Ushauri wangu kwa serikali ya Jiji la Mwanza

Ushauri wangu kwa serikali ya Jiji la Mwanza

Undava King

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2017
Posts
3,422
Reaction score
5,675
Tukitaka jiji la Mwanza liwe bora kimwonekano lakini pia liongeze thamani ya ardhi na uwekezaji ambao utachangia mapato basi hatuna budi kuanza na ile mitaa ya daraja la juu na daraja la kati ambapo ni rahisi mno kufanya marekebisho kuliko ile ndoto ya mchana ya kuibadili mabatini kuwa real estate.

Mwanza ni tofauti na miji mingine mikubwa ambapo watu wenye kipato kikubwa uishi katika mazingira yanayowafaa peke yao pasipo changanyikeni.

Ile tunayojivunia nayo kama Capripoint waweza fikiri pengine ni mtaa kweli wa madon ila ukipata nafasi ya kuuona upande wake wa pili wenye umaskini wa kutupwa kule tunapaita Capripoint idara ya maji huwezi kuamini kama ndiyo huo huo mtaa mmoja.Kuna slums kule za washashi na wajaluo Ilemela ikasome.

Bwiru nako ukishika ile njia lilipo kanisa la AIC ukanyoosha ukielekea mwaloni, ukauvuka mwalo alafu ukaanza kupandisha kuelekea juu kuna slums za ajabu sana kule za ndugu zangu wasukuma hata baiskeli kuipitisha ni kazi.

Kwa ujumla Ilemela iko vizuri kuanzia kona ya kwenda Igombe kuzunguka mpaka Tunza na kurudi RFA kote huko pako njema kabisa.

Tatizo la Ilemela liko ile mitaa ya mahakama na kule juu milimani lakini nako hakuna slums choka mbaya sana kama zile za Capripoint na Bwiru.

Kipi kifanyike kukamilisha uzuri wa Capripoint na Bwiru.
Serikali ikawalipe fidia wamiliki wa zile slums kwa awamu kulingana na uwezo wao wa mfuko kisha mabanda yale yavunjwe na kisha serikali iuze viwanja kwa faida kubwa.

Serikali ikimaliza hapo ihamie eneo la Bugando mtaa wa miembeni kuna slums za kufa mtu lakini wale jamaa wakilipwa fidia wakaliacha wazi lile eneo serikali inaweza kuliuza kwa faida kubwa sana tu.
 
Muonekano upi? MWanza kwanza ni Chafu sana na inanuka sana hilo moja.Pili ni kwamba Bila kuweka siasa na kuondoa wamachinga barabarani hakuna cha muonekano utakao tokea.Wachuuzi ndio waharibifu wa miji namba 1. Miji ni michafu sana hasa hio Mwanza.
 
Unaongea kana kwamba uko sayari tofati, hao unao sema waondolewa ndio wanyonge wa hii nchi, hao ni Industry ya kuproduce kura za wanasiasa hakuna wa kuwaonda hapo

Sio MWanza tu bali ni nchi nzima,njoo Arusha full chafu imejaaa wachuuzi tupu.
 
Kiukwelo sijawah fika hayo maeneo nasikia tu
Serikali ingewahamisha wenye uwezo wapendezeshe mji bana
 
Yaan we unataka wenzako wataabike kisa kupendezesha mji wa Mwanza? Halafu ukipendeza hao waathirika wanaotafuta riziki zao utawalisha wewe?.

Kwanza mwanza ni KICHUGUU kilichojegwa nyumba,siku kikiporomoka itakuwa hatari.
 
Ukishajipata ndo unaanza kutamani watu na maeneo vigawanywe, ila ukiwa kama mimi huwez kuwaza upuuzi huu
Umasikini siyo sifa ya kujivunia achana na huo ujinga dunia nzima inatambua kuna madaraja na katu hatulingani, kwahiyo kama ni masikini ndiyo uruhusu Tanzania nzima iwe na mwonekano wa dhiki ya mabanda kila mahali?

Isitoshe hapa nawaongelea hao hao wanyonge hili wapate fidia wakaishi maisha yanayofaa huku wakiachia maeneo promising kwa ajili ya watu wenye uwezo mkubwa kuwekeza na pesa inayopatikana hapo ndiyo itakayorudi kwa mnyonge huyo huyo kumboreshea miundombinu.
 
Yaan we unataka wenzako wataabike kisa kupendezesha mji wa Mwanza? Halafu ukipendeza hao waathirika wanaotafuta riziki zao utawalisha wewe?.

Kwanza mwanza ni KICHUGUU kilichojegwa nyumba,siku kikiporomoka itakuwa hatari.
Soma uelewe uzi kabla ya ku-comment, nimeshauri watu walipwe fidia wahame katika maeneo hayo kupisha uwekezaji mkubwa katika ardhi yenye thamani kubwa ambayo haitumiwi kimanufaa, kwa lugha nyepesi kuacha mtu mmoja ajenge banda lenye thamani ya milioni 9 kwenye ardhi iliyopaswa kuuzwa kati ya mil. 800 hadi bilioni moja ni uzwazwa.

Kwa kuwa ni pesa nyingi sana zinakuwa zimepotea na halmshauri ya jiji inazidi kuwa masikini na watu wake, huku rasilimali za kuwanasua wanazo na wamezikalia tu.
 
Hao ni wanyonge, hawawezi hamishwa na kabla ya hao waanze kudokoa wachuuzi Barabarani, hao ndio shida namba 1
Uwezi kumficha mwanao asionwe na majirani (tatizo la ajira) walahu unaweza mfichia aibu kwa kumstiri na mavazi mapya wasimwone makalio wazi (kuwapatia wenye uwezo fursa ya kuisitiri miji yetu kwa nyumba zao bora milimani ni kibarua chepesi kuliko kuondoa wamachinga)
 
Unaongea kana kwamba uko sayari tofati, hao unao sema waondolewa ndio wanyonge wa hii nchi, hao ni Industry ya kuproduce kura za wanasiasa hakuna wa kuwaonda hapo

Sio MWanza tu bali ni nchi nzima,njoo Arusha full chafu imejaaa wachuuzi tupu.
Mabadiliko makubwa siku zote uanza kidogo kidogo hatuwezi kukaa na kujikatia tamaa kuwa Tanzania yetu imetushinda hata kama serikali ya nchi hii haitujali.
 
Muonekano upi? MWanza kwanza ni Chafu sana na inanuka sana hilo moja.Pili ni kwamba Bila kuweka siasa na kuondoa wamachinga barabarani hakuna cha muonekano utakao tokea.Wachuuzi ndio waharibifu wa miji namba 1. Miji ni michafu sana hasa hio Mwanza.
Wachuuzi hawaondolewi kwa nguvu ya dola na matamko ya wanasiasa, bali nchi kujaa wachuuzi na bodaboda ni elementi kuwa serikali kwa kiasi kikubwa imefeli kuinua hali ya kipato cha wananchi wake na hivyo umasikini umetamalaki kila mahali.
 
Unawaongelea jiji gani hawa hawa wa mwanza? Ambao wameshindwa walau kulipa fidia maeneo yaliyowazi wakapanga mji na wakauza viwanja kwa faida kubwa tu, waje wapate pesa ya kuwalipa hao waliokwisha jenga? Labda muwekezaji mwenyewe ahamue kuwaondoa mmoja mmoja yeye mwenyewe lakini sio jiji, nikuulize mara ya mwisho umesikia jiji wanauza viwanja Vilivyopangwa na kupimwa ni lini, Watu wamestaarabika kuna wanaohitaji sehemu zilizopangwa vyema lakini hazipo, Badala ya kuhangaika na hao ni vyema wangeenda maeneo kama Sawa, Lwanima, Isebanda na huko usagara na kisesa wakalipa fidia maeneo yaliyowazi wapange wapime ili mji usiendelee kujengwa kiholela
 
Suala la kupanga mji jiji walipaswa kuliona kama fursa mtu anatoka zake mkoani tuseme Simiyu ama Geita Ana ndoto zake za kujenga mwanza anafika ofisi za ardhi hawana viwanja, anaingia mitaani anakutana na madalali hapo atapelekwa kwenye Squatter tu na kwa vile hana namna inabidi achukue tu angalau kidogo Ilemela huwa nasikia wakitangaza miladi ya viwanja japo sina hakika kama bado vipo
 
Tukitaka jiji la Mwanza liwe bora kimwonekano lakini pia liongeze thamani ya ardhi na uwekezaji ambao utachangia mapato basi hatuna budi kuanza na ile mitaa ya daraja la juu na daraja la kati ambapo ni rahisi mno kufanya marekebisho kuliko ile ndoto ya mchana ya kuibadili mabatini kuwa real estate.

Mwanza ni tofauti na miji mingine mikubwa ambapo watu wenye kipato kikubwa uishi katika mazingira yanayowafaa peke yao pasipo changanyikeni.

Ile tunayojivunia nayo kama Capripoint waweza fikiri pengine ni mtaa kweli wa madon ila ukipata nafasi ya kuuona upande wake wa pili wenye umaskini wa kutupwa kule tunapaita Capripoint idara ya maji huwezi kuamini kama ndiyo huo huo mtaa mmoja.Kuna slums kule za washashi na wajaluo Ilemela ikasome.

Bwiru nako ukishika ile njia lilipo kanisa la AIC ukanyoosha ukielekea mwaloni, ukauvuka mwalo alafu ukaanza kupandisha kuelekea juu kuna slums za ajabu sana kule za ndugu zangu wasukuma hata baiskeli kuipitisha ni kazi.

Kwa ujumla Ilemela iko vizuri kuanzia kona ya kwenda Igombe kuzunguka mpaka Tunza na kurudi RFA kote huko pako njema kabisa.

Tatizo la Ilemela liko ile mitaa ya mahakama na kule juu milimani lakini nako hakuna slums choka mbaya sana kama zile za Capripoint na Bwiru.

Kipi kifanyike kukamilisha uzuri wa Capripoint na Bwiru.
Serikali ikawalipe fidia wamiliki wa zile slums kwa awamu kulingana na uwezo wao wa mfuko kisha mabanda yale yavunjwe na kisha serikali iuze viwanja kwa faida kubwa.

Serikali ikimaliza hapo ihamie eneo la Bugando mtaa wa miembeni kuna slums za kufa mtu lakini wale jamaa wakilipwa fidia wakaliacha wazi lile eneo serikali inaweza kuliuza kwa faida kubwa sana tu.
Sijui Mwanza ilivurugwaje ndugu yangu; mpaka mwishoni mwa miaka ya tisini Mwanza lilikuwa jiji lenye kupendeza sana lakini leo hii Mwanza ni takataka tupu.

Ukifika pale Mwaloni pako hovyo kabisa

1713725976535.png


Huko milimani ndiko pamajengwa utadhani siyo sehemu ya mji

1713726110828.png



Ni tofauti kabisa na miji mingine iliyojengwa milimani kama vile huko Italy
1713726352282.png
 
Soma uelewe uzi kabla ya ku-comment, nimeshauri watu walipwe fidia wahame katika maeneo hayo kupisha uwekezaji mkubwa katika ardhi yenye thamani kubwa ambayo haitumiwi kimanufaa, kwa lugha nyepesi kuacha mtu mmoja ajenge banda lenye thamani ya milioni 9 kwenye ardhi iliyopaswa kuuzwa kati ya mil. 800 hadi bilioni moja ni uzwazwa.

Kwa kuwa ni pesa nyingi sana zinakuwa zimepotea na halmshauri ya jiji inazidi kuwa masikini na watu wake, huku rasilimali za kuwanasua wanazo na wa
Suala la kupanga mji jiji walipaswa kuliona kama fursa mtu anatoka zake mkoani tuseme Simiyu ama Geita Ana ndoto zake za kujenga mwanza anafika ofisi za ardhi hawana viwanja, anaingia mitaani anakutana na madalali hapo atapelekwa kwenye Squatter tu na kwa vile hana namna inabidi achukue tu angalau kidogo Ilemela huwa nasikia wakitangaza miladi ya viwanja japo sina hakika kama bado vipo
Bonge la point kaka, upo sahihi sana kwa ulichoongea
Maendeleo ya mji ndio maendeleo ya watu
 
Maendeleo ya mji ndio maendeleo ya watu
Hapo pia nimeongelea suala la kuongeza mapato, ipo hivi viwanja Vilivyopangwa na kupimwa na serikari pia huwa ni sehemu ya kuongeza mapato, Kiwanja kinachouzwa na serikari kinanunuliwa haraka kwa sababu ya ubora na assurance hivyo pesa itakayowekwa huko italudi ndani ya mda mfupi na faida juu, Labda jamaa zetu wazee wa kuvigawania ofisini waamue kuvikwiba tofauti na hapo ni chap sana hiyo pesa inaludi
 
Muonekano upi? MWanza kwanza ni Chafu sana na inanuka sana hilo moja.Pili ni kwamba Bila kuweka siasa na kuondoa wamachinga barabarani hakuna cha muonekano utakao tokea.Wachuuzi ndio waharibifu wa miji namba 1. Miji ni michafu sana hasa hio Mwanza.
Nilishawai kusema miji inachafuliwa na Wamachinga....
 
Sijui Mwanza ilivurugwaje ndugu yangu; mpaka mwishoni mwa miaka ya tisini Mwanza lilikuwa jiji lenye kupendeza sana lakini leo hii Mwanza ni takataka tupu.

Ukifika pale Mwaloni pako hovyo kabisa

View attachment 2970460

Huko milimani ndiko pamajengwa utadhani siyo sehemu ya mji

View attachment 2970466


Ni tofauti kabisa na miji mingine iliyojengwa milimani kama vile huko Italy
View attachment 2970473
Miji yetu imevurugwa na sera mbovu za CCM ambazo hazijali ustawi bora wa nchi na maendeleo ya watu, hawataki kusikia kitu kinaitwa mipango miji kama wajibu wao na badala yake huo ni mzigo wa serikali za mitaa ambapo mwenyekiti wa mtaa kwa busara zake na wajumbe wa nyumba kumi ndiyo watupangie mitaa yetu.

Hatuwezi kubomoa tulipokosea tiyari ila tunaweza kurekebisha ambapo hatujaanza, amini kuwa hapa tunapoona tumepajenga katika miji yetu ni sehemu ndogo tu ya taswira ya miji hiyo miaka 100 ijayo hivyo tukianza leo kuipangilia miji yetu kule inakotanukia na tukawa serious basi vizazi vijavyo vitatushukuru na kama gugu ni CCM basi kwa umoja wetu bila kupepesa macho umma uamke tuling'oe hatuwezi vumilia kuwa na taifa la ajabu linalozidi kutopea katika umasikini kana kwamba watanzania wote hatuna akili.
 
Back
Top Bottom