege, au sijui eti aliwashtua wadeni wetu kuhusu ndege wakaikatamata! Sanasana haya ukiwasisitizia, wanaweza kuona kuwa “he was just a honest guy”
Hayo mengine sijui aliyoyafanya Maghufuli “ya maendeleo” wala siyo hoja kwenye issue hiyo ya kushambuliwa kwake! Next time host wa kipindi akileta hizo, unampa facts tu na kustick kwenye nia haswa ya mission yako!
Sitaki kuweka bandiko refu.Ila ushauri unaendelea...
Kwanza niseme kuwa niliitizama ile interview ya TL kule HARDtalk!
Nimeona maoni ya tofauti, maoni ambayo pia yamegawanyika kutokana na msimamo ama misimamo ya watoa maoni. Lakini jambo moja wengi wasilolifahamu, ni kwamba siyo watizamaji wote watakaotizama suala lile kama vile ni siasa tu.
Watizamaji wengi, haswa wale ambao walitizama kwa nia ya kupashwa habari, audience ambayo haitizami kwa jicho la ki unazi, kinachobakia kwenye fikra zao, ni ule ukweli kwamba huyo aliyeko kwenye screen, ni mtu aliyepigwa risasi 16 Lakini akapona! Hilo ndilo lilobaki kwenye fikra zao! Na sanasana, sidhani kama walisikia chochote ambacho kwenye akili yao, kitaonekana kuhalalisha jaribio lile la mauwaji. Kwahiyo kina Pole Pole wasidhani kuwa hadhira ile iliyolengwa, Inafikiria kwa namna wanavyofikiria wao!
Pia kwa upande mwingine, Lissu asingeulizwa maswali yale, wangeishia tu kusema “ni mipango ya mabeberu”, na ikija kutokea interview ile ikachukuliwa tofauti na hadhira ile iliyokusudiwa, kinyume na walivyofikiri wao kina Polepole, watakuja tu kudai kuwa ni mipango ya mabeberu. It is just a matter of time. Maana maswali hayo hayo aliyoulizwa Lissu, serikali ama Maghufuli akiulizwa anaweza kujibu? Sidhani!
Pia kuna watu wanaendelea kupotosha. Kuhusiana na alivyojibu maswali yale. Aliyajibu vyema tu, sema tu ni aina ya uulizaji maswali kwenye kile kipindi, ambapo anakuwa kama yuko “all over the map”, yani hakuna mpangilio!
Kwa maoni yangu, hakufanya vibaya. Lakini pia, angeweza kufanya vizuri zaidi. Nilichokiona mimi, pengine ni ukosefu wa maandalizi ya kutosha kabla ya kwenda kwenye hiyo interview.
I believe he could’ve prepared better! Kuna kitu kinaitwa “mock interview ”, ambapo yeye alitakiwa awe ameshatizama sana kile kipindi, halafu angetafuta mtu ambaye ange act kama yule host wa HARDtalk hivyohivyo! Na aulizwe “possible questions”
Kwa marekani Mfano, kabla ya debate ama mdahalo kwenye kugombea, Mfano urais,wale wagombea wanatafuta watu ambao wanauwezo wa kuongea hivyo hivyo kama mtangazaji na pia mpinzani wake. Unakuta wamejiandaa kwelikweli!
Pia hakikisha una points zako ambazo utaziwakilisha no matter what! Kazi yako ni kuchagua kuwa unaziwakilisha kwa kupitia maswali gani ili usiwe nje ya topic unapojibu. Lakini majibu mengi tu yanaweza kufit kwenye aina mbali mbali za maswali!
Mfano swali lolote lenye kuhusiana na demokrasia, ni lazima jibu lake linaweza kuwa lolote lenye kuelezea hali hiyo, na siyo lazima kujibu swali specifically!
Swali alilloulizwa kuhusiana na mashoga, lilikuwa la kimtego, lakini alijibu vyema kabisa!
Niwape Mfano mmoja tu, na wala siyo kwamba nafananisha directly! Mfano ni kwasababu ya audience ambayo nina uzoefu nayo. Mfano mwanamziki maarufu wa Hip hop, anayeitwa 50 cent, yeye umaarufu wake ulipanda maradufu, kwasababu aliweza kusavaivu shambulizi la risasi tisa mwilini! Hiyo story tu, kwa wengi ilimpandisha chati vibaya mno kuliko hata bifu lake na Ja Rule ambapo ndiyo ilikuwa kama kigezo chake cha kumtoa. Lakini kila utakayemuuliza, atakumbuka hilo la kusavaivu shambulizi zaidi kuliko bifu lake na Ja rule! Risasi tisa mwilini na hakufa! Hilo lilibaki kwenye akili na fikra zao!
Audience ile haijali kuhusu eti alipigwa risasi zote hizo kwasababu sijui alipinga ununuzi wa ndege, au sijui eti aliwashtua wadeni wetu kuhusu ndege wakaikatamata! Sanasana haya ukiwasisitizia, wanaweza kuona kuwa “he was just a honest guy”
Hayo mengine sijui aliyoyafanya Maghufuli “ya maendeleo” wala siyo hoja kwenye issue hiyo ya kushambuliwa kwake! Next time host wa kipindi akileta hizo, unampa facts tu na kustick kwenye nia haswa ya mission yako!
Sitaki kuweka bandiko refu.Ila ushauri unaendelea...