Ushauri wangu kwa SUMATRA kuhusu magari ya Sauli

Wakuu habari,

Ningependa kuishauri SUMATRA wawaite na kuwashauri wamiliki/madereva wa mabasi ya SAULI kuwa kusifiwa barabarani kwa ubingwa wao wa kukimbia speed kubwa na kuovertake bila mpangilio siku moja kutagharimu maisha ya abiria wasio na hatia.

Ushauri wangu ni huo kwenu SUMATRA msije sema hamkuambiwa.
Hao Sauli lao speed, kuna hii kampuni inaitwa Maning Nice inafanya biashara sehemu nyingi nchini. Nataka nizungumzie haya mabasi yake yanayotoka Tunduru kuja Dar Es Salaam. Haya mabasi yananyanyasa sana abiria. Kwanza kifungua kinywa ni mpaka saa 8 ukifika Nangurukuru. Watu wengine wana matatizo ya vidonda vya tumbo, hivi kuanzia Mangaka, Masasi mpaka Mtama hakuna hoteli? kwanini watu washinde njaa mpaka saa 8? Safari ni adhabu? Tatizo la pili hawajali na wanadharau sheria za nchi na maelekezo ya viongozi wa serikali. Magari yanaishia Temeke mwisho badala ya stendi kuu ya mabasi ya mikoani km sheria inavyoelekeza na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ametoa agizo kwamba mabasi yote yashushe na kupakia abiria stendi kuu ya mabasi tu na si sehemu nyingine wao wamepuuza. Hawa wamenunua serikali kupitia jeshi la polisi. Wamenitesa sana napakia mizigo kwenye daladala baadaye usafiri wa mizigo kuingia stendi maana nilikuwa niunganishe safari kwenda mkoa mwingine. Serikali ifuatilie kampuni hii, lazima wanatoa rushwa kuwanyanyasa wananchi waliolipia usafiri husika
 
Ninachokiona, ni jamaa anachafuliwa tu na wala hana hiyo kitu

Mwendo anaotembea ni mwendo wa kawaida sana, ukizingatia na zile gari ikizidi 85kph inakata inazima.


Tujaribu kuwa fair, jamaa anafanya kazi nzuri na anazingatia sheria zote.

Umeshaona gari za mpinzani wake zinavyokwenda na kufanya overtaking za hovyo? Mbona hizo hauziongelei?
Gari haizimi mdau ila ile alarm huwa inapiga kelele mpaka basi zima mnaona kero.......
 
Wakuu habari,

Ningependa kuishauri SUMATRA wawaite na kuwashauri wamiliki/madereva wa mabasi ya SAULI kuwa kusifiwa barabarani kwa ubingwa wao wa kukimbia speed kubwa na kuovertake bila mpangilio siku moja kutagharimu maisha ya abiria wasio na hatia.

Ushauri wangu ni huo kwenu SUMATRA msije sema hamkuambiwa.
Àcha uoga jombaa...mwisho wa siku tutàkufà tu...acha watu wawahi wàendako
 
Hao Sauli lao speed, kuna hii kampuni inaitwa Maning Nice inafanya biashara sehemu nyingi nchini. Nataka nizungumzie haya mabasi yake yanayotoka Tunduru kuja Dar Es Salaam. Haya mabasi yananyanyasa sana abiria. Kwanza kifungua kinywa ni mpaka saa 8 ukifika Nangurukuru. Watu wengine wana matatizo ya vidonda vya tumbo, hivi kuanzia Mangaka, Masasi mpaka Mtama hakuna hoteli? kwanini watu washinde njaa mpaka saa 8? Safari ni adhabu? Tatizo la pili hawajali na wanadharau sheria za nchi na maelekezo ya viongozi wa serikali. Magari yanaishia Temeke mwisho badala ya stendi kuu ya mabasi ya mikoani km sheria inavyoelekeza na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ametoa agizo kwamba mabasi yote yashushe na kupakia abiria stendi kuu ya mabasi tu na si sehemu nyingine wao wamepuuza. Hawa wamenunua serikali kupitia jeshi la polisi. Wamenitesa sana napakia mizigo kwenye daladala baadaye usafiri wa mizigo kuingia stendi maana nilikuwa niunganishe safari kwenda mkoa mwingine. Serikali ifuatilie kampuni hii, lazima wanatoa rushwa kuwanyanyasa wananchi waliolipia usafiri husika

Bebeni take aways
 
Madereva wawili wa Saul Walishawahi kufungiwa lesen kwa miez mitatu adhabu inayo fata ni kufutiwa lesen
 
Mbona polisi wanatukamata sana wengine tuki overspeed hata kidogo tu kwenye hiyo barabara? Nimeshakamatwa nikiwa 57km/h.

Sasa hao Sauli wanakutana na polisi wa tofauti? Kuna kila dalili za rushwa hapo.
Ha ha hao wanagawa hela wananunua hizo njia.. sasa ukijifanya kuwafata nyuma nyuma ndo utajua hujui.. wao wanapita ww unapigwa mkono!
 
Wakuu habari,

Ningependa kuishauri SUMATRA wawaite na kuwashauri wamiliki/madereva wa mabasi ya SAULI kuwa kusifiwa barabarani kwa ubingwa wao wa kukimbia speed kubwa na kuovertake bila mpangilio siku moja kutagharimu maisha ya abiria wasio na hatia.

Ushauri wangu ni huo kwenu SUMATRA msije sema hamkuambiwa.
Ingawa ni vyema magari yaruhusiwe kutembea kwa speed kubwa, naamini barabara zetu hazitupi uhuru huo kwa sasa.
 
Hawa jamaa nimekutana nao wawili, yaani anaovetake anaingia upande wangu tupo uso kwa uso lakini anakomaa mm ndio inabidi nipite vichakani kumpisha.... ujinga wao utacost maisha ya watu siku moja.
Ninaunga mkono hili. Haya mabasi ni bugudha kwa watumiaji wengine wa barabara sawa sawa na madereva wa magari ya serikali. Wanakwenda ovyo na kuovertake bila kujali watumiaji wengine wa barabara kiasi cha kulazimisha wewe ambaye uko kwenye njia yako umpishe au usimame. Pia wanalazimisha kuchomeka gari au basi lao mahali ambapo ni finyu ikisababisha adha kwa wengine. Hawa polisi wa barabarani wameshindwa kuwadhibiti hawa maderdva wa mabasi na magari ya serikali.
 
Mbona polisi wanatukamata sana wengine tuki overspeed hata kidogo tu kwenye hiyo barabara? Nimeshakamatwa nikiwa 57km/h.

Sasa hao Sauli wanakutana na polisi wa tofauti? Kuna kila dalili za rushwa hapo.
Kuna dereva wa bus fulani katika stori alisema"si kwamba sauli wanakimbia sana,wanapitisha hela,tochi haziwahusu kwahiyo hiyo inawasaidia kutosimama hovyo na ndipo wanapoyapiga gap magari mengine"
Ni dereva wa bus lililoshika chat sana kwa kuwahi kufika miaka ya 2010-2015
 
Back
Top Bottom