Ushauri wako utanisaidia kwa hili

Ushauri wako utanisaidia kwa hili

1992erick

Member
Joined
Dec 28, 2012
Posts
94
Reaction score
29
Mimi ni mwanachuo wa chuo fulani jijini mbeya, mwakani namaliza degree yangu ya kwanza ya ENG. ya miaka 4. lakini hiki ninachosomea sio kama nilikipenda sana, hapana, sikujua nijaze nn wakati ule na mshawasha wa kwenda chuo.

malengo yangu yalikua kuja kua daktari, lakini wanasema hujafa hujaumbika vikatokea vikwazo ambavyo sitasahau vikazima ndoto ile, lakini saiv moyo unanisuta mawazo yananiambia huku sio kwako ulikuja tu rudi ulipotaka.

nataka nikimaliza nirudie cheti changu cha form 4 nikaanze diploma CLINICAL OFFICER mwakani kisha degree, umri wa sasa 22yrs mwakani 23

nipe ushauri wako

asanteni
 
Nisawa kutokana na MAWAZO yako! lakn nakushauri. MALIZA hiyo ENG. pia uingie serikaln. hiyo dp ya C.O sikushaur saana...
 
Maliza kwanza hiyo shahada yako baada ya hapo ndo uangalie namna ya kufikia malengo yako ya kuwa daktari.
 
Ni wazo lako kwa kile ukipendacho. ila nakushauri uendelee na hyo fani uliyosotea kwa muda mrefu, hata hivyo bado una umri mdogo kupoteza muda kurudi nyuma...
 
kwanza nikupongeze kwa hatua hiyo uliofikia..kazana kwanza umalize. lkn pia hakuna kitu kinaleta motisha wa kazi kama kufanya kile ukipendacho. kwa kuwa unadegree waweza kusoma clinical medicine na ukaja soma masters ya public health.miaka 3 sio kitu ktk kujenga future ya miaka mingi ijayo Mungu atujaliapo uhai. kuna watu wako na miaka zaidi ya 40 wanasoma certificate diploma n.k. timiza ndoto zako.
 
Asanteni wakuu sana nimewaelewa sana SANA sana, kipasta many thanks mkuu, papa oti, suka, tabora thank you.

Bado napenda kueleweshwa zaidi na zaidi

Asanteni kwa haya machache.
 
Back
Top Bottom