Kinumbo
JF-Expert Member
- Dec 8, 2019
- 3,188
- 5,811
Napenda kutoa ushauri huu kwa wafuasi wa CHADEMA na wanao kiunga mkono kwa namna moja ama nyingine. Toka uongozi mpya uingie madaraka katika chama hicho yaani mwenyekiti wake Tundu Lissu na makamu wake John Heche kumekuwa na kashi kashi nyingi za hapa na pale.
Kwa asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania ni wazi kuwa wanaelewa kuwa katika nchi hii katika chaguzi zake huwa sio za haki na zisizo fuata sheria. Hio iko wao na inaeleweka bila kupepesa macho ata walioko madarakani wanatambua hivyo. Kutokana na hilo CHADEMA ilianza kutoa elimu kwa wananchi ili kupata uelewa wa masuala hayo, hali hiyo ilipelekea mwenyekiti wake kukamatwa na kupewa kosa ya uhaini.
Ushauri wangu viongozi wa CHADEMA kwa sasa wakiongozwa na makamu mwenyekiti John Heche achaneni na hayo mambo fanyeni mambo yenu mengine. Kwa sababu hao mnao itakidi kuwapambania (wananchi) hawana muda kabisa, ndio maana mnakamatwa hadharani kama kuku na hawafanyi chochote, hebu fikiria ingekuwa Kenya.
Kiufupi mnapambana wenyewe, wafuasi na baadhi ya wananchi wanao fuata sera zenu hawako tayari kuwa pamoja na nyie ni waoga kupindukia. John Heche alisema wakutane mahakamani Kisutu, Murilo akapiga biti hakuna mtu kusogea na kweli hawajafika kwa hiyo mnaweza ona ni aina gani ya watu mko nao.
Mimi sio mfuasi wa chama chochote kile cha siasa ila Mwalimu John Heche ile elimu anayo toa kwa wananchi ni wazi kabisa inamgusa kila raia, tatizo liko kwa hao raia. Kiukweli wanao kiunga chama hicho ndio wanawaangusha. Mtaishia kuumizwa na polisi bure, kwahiyo achaneni na hayo masuala.
Leo baadhi ya viongozi wenu wameumizwa na makamu wenu John Heche pamoja na katibu wake John Mnyika mpaka sasa hawajulikani walipo na wafuasi wenu wamekaa kimya tu.
Hawa mnao itakidi mnawapigania (wananchi) hawako tayari na ndio wanawaangusha.
Kwa asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania ni wazi kuwa wanaelewa kuwa katika nchi hii katika chaguzi zake huwa sio za haki na zisizo fuata sheria. Hio iko wao na inaeleweka bila kupepesa macho ata walioko madarakani wanatambua hivyo. Kutokana na hilo CHADEMA ilianza kutoa elimu kwa wananchi ili kupata uelewa wa masuala hayo, hali hiyo ilipelekea mwenyekiti wake kukamatwa na kupewa kosa ya uhaini.
Ushauri wangu viongozi wa CHADEMA kwa sasa wakiongozwa na makamu mwenyekiti John Heche achaneni na hayo mambo fanyeni mambo yenu mengine. Kwa sababu hao mnao itakidi kuwapambania (wananchi) hawana muda kabisa, ndio maana mnakamatwa hadharani kama kuku na hawafanyi chochote, hebu fikiria ingekuwa Kenya.
Kiufupi mnapambana wenyewe, wafuasi na baadhi ya wananchi wanao fuata sera zenu hawako tayari kuwa pamoja na nyie ni waoga kupindukia. John Heche alisema wakutane mahakamani Kisutu, Murilo akapiga biti hakuna mtu kusogea na kweli hawajafika kwa hiyo mnaweza ona ni aina gani ya watu mko nao.
Mimi sio mfuasi wa chama chochote kile cha siasa ila Mwalimu John Heche ile elimu anayo toa kwa wananchi ni wazi kabisa inamgusa kila raia, tatizo liko kwa hao raia. Kiukweli wanao kiunga chama hicho ndio wanawaangusha. Mtaishia kuumizwa na polisi bure, kwahiyo achaneni na hayo masuala.
Leo baadhi ya viongozi wenu wameumizwa na makamu wenu John Heche pamoja na katibu wake John Mnyika mpaka sasa hawajulikani walipo na wafuasi wenu wamekaa kimya tu.
Hawa mnao itakidi mnawapigania (wananchi) hawako tayari na ndio wanawaangusha.