Unawaongelea jiji gani hawa hawa wa mwanza? Ambao wameshindwa walau kulipa fidia maeneo yaliyowazi wakapanga mji na wakauza viwanja kwa faida kubwa tu, waje wapate pesa ya kuwalipa hao waliokwisha jenga? Labda muwekezaji mwenyewe ahamue kuwaondoa mmoja mmoja yeye mwenyewe lakini sio jiji, nikuulize mara ya mwisho umesikia jiji wanauza viwanja Vilivyopangwa na kupimwa ni lini, Watu wamestaarabika kuna wanaohitaji sehemu zilizopangwa vyema lakini hazipo, Badala ya kuhangaika na hao ni vyema wangeenda maeneo kama Sawa, Lwanima, Isebanda na huko usagara na kisesa wakalipa fidia maeneo yaliyowazi wapange wapime ili mji usiendelee kujengwa kiholela