Habari ya usiku huu wanajukwaa?
Kwanza niwape hongera ya kuwa hadi muda huu tuko tunaendelea kupambana na hali hii ya maisha katika uchumi uliovurugwa na wavurugaji, hopefully tutasurvive as we keep on surviving.
Kama kichwa kilivyojieleza hapo juu, uzi huu nautoa ushauri wangu kwa taasisi muhimu katika ujenzi wa demokrasia(vyama vya upinzani).
Kesho tarehe 16 september kuna uchaguzi katika jimbo la ukonga. Kwa hakika kabisa ninajua (hata upinzani wanajua) kuwa Mwita waitarav(mgombea wa CCM ) atashinda. Ndio 'ATASHINDA'. Baada ya hapo Upinzania utatoa malalamiko kuwa wameibiwa kura, mkurugenzi kamatangaza isivyo halali, vituo vimeongezwa. Watalalamika kama ilivyo kawaida miaka yote.
Chadema wanajua kuwa kila mwaka wanashindwa kwa njia na mbinu zile zile. Mule ndani wanao 'wanaccm' wanajua ni vipi ambavyo upinzani huwa unashindwa..
Wanajua fika ni vipi ambavyo council inakisaidia 'tawala' katika masuala ya kifedha mathalani za mafuta kipindi cha kampeni, inajua ni vipi polisi na council zinakisaidia katia upangaji wa ratiba za kampeni, inajua ni vipi jimbo kama ukonga RSO, DSO, RPC, OCD, DC, RC, na vyombo vyote vya dola na team zao zinahamia kule, wanajua fika huyo DED hana nguvu ya 'kusimamia upinzani' ikiwa kweli 'haki' iko kwao-yupo DED mmoja huko usukumani, alimpigia magoti ex SG wa 'tawala' baada ya kushindwa na upinzani. Wanajua mapilato wengi hawawezi kusimamia kweli baada ya chaguzi..
Ni ajabu kuwa still upinzani unasimamisha wagombea katika mazingira yale yale. Ni wakati sasa wa upinzania kususia chaguzi hizi completely kwani kushiriki ni kuhalalisha mifumo hii mbovu iliyopo. Kama wanashiriki basi hakuna haja ya kuja kusimama mbele ya jamii na kulalamikia mambo yale yale kila siku...
By the way, tujiandae na kule nyanda za juu kusini....