KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Wewe hutaki kuelewa ninachoandika au unapindisha tu maksudi na kujifanya huelewi.Mimi nawaambia wanaojitambua wasipoteze muda wao kwenda kupanga mstari kwenye box la kura, labda itumike njia tofauti na hiyo ya box la kura. Kama wewe bado unaamini kuwatoa ccm kwa njia ya box la kura basi kazana kushawishi watu waende, mimi nimechagua kuwaambia kuwa box la kura ni kupoteza muda.
Wewe hutaki kuelewa ninachoandika au unapindisha tu maksudi na kujifanya huelewi.
Ni wapi nilipoandika kuwa 'ninaamini kuwa kupiga kura na kuishia hapo' ndio itakuwa njia ya kuwaondoa CCM?
Huwezi kuwa mtu 'unayejitambua' halafu ukaacha kupigania haki yako.
Wewe "usiekuwa na muda wakupoteza" usitupotezee muda na kutuwekea visingizio vya kuwalinda hao usiotaka tuwatoe madarakani. Ni lazima tuwe na mahali pa kuanzia, na kwenda kupiga kura ni sehemu mhimu ya kianzio cha mengine inapolazimu.Unapigania haki yako kwa box la kura njia ambayo imeshaonyesha wazi kufeli? Njia ya kura haitowatoa ccm zaidi ya machafuko. Tawala nyingi za kiafrika huwa hazijeshimu demokrasia ya kura, bali machafuko pekee ndio huleta mabadiliko na haki. Kama una ndugu na jamaa wenye muda wa kupoteza kapangeni mstari kwenye box la kura muwatoe ccm.
Wewe "usiekuwa na muda wakupoteza" usitupotezee muda na kutuwekea visingizio vya kuwalinda hao usiotaka tuwatoe madarakani. Ni lazima tuwe na mahali pa kuanzia, na kwenda kupiga kura ni sehemu mhimu ya kianzio cha mengine inapolazimu.
Watu kama nyinyi wanawapenda sana.
"Wajinga" ni wasiotambua wajibu wao katika taifa lao na ndio inaowahitaji sana CCM. Watu ambao hawjui kwamba kura zao zina thamani kubwa na zinatakiwa ziwe ndizo mwamuzi wa mtu anayetakiwa kuwaongoza.Wajinga wa kwenda kusimamishwa kwenye mstari kwa kura za kiini macho hawapo tena zama hizi.
"Wajinga" ni wasiotambua wajibu wao katika taifa lao na ndio inaowahitaji sana CCM. Watu ambao hawjui kwamba kura zao zina thamani kubwa na zinatakiwa ziwe ndizo mwamuzi wa mtu anayetakiwa kuwaongoza.
Siku zote CCM inawataka sana watu hao. Na ndio maana wanasema 'CCM itatawala milele', kwa sababu inajua wajinga hao wapo wengi nchi hii.
Hao wapinzani tuliokuwa tunawapambania si ndio hao hao walituletea Lowassa toka ccm na sasa karudi tena ccm? Hao wapinzani si ndio hao tulipambana kupiga kura na kuzilinda kisha wakaenda kuunga mkono juhudi? Sasa kama tunatake risk na bado wapinzani wanatuletea wanaccm na wengine wanarudi ccm kuunga mkono juhudi, tupige kura ili iweje kwa mfano.
Huu ni ushauri konki kabisa wala si wakipuuzi!Kwanza niseme kabisa huu ushauri leo hii unaweza ukawa ni wa kipuuzi. Kwa sababu kuu kadhaa.
1. Mwaka 2020 utakuwa mwaka mbaya sana kwa wapinzani kweli kweli. Achana na wale vibaraka.
Asilimia kubwa hawatarudi hata list yao ipo na wengine kwa kugundua hili waliamua kuhamia CCM ili waweze pata riziki yao ya kila siku.
Tumeona maeneo ambayo Mh. Ametembelea pasipo unafiki akibagua walio chagua upinzani na waliochagua CCM.amesema kama una torch ukachanganya batteries na gunzi itawaka? Haiwaki.kaongea ukweli.
Kwa point hii tu wapinzani wanapitaje? Umeona maeneo ambayo amekuta wamechagua wapinzani alivyokuwa akiwajibu?lakini yeye si ndo analipa watendaji,wakurugenzi,anachagua wanahusika na uchaguzi?
WITO WANGU.
Mwaka 2020 mwachieni yeye agombee na wabunge wake. Kawaida dhambi ya Ubaguzi kama mtu anayo haitakosekana.atagundua wote ni CCM.na kuna maeneo mengi hatakuwa ametimiza ahadi.atatafuta namna ya kuwabagua.
Itafahamika kuna CCM Mag na CCM Asili. Hapo wapinzani kaeni pembeni muwe mnachochea tu moto.maana atakuja sema sehemu mmemchagua CCM mbunge lakini hafai.
Kawaida ya Ubaguzi upo kama pia. Yaani unaanzia juu kukubwa unashuka chini kudogo.level ya juu iliyopo sasa hivi ni CCM vs Upinzani. Ukiondoa Upinzani itakuwepo CCM yenyewe kwa yenyewe. Na hapo watu watakulana kwa misingi flani flani. So CCM yenyewe haitobaki salama.
Ushauri wangu wa kipuuzi kaeni chini mfikiri namna gani ya kujipanga kisayansi zaidi. Kuna kipindi semeni "sisi yetu macho tu"
"Siku watu wakigundua Adui yao Halisi ni nani Ukombozi utapatikana"
Huu ni ushauri konki kabisa wala si wakipuuzi!
Wapinzani ambao sio mapandikizi wasipoteze hela za kugombea na kufanya kampeni. Wakishachukua kiinua mgongo watafute shughuli nyingine za kufanya, wakae pembeni wamuachie chama chake na Bunge lake. Halafu tuone atakapotufikisha kimaendeleo
Kwa ushauri huu mlinitukana wana Chadema. Naona nlichoshauri ndicho Chadema walichoamua leo. Kutoshiriki Uchaguzi.
Mkuu labda wewe ndiye mkono wa kushoto wa Mh.Mbowe na kamati yake.Walikuwa wananikashifu kwa huu ushauri toka mwanzo.leo wamefanya yale yale nliyoyasema.