Ushauri wa kupata usingizi mchana

Ushauri wa kupata usingizi mchana

Watu hamchoki kabisa
Sikuwa na hii shida awali ila niliumwa mgongo sasa zile dawa za pingili za mgongo sijui ndio zimeniachia hii shida, kwani dawa Zake nyingi nilikuwa nikinywa nakuwa kama teja, nalala muda wote, nahisi baada ya kuzizoea kwenye mwili hii hali ndio imenikuta, tena nikishtuka hvyo nakuwa full of energy sipati usingizi, naweka simu mbali lakini haisaidii, nalazimisha kufunga macho ila bado
 
Kama na mtu wako yupo free muda huo,piga viwili.

Usipolala baada ya hapo nenda hospitali!
 
Ma
Tengeneza mazingira unayolala kuwe na ubaridi kidogo, oga maji ya baridi kidogo kama unakaa mikoa yenye joto kama yenye baridi ni vizuri uvae soksi, alafu punguza screentime angalau nusu saa kabla ya kulala, punguza taa zenye mwanga mkali,

Au punguza maongezi kichwani mwako au jitahidi usiwe unawaza mambo kabla ya kulala
ongezi kichwani ni nini?na unapunguzaje?
 
Bora kukosa usingizi mchana ila sio usiku, mimi nasumbuliwa na kukosa usingizi usiku nikillala saa tano nikkishtuka saa sita ni mpaka kesho saa tano tena ndio nitalala, hii hali inanitesa sana, nikilala kosa ni kushtuka
umejaribu kupiga safari kubwa mbili kabla ya kulala?
 
Ma

ongezi kichwani ni nini?na unapunguzaje?
Ni kama mawaza ila yanakuwa kwenye mfumo wa mazungumzo
Mf: unataka kwenda dukani ila unahofia watakuwa wamefunga sasa haya mawazo yakuwa kwenye mazungumzo
" sijui jamaa atakuwepo, nisije kwenda alafu hayupo nikawa najisumbua tu, au sijui niende tu hivyo nikimkosa ntaenda duka lingine"

Sasa mara nyingi usiku ukienda kulala ubongo huwa na tabia ya kukumbuka matukio ya siku nzima uliyofanya, ukianza kuwaza na kutumia huo mfumo wa maongezi (internal monologue) unachelewa mno kulala
 
Back
Top Bottom