Carnivora
JF-Expert Member
- Jan 26, 2018
- 3,650
- 6,028
Habari za Jumapili wadau
Kuna sintofahamu kuhusu usalama wa privacy zetu humu lakini watajua wenyewe. Watakuwa wameshauza ramani ya vita kwa adui. Sasa hatuandiki tena habari wanazozitafuta. Shauri zao....twende kwenye mada.
Mke wa best yangu, rafiki yangu wa kufa na kuzikana, siku moja nilimueleza kitu naye akanishauri bila kumuomba ushauri, au niseme alitoa maoni yake.
Ilikua tunapita mahali karibu na duka, rafiki yangu akaingia dukani kununua baadhi ya vitu mimi nikabaki na shemeji tukitembea mdogo mdogo ili tusije mwacha jamaa mbali. Kipindi hicho wana mwaka 1 tu wa ndoa yao.
Nikamwambia shemeji mi nataka kuoa ila mwanamke ninayetaka kumuoa hayuko tayari kwa sasa, nataka kuforce. Kimsingi mwanamke huyo ameshamaliza masomo na ameshaanza kazi ana kipato cha kujikimu lakini hayuko tayari kwa ndoa muda huu. Akaniuliza sababu ni nini? Nikamjibu mwanamke anasema anahisi ana deni kwa familia yake, yaani anawaza kuijengea, kuihudumia, na kuipa sapoti na hasa mama yake mzazi. Kwa hiyo hadi atakapoona familia hiyo ipo kwenye hatua anayoitaka ndio awe tayari kwa ndoa.
Akahoji, hayo yatachukua muda gani? Jibu langu likawa kwa kweli sijui. Akaniambia, shem huyo mwanamke achana naye. Ndio yule xxx (akamtaja) uliesema mwanafunzi wa chuo? Sasa mtu umekuwa naye miaka yote hiyo alisema umngoje amalize masomo sasa hivi ameanza drama zingine .
Akaendelea, sikia shem, watu mnapofunga ndoa miaka ya mwanzoni mnakomaa sana kujijenga kimaisha. Kama mna viwanja muanze kukomaa kujenga mnajibana hivyo hivyo mnakwenda. Sasa mtu ambaye anawaza kwao, kila kitu kwao, afanye maendeleo na familia yake kwanza ndio aangalie ndoa hamtafika popote. Hii hata kama mwanaume ana mawazo ya leo kwao, kesho kwao, kila kitu kwao hamtafanya lolote. Familia zipo tu na msaada kwa familia hauishi leo wala kesho. Inabidi mkomae mjiimarishe kwanza kisha ndio muangalie kuna nini kimesalia...ina maana ye' anawaza kuendeleza kwao huyo mtashauriana naye jambo gani sasa?
Akauliza, kwani huko kwao ni familia ya shida? Nikamjibu hapana. Familia ya kawaida tu si tajiri lakini sio masikini. Yeye mwenyewe, dada yake na mdogo wao wa mwisho mzee wao kamudu kuwasomesha private tangu shule za msingi na wanaishi vizuri tu. Na mama yake ni mjasiliamali pia ila ndio hivyo tu anataka kuonekana ni hero of the family. Akasema, atakupotezea muda huyo. Oa mwanamke mkae mpange mipango yenu mwanamke anayewaza kwao kila kitu na wakati yuko kwenye ndoa hamtafanya la maana. Ni miaka kadhaa imepita, lakini mpaka leo nayakumbuka maneno yake shemeji.
Siku moja nilijifanya kukomaa naye kuwa mi nataka kupeleka posa kwao la sivyo napiga chini. Alichonijibu....kama unaniacha kisa nimekataa ndoa ni sawa tu. Sipo tayari kwa kweli. Siwezi kukimbilia ndoa baadae inishinde. Nikamuuliza kinamshinda nini? Hana majibu.
Nikapiga chini kimya kimya. Hakugundua. Alikuja kushtuka hatuko kama zamani. Why this, why siku hizi uko kimya, why hivi mara vile. Sikumpa majibu yaliyoeleweka. Soon kidogo nikapata deal nikaenda Sierra Leon nikakaa miaka 2, akawa hanipati kwa simu ukawa ndio mwisho wetu.
Kuna sintofahamu kuhusu usalama wa privacy zetu humu lakini watajua wenyewe. Watakuwa wameshauza ramani ya vita kwa adui. Sasa hatuandiki tena habari wanazozitafuta. Shauri zao....twende kwenye mada.
Mke wa best yangu, rafiki yangu wa kufa na kuzikana, siku moja nilimueleza kitu naye akanishauri bila kumuomba ushauri, au niseme alitoa maoni yake.
Ilikua tunapita mahali karibu na duka, rafiki yangu akaingia dukani kununua baadhi ya vitu mimi nikabaki na shemeji tukitembea mdogo mdogo ili tusije mwacha jamaa mbali. Kipindi hicho wana mwaka 1 tu wa ndoa yao.
Nikamwambia shemeji mi nataka kuoa ila mwanamke ninayetaka kumuoa hayuko tayari kwa sasa, nataka kuforce. Kimsingi mwanamke huyo ameshamaliza masomo na ameshaanza kazi ana kipato cha kujikimu lakini hayuko tayari kwa ndoa muda huu. Akaniuliza sababu ni nini? Nikamjibu mwanamke anasema anahisi ana deni kwa familia yake, yaani anawaza kuijengea, kuihudumia, na kuipa sapoti na hasa mama yake mzazi. Kwa hiyo hadi atakapoona familia hiyo ipo kwenye hatua anayoitaka ndio awe tayari kwa ndoa.
Akahoji, hayo yatachukua muda gani? Jibu langu likawa kwa kweli sijui. Akaniambia, shem huyo mwanamke achana naye. Ndio yule xxx (akamtaja) uliesema mwanafunzi wa chuo? Sasa mtu umekuwa naye miaka yote hiyo alisema umngoje amalize masomo sasa hivi ameanza drama zingine .
Akaendelea, sikia shem, watu mnapofunga ndoa miaka ya mwanzoni mnakomaa sana kujijenga kimaisha. Kama mna viwanja muanze kukomaa kujenga mnajibana hivyo hivyo mnakwenda. Sasa mtu ambaye anawaza kwao, kila kitu kwao, afanye maendeleo na familia yake kwanza ndio aangalie ndoa hamtafika popote. Hii hata kama mwanaume ana mawazo ya leo kwao, kesho kwao, kila kitu kwao hamtafanya lolote. Familia zipo tu na msaada kwa familia hauishi leo wala kesho. Inabidi mkomae mjiimarishe kwanza kisha ndio muangalie kuna nini kimesalia...ina maana ye' anawaza kuendeleza kwao huyo mtashauriana naye jambo gani sasa?
Akauliza, kwani huko kwao ni familia ya shida? Nikamjibu hapana. Familia ya kawaida tu si tajiri lakini sio masikini. Yeye mwenyewe, dada yake na mdogo wao wa mwisho mzee wao kamudu kuwasomesha private tangu shule za msingi na wanaishi vizuri tu. Na mama yake ni mjasiliamali pia ila ndio hivyo tu anataka kuonekana ni hero of the family. Akasema, atakupotezea muda huyo. Oa mwanamke mkae mpange mipango yenu mwanamke anayewaza kwao kila kitu na wakati yuko kwenye ndoa hamtafanya la maana. Ni miaka kadhaa imepita, lakini mpaka leo nayakumbuka maneno yake shemeji.
Siku moja nilijifanya kukomaa naye kuwa mi nataka kupeleka posa kwao la sivyo napiga chini. Alichonijibu....kama unaniacha kisa nimekataa ndoa ni sawa tu. Sipo tayari kwa kweli. Siwezi kukimbilia ndoa baadae inishinde. Nikamuuliza kinamshinda nini? Hana majibu.
Nikapiga chini kimya kimya. Hakugundua. Alikuja kushtuka hatuko kama zamani. Why this, why siku hizi uko kimya, why hivi mara vile. Sikumpa majibu yaliyoeleweka. Soon kidogo nikapata deal nikaenda Sierra Leon nikakaa miaka 2, akawa hanipati kwa simu ukawa ndio mwisho wetu.