INAENDELEA.....
Basi mimi nikiwa zangu huko Sierra Leone wadau wangu waliokuwa wanamfahamu wakawa wananiambia yanayoendelea huku. Maana alikua anafanya kazi sehemu fulani ofisi ya public. Alikua akiuliza Meraki yuko wapi siku hizi, hata pale dukani kwake simuoni. Nilienda nikamkuta mama mmoja akadai yeye ni mama yake na Meraki akaniambia mwanawe amesafiri kidogo.
Ni kweli dukani kwangu nilimuacha mama yangu mzazi, uzuri hakumuambia exactly niko wapi. Na washkaji hawakumuweka wazi nilipo.
Kumbe akapata bwana mzungu, baada ya kuona mimi sina uelekeo naye tena. Mzungu alikuja huku kwa project ya miezi 3 na shirika moja la kimataifa. Ni mmarekani ila kituo chake cha kazi ni Thailand. Ndipo walipokutana na kuanza kudate.
Dada alianza kubadilika. Akawa mlevi sana inasemekana unga na shisha alikua anavuta. Akawa teja kabisa. Alikua na pesa sana akanunua viwanja double kule Kibada, 50x100 viwili na kuanza harakati za ujenzi. Kabla mambo yaive, mzungu akawa anarudi Thailand. Wakakubaliana waondoke wote.
Wazazi wakagoma. Hawezi kuondoka na mtu bila ndoa. Ndipo ikabidi mama yake amhoji, wakati unasoma mwanangu uliniambia kuna mtu anaitwa Meraki yuko wapi? Mbona ulikua ukinisimulia ni kijana mzuri tu....ikabidi atoboe siri Meraki hajui yuko wapi. Anahisi alishamwacha ndipo akaangukia mikono ya mzungu. Mama akagoma, akasema kwanza huyo mzungu ni mkristo na wala hajakuoa, na wala sisi hatumfahamu unawezaje kuondoka naye?
Ikabidi Mmarekani ajipeleke kwa wazazi wa binti kuwaaminisha. Haikufua dafu. Mzungu ikabidi aondoke, wabaki wanawasiliana tu. Uchumi wake ukarudi pale pale two squared kama zamani. Ila ulevi hakuacha na akapata mimba. Alinusurika kufa wakati wa kujifungua, alikimbizwa toka Amana mpaka Muhimbili ambapo alilazwa siku 17. Mtoto akakosa, Alhamdulillah alibaki salama.
Mwaka huu January nilinunua eneo kule Kibada. Juzikati hapo dalali yule akanipigia bwana kuna eneo jirani na uliponunua pale kwenye matofali kunauzwa. Nikamwambia mbona eneo kubwa sana lile ntaliweza? Akasema ni nusu yake inauzwa. Nikamwambia tuonane leo Jumapili.
Leo nikawasha kitoy changu na mamsapu pembeni tukaenda. Kufika nikamkuta dalali na mama mmoja. Haraka haraka nikamfananisha na x wangu lakini sikutilia maanani. Katika maongezi si ndio akasema eneo hili ni la bint yangu tukikubaliana atakuja kuweka saini. Machale yakanicheza. Ikanibidi nichokonoe. "Mama, bint yako ndio yule xxx (nikirefer anakofanya kazi). Ndio, kwani unamfahamu? Akajibu mama. Nikamwambia nimeona mnafanana, yule dada namfahamu. Mamsapu akanikata jicho.
ITAENDELEA.....